Paul Makonda
Member
- Jul 8, 2011
- 97
- 185
Tukielekea Kwenye Mjadala wa Leo Jioni Hii:
Tumekaribia kufikia makubaliano ya jinsi ya kupiga kura ya maamuzi. Makubaliano yoyote yawe kwa misingi ya kulinda maslahi ya taifa na heshima ya bunge hili. Pamoja na kuwa watanzania wengi hawatuelewi katika mijadala yetu kama kweli tuna nia thabiti ya kutengeneza katiba ya Jamhuri.
ubishani wa aina gani ya kura tutaitumia, unatakiwa ufike mwisho. Ama kura za wazi ama za siri ni mambo yanaweza kwisha. Kuna kura ya Kielektronic ambalo nalo laweza kuwa wazi ama Siri.
Kwa mujibu wa mabadiliko ya kanuni kupitia kamati ya Kanuni na Maridhiano. Imetoa maadhimio ya ama SIRI ama WAZI.
Mjadala huu unaenda mbali kwenye kulazimishana sasa wale wa WAZI wanawavuta wa Siri na wale wa SIRI halikadhalika wanawavuta wa Wazi.
Sasa, kwa nini wote tusiachane na hizo kura za WAZI ama SIRI za Makaratasi na twende kwenye DIJITALI yaani Tuingie kwenye ELECTRONIC VOTING.
Mivutano ya Wazi au Siri ni ya kimakundi. Haina Maslahi na Taifa na daiyo maana makundi haya yameanza kutafuta ushawishi wa kundi kuungwa mkono na wajumbe wengi kuliko jingine. Na kama tukiacha hali hii iendelee, tutajikuta tunatakiwa tupumzike siku mbili au tatu kwa ajili ya watu kupiga kampeni za kuhamishana huku na kule. Na kupumzika nakokusema si lazima kuwe rasmi maana kuna watu humu wanaweza kuja na Vurugu zisizo na maana na kulazimisha Mwenyekiti ama Makamu Mwnyekiti kuahirisha Bunge hili Maalum.
Tuhame kwa pamoja, ELEKTRONIK ndo Mpango wa kutuondoa katika Mgogoro huo. Mfano mzuri wa Kura za Elektronik ni Mifumo ya Kura za Maoni Marekani, Mataifa ya Ulaya na hivi Juzi Kenya. Tofauti ndogo ya sisi hapa na huko ni kwamba huko wanatumia njia ya Mtandao kupiga kura kwa Internet na kisha unapata Majibu mara tu baada ya Uchaguzi. Uholansi wanatumia Elecronik kwa uchaguzi Mkuu.
Kura ya Kielektronik.
Tutapiga kura kwa kutumia vifaa vya kisasa kabisa tunavyotumia kwa mawasiliano humu bungeni na kura zote zitahesabiwa na machine (Mtambo maalum) na tutapata majibu sahihi ya kweli yasiyo na shaka ya uhalali wake.
Wapo wanaojenga hofu eti Mfumo huu ni wa Wizi. Hapa tuwaeleze kuwa Electronic ni ya Kuaminiwa ndiyo maana kuna watu wanasomea kwa miaka mingi. Na kama Kuna Alegations kuwa huo ni Mfumo wa Wizi, basi na ithibitishwe kuwa waliosomea wamesomea Wizi.
Tutafanya kazi hiyo kwa muda mfupi sana na kwa muda mfupi huo tutapata majibu. Sasa hapo ukitaka UWAZI au USIRI hiari yako maana kwa wale wa WAZI watapata PRINTOUT ya Kura zote na Kila mtu kwa Jina lake, na Wale wa SIRI wataachana na Kupata hiyo PRINTOUT.
Elektronic itaendelea kutuweka wamoja wenye kupingana kwa Hoja bila Kupigana litakapofika suala la Kuamua Kwa Kura. Pamoja na Changamoto zake Mfano a ni upatikanaji wa nishati ya Umeme kwa muda wote, na
Inahitaji kujiridhisha na kufanya majaribio, lakini ukilinganisha na Changamoto, Faida ni nyingi na zenye mantiki kuliko Changamoto.
