Kupimiwa shamba au kiwanja mpaka kupata hati

Kupimiwa shamba au kiwanja mpaka kupata hati

Huhitaji kugharamia kujua plot yako kama imepimwa ama la. Hujui Global Position System (GPS)? Basi utaendele kuibiwa tupu, hiyo ni elimu ya basic kbs, gps ziko mpk za laki tu na simu zingine ziko nayo.
Afu punguza maneno ya kiswahili swahili

Mkuu upo sahihi kuhusu hii knowledge,binafsi nimeanza kufikiria kuwa na GPS Yangu na kujifunza kuitumia ila Hizo za kwenye simu coordinates zake hazifai,huwa zina hitaji kufanyiwa conversion ili uweze kupata eneo kwenye mchoro kule ardhi

Ndio hapo sijaelewa labda aje afafanue vizuri inakuwaje kwenye hiyo laki 3???maana naona kuna changa la macho hapo.... xfactor tafadhali njoo mara moja tusaidie hapa.....

Hii bei ya laki 3 ni kubwa sana kwa kuchukua GPS,bei ya juu kabisa ni laki 1 na kuna ambao wanafanya mpaka kwa elfu 50 kama ni mfanyakazi wa Ardhi maana kwa kawaida kwenda site ni elfu 50 na kupeleka coordinates ardhi ni elfu 50 which makes laki 1.

Japo bei zao kupima mpaka kuweka mawe na kupata hati sio Mbaya sana.kwa kawaida bei ya ekari moja ni around 2M kama eneo husika lina plan ya mipango miji otherwise kama hamna city plan then itabidi uongeze kama 4M kwa ajili ya kuchora city plan na kuipitisha
 
Last edited by a moderator:
Hizi mambo nazipiga sana lakini zina changamoto sana hususani kitengo cha Ardhi wizarani, inahitaji mteja uwe mvumilivu kweli.
 
okey hii ishu ipo hivi, kama una ardhi haijapimwa kwanza tutatakiwa tuiangalie kwa kuchukua coordinate za eneo husika na kuzipeleka ARDHI, hapo watatuangalizia eneo letu kama lina mchoro au halina mchoro. kama Eneo lina mchoro tutaangalia eneo hilo ni la matumizi gani? kama ni matumizi sahihi tutaanza process za kupima.

kama eneo lako halina mchoro tunakuandalia mchoro tunaupeleka manispaa husika ukipitishwa tunaurudisha ardhi kwa process zingine, kwa kesi hii ya ardhi isiyo na mchoro kidogo pana shida kama kiwanja kipo kimoja hasa hapo kwenye kuupitisha manispaa

baada ya kupata mchoro na kujiridhisha na matumizi ndo tunaanza kazi ya survey mpaka kupata offer then kupatikana kwa hati.
kama unahitaji tukakuangalizia eneo tu gharama zetu ni laki 3
kama ulishaanza umefika hatua ya kuweka mawe huna hati tukianzia kwenye mawe mpaka hati gharama zetu ni milion 2
na kama unataka tukufanyie kazi kanzia kuangalia eneo hadi kukupimia namaanisha kuweka mawe gharama zetu ni milion 2
na kama unataka tukufanyie mchakato mzima gharama zetu ni milion 4
karibuni

Mimi eneo langu lishapimwa na lina hati ila baadhi ya beacons hazionekani kwa sasa na nahisi zimeng'olewa na majirani, je gharama itakuwa kiasi gani ili kufufua mipaka?
 
Back
Top Bottom