Elections 2015 Kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma: Mwigulu Nchemba atangaza nia kugombea Urais

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,020
144,377
Sasa ni zamu ya Mwigulu Nchemba na anatarajia kutangaza nia kuanzia saa 9 mchana wa leo na atafanya hivyo live kupitia star tv akiwa Chuo cha Mipango, Dodoma.

Muda: saa 9 Alasiri hadi Saa 12 Jion.
Mahali: Chuo cha Mipango Dodoma.
Ukumbi: Mwl. Nyerere Hall

KAULI MBIU YA MWIGULU: MABADILIKO NI VITENDO, WAKATI NI SASA

Mwigulu anadai alibeba zege baada ya kumaliza chuo kikuu na mke wake akiwa mama ntilie akiwapikia yeye na vibarua wengine wa ujenzi.

Pia naona Mwigulu anamponda EL kiani kwa kusema watu wanajisifu kuwa wamekuwepo serikalini muda mrefu wakati huo huo wamelisababishia Taifa hasara kubwa katika muda huo mrefu waliokaa serikalini.

Inasikitisha kumuona analalamikia mambo mengi yanayoendelea chini ya serikali hii ya CCM wakati kila siku wanawakejeli wapinzani wanapolalamikia na kuhoji mambo hayo Bungeni.

Kwa kifupi,Mwigulu leo anaivua nguo CCM hadharani na zaidi leo anamponda kiana mh.sana na pia anaonyesha kuwa Mkulu na chama chake wamekuwa ni dhaifu.

 

Attachments

  • 20150531_161615.jpg
    20.5 KB · Views: 3,782
Mwigulu Nchemba Leo anatarajia kutangaza nia ya Urais katika ukumbi wa Nyerere hall chuo cha Mipango Dodoma, nitakuwa natoa updates kwa kinacho endelea kwenye ukumbi huu wa Nyerere hall chuo cha Mipango.
 
Naona hii sasa imekuwa ndio fashion na utamaduni kwa wana-CCM wanaosaka uraisi.

Muda huu ninapoandika kuna magari aina ya coaster yamekodishwa ili kubeba wanafunzi wa chuo kikuu na kuwapeleka Chuo cha Mipango Dodoma kwenye tukio la Mwigulu kutangaza nia.

Nasikitika kuona hata wanafunzi wa vyuo vikuu nao hawajitambua!

Binafsi nimebaki naangali tu tukio hili nikiwa kwenye gate kubwa la kuingilia na kutoka hapa chuoni.
 
Kakodi mengi sana kwa kweli naona yamejaa hapa UDOM na wanafunzi wanazidi kumiminika kuingia kwenye gari.

Nchi hii ni shidaaaaa!!!!!
 
mkuu na wewe si uko hiko chuo tunategemea update kutoka kwako
 
Karibu sana mwigulu.ila Mimi naamini unajitengenezea crblty kwa ajili ya baadae.ki ukweli kwa sasa uwezi unamabifu.ya ajabu AF kama dikteta flan.ila unafanya Sana'a yako vizuri.keep it up...
 
Hivi jana mbona star tv hawakurusha live wakati lowassa anatangaza nia?
 

Mkuu hapo ndo utajua ni kwa kiasi gani wasomi wa Tanzania wanavyotumika kuzuia mabadiliko ya kweli kwenye nchi hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…