Kutoa nyongo

snochet

JF-Expert Member
Mar 31, 2011
1,407
1,110
eti wadau,nina haka kaswali kangu kadogo,kuna watu wana katabia ka kuchokonoa koo hasa wakiwa wanapiga mswaki,ivi hii kitu ina madhara kiafya?
 
eti wadau,nina haka kaswali kangu kadogo,kuna watu wana katabia ka kuchokonoa koo hasa wakiwa wanapiga mswaki,ivi hii kitu ina madhara kiafya?
njia nzuri zaidi ya kutuliza nyongo ni kunywa glasi mbili za maji ya vuguvugu asubuhi nusu saa kabla ya kula kitu chochote au kunywa nusu kikombe cha aloe vera(shubiri) asubuhi ukiamka na usiku nusu saa kabla ya kula.
 
nimekusoma,lakini je kutoa huko kwa nyongo kuna madhara yoyote kiafya?
 
Sijui mnamaanisha nini mkisema 'kutoa nyongo', lakini kama mnazungumzia nyongo ninayoijua mimi kisayansi...haitolewi kwa mswaki wa koo wala kunywa maji ya vugu vugu!

Nyongo (bile) inahifadhiwa kwenye mfuko maalum tumboni (gall bladder) ambao umejishikiza karibu na ini tumboni huko. Una kimrija (bile duct) ambacho kinaconnect na utumbo mdogo sehemu inayoitwa duodenum, hivyo nyongo humwagwa kwenye utumbo mdogo ambapo husaidia kwenye umeng'enyuaji wa vyakula vyenye asili ya mafuta (emulsification of fat), ziada iantoka kwenye haja kubwa (ndiyo inayoipa haja kubwa rangi ya kimanjano au brownish).

Sasa hicho mnachoongelea hapo hakina uhusiano wowote na nyongo. unapochokonoa koo na mswaki unapata 'gag reflex' (ile kama unataka kutapika) ambacho sio kitu kizuri...pia koo lina ngozi laini hivyo waweza lichubua, na kwa sababu mdomo ni mchafu (kuna bacteria hata ukipiga mswaki mara kumi kwa siku), wale bacteria wanaweza ingia kupitia kidonda na hivyo kupata infection ya tonsils (Tonsilitis), na mbaya zaidi infection inaweza fikia kwenye moyo (especially kwa watu wenye matatizo ya moyoy already) ukapata tatizo la hatari linaloitwa 'bacterial endocarditis'.

Kuchokonoa koo hakuna faida yeyote.
 
thanx kwa ufafanuzi huu makini
Sijui mnamaanisha nini mkisema 'kutoa nyongo', lakini kama mnazungumzia nyongo ninayoijua mimi kisayansi...haitolewi kwa mswaki wa koo wala kunywa maji ya vugu vugu!

Nyongo (bile) inahifadhiwa kwenye mfuko maalum tumboni (gall bladder) ambao umejishikiza karibu na ini tumboni huko. Una kimrija (bile duct) ambacho kinaconnect na utumbo mdogo sehemu inayoitwa duodenum, hivyo nyongo humwagwa kwenye utumbo mdogo ambapo husaidia kwenye umeng'enyuaji wa vyakula vyenye asili ya mafuta (emulsification of fat), ziada iantoka kwenye haja kubwa (ndiyo inayoipa haja kubwa rangi ya kimanjano au brownish).

Sasa hicho mnachoongelea hapo hakina uhusiano wowote na nyongo. unapochokonoa koo na mswaki unapata 'gag reflex' (ile kama unataka kutapika) ambacho sio kitu kizuri...pia koo lina ngozi laini hivyo waweza lichubua, na kwa sababu mdomo ni mchafu (kuna bacteria hata ukipiga mswaki mara kumi kwa siku), wale bacteria wanaweza ingia kupitia kidonda na hivyo kupata infection ya tonsils (Tonsilitis), na mbaya zaidi infection inaweza fikia kwenye moyo (especially kwa watu wenye matatizo ya moyoy already) ukapata tatizo la hatari linaloitwa 'bacterial endocarditis'.

Kuchokonoa koo hakuna faida yeyote.
 
duh umetufahamisha,wengi tulikuwa tunajua unatoa nyongo kwa staili hyo ya kupiga mswaki kwenye koo
 
Back
Top Bottom