Kwa Babu wa Loliondo

Kwa Babu wa Loliondo

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
38,562
Reaction score
48,911
Kwa wale mliokwenda,

Mkanywa DAWA,

Mkapona kweli,

Huu ni wasaa wenu kudhihirishia ulimwengu kua Yaliyokuwepo ndio yenyewe.
 
mama yangu mdogo baada ya kunywa kikombe alipoteza uhai wake
 
duh story ninazozipata wengi wamekufa sana...r.i.p
 
hivi babu mwenyewe yupo...na kikombe anatoa au?
 
Kuna mtu alisema ilikuwa kuhamisha mawazo ya watu kwenye agenda zilizokuwepo wakati huu, tunahitaji shujaa kama yeye kuhamisha watu kwenye masuala ya katiba pendekezwa kwa sasa maana majibu kwa sasa yako ndivyo sivyo
 
Ukisema walikufa ina maana dawa yake ndio iliuwa au wao walikufa kwaa maradhi. Mwili ukishaugua mwisho ni kifo maana roho ya Mungu haikai kwenye hekalu dhaifu.Inasepa zake.
 
Nikikumbuka huwa nasikitika sana,hivi tuna wizara ya afya yenye wasomi,hivi tuna maabara za utafiti wa madawa ya binadamu,vyuo vikuu vyetu vina watafiti wa madawa ?hivi hii NIMR(national institute of medical research)ipo ?,Babu kawapoteza wengi,Mama yangu mdogo alikuwa na kansa ya kizazi kwa miaka 4,alipoenda kwa babu kanywa kikombe kaamini amepona kaacha kutumia dawa,alifariki gafla kwenye basi njiani akitoka moshi kuja Dar es salaam
 
R . I .P MZEE SUNGURA ulienda kwa babu ukizan utapona kumbe ndio ilikuwa ndio safari yk ya mwishoo daaaaaaaa
 
Nilipata dili ya kupeleka wazee wa 3 na wake zao.
Amebaki mmoja tu.(bila mke)
Nilirudi na magadi mengi
Nina kumbu kumbu ya magadi mengi nilirudi nayo.
of coz na mimi nilikunywa.
 
Kwa wale mliokwenda,

Mkanywa DAWA,

Mkapona kweli,

Huu ni wasaa wenu kudhihirishia ulimwengu kua Yaliyokuwepo ndio yenyewe.

Sidhani Kama Wapo Hai Mkuu Kwani Nijuavyo Karibia Wote Wameshakufa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom