Kuwa na uwezo wa kujitegemea ni muhimu kuliko utajiri

mwehu ndama

JF-Expert Member
Nov 12, 2019
543
1,874
Leo nimeona nishiriki nanyi katika darasa hili huru enyi vijana wa enzi hii ya bibi kizimkazi, Naam!!, nisikilizeni nyinyi nyote mnaoteswa na kusononeka juu ya maisha ya kifahari ya watu wengine.

Maisha yetu katika nyakati za sasa yamejawa na ushindani mkubwa tena wa hovyoo na usio na tija hasa kutokana na ukuaji wa teknolojia, watu wamebadilisha dhana zao za mafanikio ya kimaisha kwa kujilinganisha na mfumo wa maisha ya watu wengine, mfano kuangalia wanachokula, wanachovaa, wanachoendesha na wanapolala bila kujifanyia tathimini binafsi na kukubaliana na ukweli kwamba hata walipofika kwa sasa pia ni mafanikio tosha kulinganisha na walipotoka

Jinamizi hili la kuishi ndani ya ndoto za watu wengine linatesa sana, litakufanya upoteze hata kile kidogo ulichonacho kwa kukimbilia vikubwa ili uishi kama wao, na katika nyakati kadhaa utapata upofu na hutoziona fursa ndogo ndogo zilizokuzunguka ambazo pia zingekuvusha taratibu kwa haraka ya kuwa kama hao uwaonao tik tok, instagram na marafiki waliokuzunguka.

Binafsi nayatazama mafanikio ya kimaisha katika mlengo wa mtu kuwa na uwezo wa kujitegemea kimahitaji pasipo kuwa mzigo kwa mtu mwingine, na hapa mahitaji yako nilazima yaendane sawa sawa na kile kinachoingia mfukoni mwako wew.
Ni upumbavu mkubwa, tena ni uhayawani ulio tukuka kwa kijana ambae hujawah hata kujilipia kodi wala kujihudumia kimatibabu, chakula na mavazi kuanza kutamani utajiri na maisha ya kifahari huku ukiwa juu ya kochi la nyumbani kwa shemeji na remote mkononi.

Ewe kijana, Pambana kwanza uweze Kujitegemea, utajiri na ufahari sio wote tutakao vipata ingawa wote tuna nafasi sawa ya kuvipata, ila katika hilo heshimu sana msingi wa kipato chako cha sasa na kamwe usiwe mwepesi wa kuacha shughuli yako hiyo kwa kukimbilia utajiri wa haraka haraka sababu utakapoanguka, anguko hilo huwa baya sana na utatamani walau upate hata nusu ya unachokipata sasa.

Kujitegemea ni raha sana, ni hatua nzuri sana katika maisha kabla ya kuwaza utajiri hakikisha una maintain hiyo hali ya kujitegemea mpaka kifo chako bila kujali kiasi cha kipato chako, hakikisha unakuwa mashindani wa hatua zako mwenyewe na hakika utapiga hatua kubwa bila masononeko!

Vijana tupambanie kujitegemea na sio utajiri
 
Hutakiwi kabisa kujifananisha na watu wengine maana hili ni kosa, kujifananisha huzaa tamaa, chuki, husda na hupelekea kukata tamaa nk...hivi usipime juhudi zako na za watu wengine pima juhudi na mafanikio yako Kwa kuangalia ulipotoka na namna gani utaweza kuhimili uzito wa huko unapokwenda, watu unaotaka kupimana nao ubavu, nguvu, mashindano hujui wamepata vitu vyao kutokea wapi, Kwa njia gani na maarifa yapi hili ni muhimu sana Kwa kijana hasa anayejitafuta katika suala zima la kufanikisha ndoto zake.
 

Ushauri mzuri sana kwa vijana, natamani kila mtu angewaambia vijana habari kama hizi. Vijana wana magonjwa kwa kujilinganisha na watu wanaowaona kwenye mitandao na hata baadhi ya marafiki zao wenye maisha ya juu. Kijana anapata kazi leo na anatamani aanze kuishi kama boss wake leo leo.

Kuna vijana hadi unatamani kuwashauri waachane na mitandao ya kijamii kwa jinsi inavyowapa presha.
 
Leo nimeona nishiriki nanyi katika darasa hili huru enyi vijana wa enzi hii ya bibi kizimkazi, Naam!!, nisikilizeni nyinyi nyote mnaoteswa na kusononeka juu ya maisha ya kifahari ya watu wengine.

