Tzhacker 000
JF-Expert Member
- Dec 11, 2017
- 659
- 690
Utapeli ni tatizo kubwa sana kwa kila mtu,hasa mtumiaji wa mtandao, huenda wewe ushawahi kukutana na aina fulani ya utapeli.
Kuna aina nyingi sana za utapeli wa kimtandao, leo tutaona baadhi tu na shuhuda mojawapo.
1. KUPIGIWA SIMU NA WATOA HUDUMA WAONGO
Hii imetokea watu wengi sana,unapigiwa simu na mtu anaejitambulisha kuwa anatoka kwenye kampuni za simu kama Tigo, Vodacom au Airtel unaambiwa kuna bonasi umepewa,lakini unatakiwa kutaja jina lako kamili, umri na kiasi cha pesa ulichonacho, basi hapo mtaongea kwa kirefu lakini utaambiwa kabla hujatumiwa pesa tuma kiasi fulani kwanza kwenye namba atakayokupa, lakini pale utakapotuma basi na ndio mwisho wa mawasiliano na hutompata tena.
2.KUPATA RAFIKI MTANDAONI
Wale wapenzi wa Facebook ndio wahanga wengi katika hili,kama ni binti au kijana atakuja rafiki wa jinsia tofauti na wewe.
Cha kwanza kabisa atakuamisha toka Facebook na kutaka muwasiliane kwa barua pepe,huko atakupa historia yake na utajiri aliokua nao baba yake,akijifanya kuwa ni mkimbizi na hana wazazi,anaishi ukimbizini lakini ana akiba ya pesa alizowekewa na baba yake toka mdogo.
Na hapo akukutajia kiasi kikubwa sana,ila anataka ombi moja tu kwako,atoke kambini aje uraiani na kama utafanikisha mtakuja kuwa pamoja au kama umeowa/kuolewa atakulipa kiasi fulani cha pesa,mtatua muda sana kuwasiliana mpaka kuja kuhitaji pesa yako.
ili aendeshe kesi za mirathi na malipo kwa mawakili, kama utakuwa na tamaa ya uhitaji wa hizo pesa mwisho wa siku utapigwa wewe.
3.KUJISHINDIA ZAWADI FULANI TOKA NJE YA NCHI.
Huu ni wizi mpya ambao ndio unaotumika sana, cha kushangaza unaweza kuambiwa umeshinda pesa nyingi sana wakati hajawahi cheza mchezo wowote mtandaoni. Ila sharti lao tuma majina yako kamili,namba yako ya simu, mwaka uliozaliwa kwa kutumia barua pepe. Hapo ukituma hayo maelezo nirahisi mtu kukujua kiundani na unampa njia rahisi ya kukufanyia utapeli.
Habari Leo