Kusafirisha Wasomali

Emlth

Senior Member
Joined
Jan 26, 2022
Posts
128
Reaction score
193
Habari zenu wakuu.

Kuna jambo leo naomba kuskia kutoka kwenu, hasa wenye uzoefu na usafirishaji watu nchi moja kwenda nyengine.

Kuna kijiwe huwa nashinda mida ya jioni kupoteza muda baada ya mihangaiko ya siku, sasa kuna mabrother flani deal zao huwa ni kuwavusha wasomali kutoka tanzania kwenda zambia kama mjuavyo hapa mpakani tunduma na zambia tupo free tu kuingia nchi nyngne na kutoka pamoja na biashara bila bughudha yoyote

Sasa swali kubwa ni hili ,je wasomali hawaruhusiwi kuhama nchi au kutembelea nchi nyingine? maana hawa watu inasemekana wanasafirishwa kwa gharama kubwa kitu kinachoashiria pesa ya document haiwashindi na hata ukiwafumania ukapiga mkwara kukuachia laki kadhaa ni kawaida, sasa ni kipi hasa kinafanya wawe wanasafiri kimagendo?

Karibuni kwa mchango wenu
 
Inavyosemekana Somali pamoja na Ethiopia kupata vibari au paspoti ya kusafiria kwa vijana ni ngumu sana,sababu wanaitajika wakawe mstari wa mbele vitani kwa majeshi yao ya selikali zao,sasa imewekwe sheria ngumu kupata pasi za kusafiria
Kwa hiyo huwa wanaondoka bila vibari,lakini wengine wenye uwezo huwa wanatumia paspoti za Kenya na Tanzania
 
Bwana mdogo kama una wazazi na pia una ndugu wanaokupenda acha mara moja utawaumiza ukijiingiza huko.
 
Kusafiri ni asili ya msomali, roho ngumu vizazi na vizazi hata tukienda mbali kuzaliana na makabila mengine.
 
😂 ila wasomali wanapenda kuhama na kusafiri hawapendi kaa sehemu moj ukiona wamekaa sehemu sana ujue kuna pesa wanapata
Aisee we kademu kidogo nikutongoze. Kumbe ni wewe. Kwanini ulibadili ID lakini?
 

Hawa jamaa huwa wepesi KUJILIPUA ndio maana wanaogopeka
 
Inavyosemekana?
Kwa hiyo huna uhakika na unachoandika

Kwa taarifa yako Wasomali ni moto wa kuotea mbali
Wakitaka passport yeyote duniani wanapata na huko kwao wanapewa sana ila tatizo wakiingia hapa wanazificha na kupata vibali vya nchi husika ama bila permits wasije wakarudishwa tena Somalia au Ethiopia

Miaka ya 70 nakumbuka walikuwa wanakugongea visa kuwa uliingia nchi ambayo hujawahi kwenda ila muhuri umepigwa kuwa uliingia na kutoka

Yaani ukiomba visa nchi nyingine unapata maana passport inaonyesha wewe ni mtu wa masafari tu


Hiyo ni miaka 50 iliyopita

Ukitaka kusafiri popote hushindwi ukiweka nia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…