Mungu Ibariki Tanzania
Paul C. Makonda,
Mjumbe Bunge Maalum la Katiba
Tumekaribia kufikia makubaliano ya jinsi ya kupiga kura ya maamuzi. Makubaliano yoyote yawe kwa misingi ya kulinda maslahi ya taifa na heshima ya bunge hili. Pamoja na kuwa watanzania wengi hawatuelewi katika mijadala yetu kama kweli tuna nia thabiti ya kutengeneza katiba ya Jamhuri.
ubishani wa aina gani ya kura tutaitumia, unatakiwa ufike mwisho. Ama kura za wazi ama za siri ni mambo yanaweza kwisha. Kuna kura ya Kielektronic ambalo nalo laweza kuwa wazi ama Siri.
Kwa mujibu wa mabadiliko ya kanuni kupitia kamati ya Kanuni na Maridhiano. Imetoa maadhimio ya ama SIRI ama WAZI.
Mjadala huu unaenda mbali kwenye kulazimishana sasa wale wa WAZI wanawavuta wa Siri na wale wa SIRI halikadhalika wanawavuta wa Wazi.
Sasa, kwa nini wote tusiachane na hizo kura za WAZI ama SIRI za Makaratasi na twende kwenye DIJITALI yaani Tuingie kwenye ELECTRONIC VOTING.
Mivutano ya Wazi au Siri ni ya kimakundi. Haina Maslahi na Taifa na daiyo maana makundi haya yameanza kutafuta ushawishi wa kundi kuungwa mkono na wajumbe wengi kuliko jingine. Na kama tukiacha hali hii iendelee, tutajikuta tunatakiwa tupumzike siku mbili au tatu kwa ajili ya watu kupiga kampeni za kuhamishana huku na kule. Na kupumzika nakokusema si lazima kuwe rasmi maana kuna watu humu wanaweza kuja na Vurugu zisizo na maana na kulazimisha Mwenyekiti ama Makamu Mwnyekiti kuahirisha Bunge hili Maalum.
Tuhame kwa pamoja, ELEKTRONIK ndo Mpango wa kutuondoa katika Mgogoro huo. Mfano mzuri wa Kura za Elektronik ni Mifumo ya Kura za Maoni Marekani, Mataifa ya Ulaya na hivi Juzi Kenya. Tofauti ndogo ya sisi hapa na huko ni kwamba huko wanatumia njia ya Mtandao kupiga kura kwa Internet na kisha unapata Majibu mara tu baada ya Uchaguzi. Uholansi wanatumia Elecronik kwa uchaguzi Mkuu.
Kura ya Kielektronik.
Tutapiga kura kwa kutumia vifaa vya kisasa kabisa tunavyotumia kwa mawasiliano humu bungeni na kura zote zitahesabiwa na machine (Mtambo maalum) na tutapata majibu sahihi ya kweli yasiyo na shaka ya uhalali wake.
Wapo wanaojenga hofu eti Mfumo huu ni wa Wizi. Hapa tuwaeleze kuwa Electronic ni ya Kuaminiwa ndiyo maana kuna watu wanasomea kwa miaka mingi. Na kama Kuna Alegations kuwa huo ni Mfumo wa Wizi, basi na ithibitishwe kuwa waliosomea wamesomea Wizi.
Tutafanya kazi hiyo kwa muda mfupi sana na kwa muda mfupi huo tutapata majibu. Sasa hapo ukitaka UWAZI au USIRI hiari yako maana kwa wale wa WAZI watapata PRINTOUT ya Kura zote na Kila mtu kwa Jina lake, na Wale wa SIRI wataachana na Kupata hiyo PRINTOUT.
Elektronic itaendelea kutuweka wamoja wenye kupingana kwa Hoja bila Kupigana litakapofika suala la Kuamua Kwa Kura. Pamoja na Changamoto zake Mfano a ni upatikanaji wa nishati ya Umeme kwa muda wote, na
Inahitaji kujiridhisha na kufanya majaribio, lakini ukilinganisha na Changamoto, Faida ni nyingi na zenye mantiki kuliko Changamoto.
Mungu Ibariki Tanzania
Paul C. Makonda,
Mjumbe Bunge Maalum la Katiba