Maisha yetu katika nyakati za sasa yamejawa na ushindani mkubwa tena wa hovyoo na usio na tija hasa kutokana na ukuaji wa teknolojia, watu wamebadilisha dhana zao za mafanikio ya kimaisha kwa kujilinganisha na mfumo wa maisha ya watu wengine, mfano kuangalia wanachokula, wanachovaa, wanachoendesha na wanapolala bila kujifanyia tathimini binafsi na kukubaliana na ukweli kwamba hata walipofika kwa sasa pia ni mafanikio tosha kulinganisha na walipotoka

Jinamizi hili la kuishi ndani ya ndoto za watu wengine linatesa sana, litakufanya upoteze hata kile kidogo ulichonacho kwa kukimbilia vikubwa ili uishi kama wao, na katika nyakati kadhaa utapata upofu na hutoziona fursa ndogo ndogo zilizokuzunguka ambazo pia zingekuvusha taratibu kwa haraka ya kuwa kama hao uwaonao tik tok, instagram na marafiki waliokuzunguka.

Binafsi nayatazama mafanikio ya kimaisha katika mlengo wa mtu kuwa na uwezo wa kujitegemea kimahitaji pasipo kuwa mzigo kwa mtu mwingine, na hapa mahitaji yako nilazima yaendane sawa sawa na kile kinachoingia mfukoni mwako wew.
Ni upumbavu mkubwa, tena ni uhayawani ulio tukuka kwa kijana ambae hujawah hata kujilipia kodi wala kujihudumia kimatibabu, chakula na mavazi kuanza kutamani utajiri na maisha ya kifahari huku ukiwa juu ya kochi la nyumbani kwa shemeji na remote mkononi.

Ewe kijana, Pambana kwanza uweze Kujitegemea, utajiri na ufahari sio wote tutakao vipata ingawa wote tuna nafasi sawa ya kuvipata, ila katika hilo heshimu sana msingi wa kipato chako cha sasa na kamwe usiwe mwepesi wa kuacha shughuli yako hiyo kwa kukimbilia utajiri wa haraka haraka sababu utakapoanguka, anguko hilo huwa baya sana na utatamani walau upate hata nusu ya unachokipata sasa.

Kujitegemea ni raha sana, ni hatua nzuri sana katika maisha kabla ya kuwaza utajiri hakikisha una maintain hiyo hali ya kujitegemea mpaka kifo chako bila kujali kiasi cha kipato chako, hakikisha unakuwa mashindani wa hatua zako mwenyewe na hakika utapiga hatua kubwa bila masononeko!

Vijana tupambanie kujitegemea na sio utajiri
Hiki ndio kitu ninacho akilini mwangu....maswala ya utajiri sijawahi kufikiria kichwani kwangu zaidi ya kujitegemea kimaisha kwa mahitaji ya msingi tu.
 

Ushauri mzuri sana kwa vijana, natamani kila mtu angewaambia vijana habari kama hizi. Vijana wana magonjwa kwa kujilinganisha na watu wanaowaona kwenye mitandao na hata baadhi ya marafiki zao wenye maisha ya juu. Kijana anapata kazi leo na anatamani aanze kuishi kama boss wake leo leo.

Kuna vijana hadi unatamani kuwashauri waachane na mitandao ya kijamii kwa jinsi inavyowapa presha.
Sahihi,kabisa, ni stress za kujitakia kuwa na ndoto za kumiliki nyumba ya kifahari ikiwa hujaamua hata kutoka kwenu
 
Hiki ndio kitu ninacho akilini mwangu....maswala ya utajiri sijawahi kufikiria kichwani kwangu zaidi ya kujitegemea kimaisha kwa mahitaji ya msingi tu.
Mimi ndio vita kuu niliyonayo sasa, kuanza kuhakikisha sipotezi hiki kidogo nachoingiza kivyovyote, kabla ya kutoka kutafuta kingine, hii tunaita defensive lifestyle
 
As long as ninaweza Kula asubuhi tu supu nzito ,chapati kubwa mbili ,maji ya baradi ya uhai ,Bando likiwa full ....Kwa pesa zangu mwenyewe Bila kumpigia goti kiumbe yeyote....nimeshatoboa maisha
 
As long as ninaweza Kula asubuhi tu supu nzito ,chapati kubwa mbili ,maji ya baradi ya uhai ,Bando likiwa full ....Kwa pesa zangu mwenyewe Bila kumpigia goti kiumbe yeyote....nimeshatoboa maisha
Huo ni ushindi tosha kaka, kazia hapo hapo mengine yatakuja by default
 
Ubarikiwe mkuu somo zuri sana nakumbuka ujanani ilikuwa shida sana kuweka akiba lakini kwa sasa ni Torati. Kujitegemea ni raha unajiamini unakuwa na kiburi flani kwamba huwezi kuwa Chawa. Daima Mtegemee Mungu Binadamu Hufa
 
Back
Top Bottom