Katika utawala wa Awamu ya 3 zilizokuwa nyumba za serikali nchini ziliuzwa kwa mizengwe kwa bei ya chini sana ukilinganisha thamani halisi ya nyumba na viwanja vyake.
Kuna nyumba zilizokuwa katika viwanja vikubwa kiasi kwamba walionunua waliweza kujenga nyumba nyingine hadi tatu au kuweka majengo ya milango ya biashara yenye milango isiypungua 10 bila kuingilia nyumba iliyokuwepo.
Hakukuwa na sababu hasa ya msingi iliyosukuma nyumba zile kuuzwa zaidi ya ubinafsi wa viongozi hasa katika baraza la mawaziri kwa kutamani ulaji ule .
Kutokea wakati ule watumishi wa serikali wenye hadhi ya kupewa nyumba wamekuwa wakitumia mabilioni ya fedha kwa ajili ya kulala katika hotel za gharama kubwa badala ya fedha hizo kufanya shughuli za wananchi kama vile huduma za shule, maji au afya.
Zoezi hili la uuzwaji wa nyumba za serikali lilikuwa la kiharamia lililoacha maswali mengi ambayo hadi leo yanaulizwa. Mfano mmoja kuna nyumba ziliuzwa zikiwa zinamilikiwa na Jeshi la polisi zilikuwa mita tano kutoka vituo vya polisi na walionunua kwa sasa walishastaafu kazi hivyo unakuta zinakaliwa na raia wa kila aina wazuri na wabaya.
Nina mifano hai mingi ya madhara yanayoendelea kutokana na kadhia hii, namuomba mhe. na wah.wanaomsaidia waone hili jipu na KULITUMBUA ninafahamu gharama za kurejesha siyo kubwa kwani wanunuzi walizuiwa kuziendeleza kwa mda mrefu abao haujaisha. Ingawa ktk utawala wa JK wanunuzi wameendeleza sana majengo na viwanja vyake.
Sasa kama na mh. JPM anahuska sijui itakuwaje. mmmh. asante.
Kuna nyumba zilizokuwa katika viwanja vikubwa kiasi kwamba walionunua waliweza kujenga nyumba nyingine hadi tatu au kuweka majengo ya milango ya biashara yenye milango isiypungua 10 bila kuingilia nyumba iliyokuwepo.
Hakukuwa na sababu hasa ya msingi iliyosukuma nyumba zile kuuzwa zaidi ya ubinafsi wa viongozi hasa katika baraza la mawaziri kwa kutamani ulaji ule .
Kutokea wakati ule watumishi wa serikali wenye hadhi ya kupewa nyumba wamekuwa wakitumia mabilioni ya fedha kwa ajili ya kulala katika hotel za gharama kubwa badala ya fedha hizo kufanya shughuli za wananchi kama vile huduma za shule, maji au afya.
Zoezi hili la uuzwaji wa nyumba za serikali lilikuwa la kiharamia lililoacha maswali mengi ambayo hadi leo yanaulizwa. Mfano mmoja kuna nyumba ziliuzwa zikiwa zinamilikiwa na Jeshi la polisi zilikuwa mita tano kutoka vituo vya polisi na walionunua kwa sasa walishastaafu kazi hivyo unakuta zinakaliwa na raia wa kila aina wazuri na wabaya.
Nina mifano hai mingi ya madhara yanayoendelea kutokana na kadhia hii, namuomba mhe. na wah.wanaomsaidia waone hili jipu na KULITUMBUA ninafahamu gharama za kurejesha siyo kubwa kwani wanunuzi walizuiwa kuziendeleza kwa mda mrefu abao haujaisha. Ingawa ktk utawala wa JK wanunuzi wameendeleza sana majengo na viwanja vyake.
Sasa kama na mh. JPM anahuska sijui itakuwaje. mmmh. asante.