Kura ya wazi itawaumbua CCM

Kura ya wazi itawaumbua CCM

Naona unakuja na hoja dhaifu sana tena sana unless unakusudia kuuendeleza uCCM!
Hivyo unafikiri sote tuna uwezo sawa wa kufikiri. Ni sawa uwezo wako wa kufikiri umekufanya uamini unavyoamini na mimi nina mtazamo tofauti wala usinione kuwa sina uelewa.
Hata hivyo ninachokieleza mimi ni kuwa huo uchaguzi wa CCM katika mfumo wa kupiga kura, kama walikusudia uwanufaishe basi wajitayarishe na upande wa pili wa shillingi yaani taathira mbaya kwa uamuzi wao.

Jee na wewe hujaelewa bado?

Nilichokuambia siyo swala la kujenga hoja bali ni ukweli wa hali ilivyo katika upigaji wa kura kwenye bunge Maalum.

Uchaguzi gani huo wa CCM na uamuzi upi huo unaodai wakati kuna upigaji kura wa aina mbili kwa sasa katika bunge la katiba?.

Mbunge akipenda wazi anapiga wazi na mwingine akipenda siri anpiga siri.
 
Nilichokuambia siyo swala la kujenga hoja bali ni ukweli wa hali ilivyo katika upigaji wa kura kwenye bunge Maalum.

Uchaguzi gani huo wa CCM na uamuzi upi huo unaodai wakati kuna upigaji kura wa aina mbili kwa sasa katika bunge la katiba?.

Mbunge akipenda wazi anapiga wazi na mwingine akipenda siri anpiga siri.

Naam hilo na liwe uamuzi wa kila mtu, lakini ni uamuzi utakaowagharimu hao walioshinikiza kura ya wazi. Kama utakuwa tayari kuchangia hoja zako kwa hilo karibu!
 
Mkuu, Kanuni za bunge la Katiba hazilamishi mbunge yoyote kupiga kura ya wazi au siri.

Kilichofanyika ni wabunge kupewa uhuru wa kupiga kura ya wazi kama anapenda au ya siri vile vile kama anapenda, kwa maana nyingine, kila kundi lilipata kile lilichokuwa likitaka kuhusiana na aina ya upigaji wa kura. Hakuna mbunge au kundi la wabunge kwa sasa limelazimishwa nje ya matakwa yake katika aina ya upigaji wa kura

Andiko lako linaonyesha wewe ndiyo hujafahamu kilichokubaliwa au unafahamu lakini unajaribu kupotosha wana Jf.

Ni angalizo tu.
“Hawawezi kupata theluthi mbili, sisi Wawakilishi na Wabunge kutoka vyama vya CUF na Chadema kutoka Zanzibar tunafikiria kupiga kura za wazi ili tuweze kudhibiti kura zetu,” alisema Haji, ambaye ni Mwakilishi kutoka Jimbo la Kiwani.

source: Mwananchi.

Ng'wamapalala,
Inawezekana sasa ukapata jawabu nani kati yangu na wewe asiefahamu!
 
Back
Top Bottom