Halmashauri nyingi za Mikoa ya Kusini zinategemea ushuru wa mazao mbali mbali kama chanzo yamapato ya ndani. Korosho ni zao moja ambalo lilikuwa linaziingizia Halmashauri fedha nyingi za ndani. Kwa mfumo wa ununuzi wa korosho wa msimu huu wa 2018/2019, Halmashauri zinaonekana zitakosa mapato yatokanayo ya ushuru katika zao hilo. Sababu kuu ni kwamba bei aliyotangaza bwana mkuwa ya 3,300/= italipwa kwa mkulim amoja kwa moja. Maana yake hatutakuwa na makato kwa ajili ya vyama vya msingi wala Halmashauri. Jambo hilo linaonesha Halmashauri nyingi zitayumba sana kwa huu. Hazitaweza kujiendesha.
Kuna Halmashauri moja ilitarajia kukusana takribani 2,700,000,000/= kwa mwaka 2018/2019 kati ya hizo takribani Tshs 1,800,000,000/= ilitegemewa ipatikane kutokana na uhuru wa korosho pekee. Pesa hiyo isipopatikana maana yake Halmashauri hiyo haitaweza kujiendesha. Mazao mengine ambayo yalitakiwa yachangie kwenye mapato ni pamoja na choroko na mbaazi ambayo hadi sasa hayana soko na wakulima ni kama wameacha kulima mazao hayo. Madiwani wa Halmashauri hiyo hawajalipwa posho zao za mwezi na zile za vikao vya kamati pamoja na baraza tangu Mwezi wa sita 2018. Sababu ni kwamba Halmashauri haina fedha za ndani za kulipa posho hizo.
Wanaomshauri Bwana mkubwa wangemuambia jambo hili ili ajue. vinginevyo Halmashauri nyingi za Kuisni hazitaweza kujiendesha kwa sababu hazitakuwa na fedha.
Kuna Halmashauri moja ilitarajia kukusana takribani 2,700,000,000/= kwa mwaka 2018/2019 kati ya hizo takribani Tshs 1,800,000,000/= ilitegemewa ipatikane kutokana na uhuru wa korosho pekee. Pesa hiyo isipopatikana maana yake Halmashauri hiyo haitaweza kujiendesha. Mazao mengine ambayo yalitakiwa yachangie kwenye mapato ni pamoja na choroko na mbaazi ambayo hadi sasa hayana soko na wakulima ni kama wameacha kulima mazao hayo. Madiwani wa Halmashauri hiyo hawajalipwa posho zao za mwezi na zile za vikao vya kamati pamoja na baraza tangu Mwezi wa sita 2018. Sababu ni kwamba Halmashauri haina fedha za ndani za kulipa posho hizo.
Wanaomshauri Bwana mkubwa wangemuambia jambo hili ili ajue. vinginevyo Halmashauri nyingi za Kuisni hazitaweza kujiendesha kwa sababu hazitakuwa na fedha.