Kwa ambao bado wana imani na pinda

jamani kuna ubaya gani kwa mtu kama pinda kuwa na tuvibasi kama vya sumry, mbona kuna watu wajingawajinga tu wanamiliki mabasi kibao..acheni wivu wa kijinga
 
Mimi bado nina imani na mtoto wa mkulima Mhe Pinda tena nina imani kwa hili hawezi kunyamaza atajibu tuu .ebu tumpe muda afikirie cha kujibu.Aisee kama unataka kupata ugonjwa wa moyo na kufupisha umri wa kuishi hapa duniani ebu endelea kudadisi mali hii ni ya nani...maana walionazo wengi siyo wenyewe.

Mimi naamini mtoto wa mkulima kwa ustaharabu kabisa atasimama na kujibu ili wananchi tupate umri wa kuishi...unajua ukiendelea kudadisi kuwa mali hii ni ya nani au kampuni hii ni ya nani unaweza kufupisha siku za kuishi hapa chini a jua toka miaka 10 hadi mwezi mmoja?...si mmesikia kuwa issue za Rais au waziri mkuu huwa hazijadiliwi? sina hakika kama kuna mtu wa kumkanya Rostam,karamagi au Lowassa maana jeuri yao ya pesa inatisha

ebu mpeni muda mtoto wa mkulima atajibu kuwa si mali yake ila amewekeza kwa ajili ya wajukuu zake na vitukuu vyake ndiyo maana hajawahi kutaja kuwa ana mali au hisa na Sumry.
Mzee Mafwili
 
Back
Top Bottom