Toosweet
JF-Expert Member
- May 27, 2012
- 2,141
- 1,982
Umuofia Kwenu,
Tukio la kupotea na kupatikana kwa mtangazaji wa AzamTV,Fatna Ramole na kisha kupatikana baada ya siku mbili limezua sintofahamu.
Taarifa za kupotea Fatna zilisambazwa na dada yake, Lulu Ramole kwenye ukurasa wake wa Twitter. Alisema tayari wametoa taarifa za kupotea kituo cha polisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao waliahidi kuendelea na uchunguzi.
Hata hivyo, saa nane mchana Jumamosi ya terehe 1 Juni, 'msamaria mwema' aliwapigia ndugu simu kuwa amepatikana Makongo lakini kuhusu kapatikanaje hawawezi kueleza kwa kuwa uchunguzi unaendelea.
Chanzo cha habari cha Azam kimesema Fatna aliondoka ofisini siku ya Alhamis jioni kama kawaida.
"Nilipigiwa simu na mpenzi wake siku ya Alhamisi akinifahamisha kuwa simu ya Fatna haipatikani,hiyo ikiwa ni muda mfupi baada ya kumwambia gari lake liligongwa, " kilisema chanzo.
Kamanda wa polisi wa Kinondoni Susan Kaganda alisema hana taarifa rasmi na aliahidi kufuatilia.
Source:Mwananchi.
Tukio la kupotea na kupatikana kwa mtangazaji wa AzamTV,Fatna Ramole na kisha kupatikana baada ya siku mbili limezua sintofahamu.
Taarifa za kupotea Fatna zilisambazwa na dada yake, Lulu Ramole kwenye ukurasa wake wa Twitter. Alisema tayari wametoa taarifa za kupotea kituo cha polisi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao waliahidi kuendelea na uchunguzi.
Hata hivyo, saa nane mchana Jumamosi ya terehe 1 Juni, 'msamaria mwema' aliwapigia ndugu simu kuwa amepatikana Makongo lakini kuhusu kapatikanaje hawawezi kueleza kwa kuwa uchunguzi unaendelea.
Chanzo cha habari cha Azam kimesema Fatna aliondoka ofisini siku ya Alhamis jioni kama kawaida.
"Nilipigiwa simu na mpenzi wake siku ya Alhamisi akinifahamisha kuwa simu ya Fatna haipatikani,hiyo ikiwa ni muda mfupi baada ya kumwambia gari lake liligongwa, " kilisema chanzo.
Kamanda wa polisi wa Kinondoni Susan Kaganda alisema hana taarifa rasmi na aliahidi kufuatilia.
Source:Mwananchi.