CCM katika jitihada zake za kuiteka Katiba wametumia mbinu ya kuwanyamazisha wanachama wao walio kwenye bunge la Katiba wametumia mbinu ya kulazimisha kura ya wazi.
Walichofanya CCM ni kuangalia mambo kwa mtazamo mfupi sana na hawakuzingatia matokeo ya baadae muda si mrefu. Wamesahau kuwa kuna mambo mawili ambayo walitakiwa kuyatilia maanani hasa kwa upande wa Zanzibar.
1. Wamesahau kuwa siku zote ushindi wao unakuwa wa mizengwe kule Zanzibar au tuseme ni ushindi kiduchu.
Sasa uwazi una maana kuwa wapiga kura kwenye chaguzi na wananchi kwa jumla watawajuwa nani na nani ndio "wasaliti" wa maoni ya Wazanzibari hivyo basi wanabidi wajitayarishe na kushindwa na kunyooshewa vidole na wakazi wenzao. Hali inakuwa mbaya zaidi kwa wale wa makundi maalum wataishi vipi mitaani?
2. CCM imezoea kuwanunua wapinzani na kwa kukabiliana na hili umoja wa UKAWA utawaagiza wanachama wake wote nao wapige kura za wazi ili kuzuia usaliti kwa kununuliwa na CCM. Kwa upande wa Zanzibar wale watu 16 walioelezwa na rais hawatoweza kununuliwa.
Nategemea kuwa hii kura ya wazi itakuwa ni chaguo la vyama vya upinzani ili kuonyesha mtizamo wao wa serikali tatu na kuwafanya watakaopiga kura ya siri kuonekana wasaliti.
Walichofanya CCM ni kuangalia mambo kwa mtazamo mfupi sana na hawakuzingatia matokeo ya baadae muda si mrefu. Wamesahau kuwa kuna mambo mawili ambayo walitakiwa kuyatilia maanani hasa kwa upande wa Zanzibar.
1. Wamesahau kuwa siku zote ushindi wao unakuwa wa mizengwe kule Zanzibar au tuseme ni ushindi kiduchu.
Sasa uwazi una maana kuwa wapiga kura kwenye chaguzi na wananchi kwa jumla watawajuwa nani na nani ndio "wasaliti" wa maoni ya Wazanzibari hivyo basi wanabidi wajitayarishe na kushindwa na kunyooshewa vidole na wakazi wenzao. Hali inakuwa mbaya zaidi kwa wale wa makundi maalum wataishi vipi mitaani?
2. CCM imezoea kuwanunua wapinzani na kwa kukabiliana na hili umoja wa UKAWA utawaagiza wanachama wake wote nao wapige kura za wazi ili kuzuia usaliti kwa kununuliwa na CCM. Kwa upande wa Zanzibar wale watu 16 walioelezwa na rais hawatoweza kununuliwa.
Nategemea kuwa hii kura ya wazi itakuwa ni chaguo la vyama vya upinzani ili kuonyesha mtizamo wao wa serikali tatu na kuwafanya watakaopiga kura ya siri kuonekana wasaliti.