Kuwategemea Manabii Ni Ibada Ya masanamu

Kuwategemea Manabii Ni Ibada Ya masanamu

Kasiano Muyenzi

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2018
Posts
13,972
Reaction score
22,922
Yesu hakuahidi kututumia manabii kwa mwongozo wa maisha. Yesu aliahidi kututumia Roho Mtakatifu ili atuongoze (Yohana 14:16-18).

Chini ya Agano la Kale, Mungu alizungumza zaidi kupitia manabii kwa sababu Roho wa Mungu alikuwa ndani yao. Katika kipindi kipya cha neema, Roho Mtakatifu yuko ndani ya kila aliyemwamini Yesu Kristo.

Katika historia ya kanisa, nabii yeyote wa kweli anaelekeza watu kwa Yesu. Hakuna mtu wa kweli wa Mungu anayeelekeza watu kwake. Manabii wa kweli wanataka kila mtu asitawishe uhusiano wa kibinafsi na Yesu.

Imeandikwa "Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu" 1 Tim 2:5.

Ninaamini katika kuomba pamoja na kuombeana. Lakini mtu yeyote anayekuambia kwamba lazima akuombee ili Mungu akujibu maombi yako ni nabii wa uongo. Manabii wa uwongo huunda ugonjwa wa utegemezi.

Uwe makini
1675574694776.jpg
 
Mt Fransisko wa Asis alifundisha kuwa ni heri zaidi kutoa kuliko kupokea!
JK II aliwahi kisema: ukila vya watu nawe kubali kuliwa walau kidogo.

Najiuliza ilikuaje Mch Munisi akakubali kupokea gari licha ya kuwa anayo magari lakini hataki kutimiza masharti ya msaada huo?
 
Mt Fransisko wa Asis alifundisha kuwa ni heri zaidi kutoa kuliko kupokea!
JK II aliwahi kisema: ukila vya watu nawe kubali kuliwa walau kidogo.

Najiuliza ilikuaje Mch Munisi akakubali kupokea gari licha ya kuwa anayo magari lakini hataki kutimiza masharti ya msaada huo?
Hakujua kuwa ni msaada wenye masharti. Sasa baada ya nabii kuonyesha sura yake halisi kwa Munisi kwamba huo msaada sio wa hivi hivi tu, anapaswa arudi kwa nabii kumshukuru nabii mkuu.

Hapo ndipo alipogoma, binafsi namuunga mkono, arudishe tu huo msaada wa masharti.
 
Sasa kama watu hawafundishwi kumjua roho mtakatifu na nguvu zake makanisani mwao ni rahisi kutekwa na manabii feki. Watandanganyika sana mpaka akili ziwakae sawa. Wachungaji wao ndio chanzo cha waumini kuzurura hovyo kutafuta malisho bora
 
Hakujua kuwa ni msaada wenye masharti. Sasa baada ya nabii kuonyesha sura yake halisi kwa Munisi kwamba huo msaada sio wa hivi hivi tu, anapaswa arudi kwa nabii kumshukuru nabii mkuu.

Hapo ndipo alipogoma, binafsi namuunga mkono, arudishe tu huo msaada wa masharti.
Fuatilia pia issue ya Askofu mstaafu Koda aliyekuwa Askofu wa Same
 
Sasa kama watu hawafundishwi kumjua roho mtakatifu na nguvu zake makanisani mwao ni rahisi kutekwa na manabii feki. Watandanganyika sana mpaka akili ziwakae sawa. Wachungaji wao ndio chanzo cha waumini kuzurura hovyo kutafuta malisho bora
Hii ni kweli kabisa, wachungaji wa siku hizi hawajui kulisha kondoo
 
Manabii ni wapigaji sana na wahanga ni WA awake.
Japo kuna wahanga wanaume pia, Ila wanawake ni wengi zaidi na ndio wateja wakubwa wa chupi, maji, mafuta, vitambaa na vitu vingine viuzwavyo na manabii.
 
Yesu hakuahidi kututumia manabii kwa mwongozo wa maisha. Yesu aliahidi kututumia Roho Mtakatifu ili atuongoze (Yohana 14:16-18).

Chini ya Agano la Kale, Mungu alizungumza zaidi kupitia manabii kwa sababu Roho wa Mungu alikuwa ndani yao. Katika kipindi kipya cha neema, Roho Mtakatifu yuko ndani ya kila aliyemwamini Yesu Kristo.

Katika historia ya kanisa, nabii yeyote wa kweli anaelekeza watu kwa Yesu. Hakuna mtu wa kweli wa Mungu anayeelekeza watu kwake. Manabii wa kweli wanataka kila mtu asitawishe uhusiano wa kibinafsi na Yesu.

Imeandikwa "Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu" 1 Tim 2:5.

Ninaamini katika kuomba pamoja na kuombeana. Lakini mtu yeyote anayekuambia kwamba lazima akuombee ili Mungu akujibu maombi yako ni nabii wa uongo. Manabii wa uwongo huunda ugonjwa wa utegemezi.

Uwe makini View attachment 2506871


YEREMIA 17:5
"BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA."
 
YEREMIA 17:5
"BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA."
Mama D Umeua watu kwa hii nyundo ✔️🙏
 
Mama D Umeua watu kwa hii nyundo ✔️🙏

Kumbukumbu la Torati 13:1-2
“Akitokea nabii au mtabiri wa ndoto miongoni mwenu, akawaahidi na kuwapa ishara au maajabu fulani, halafu ishara au maajabu hayo yatokee, kisha aseme: ‘Tufuate miungu mingine na kuitumikia, (miungu ambayo hamjapata kuijua)"
 
Huyo jamaa sijui nabii first mbona kama huwa anajichubua maana rangi haieleweki iyo sijui mwekundu.
 
Mama D Umeua watu kwa hii nyundo ✔️🙏

Kuna watu wanafikiri kwa Mungu ni lelemama.

Yaani wewe ufanikiwe tuu kwa miujiza bila kufuata sheria za Mungu, bila kujali na kuomba....Thubutu

Watumishi wa Mungu wanatuongoza njia sahihi ya sisi kupita kufika kwa tunakotaka, sio wapite wao afu wewe ufike!

Hakuna vishoka kwenye kutafuta baraka!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom