SOKETI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2010
- 206
- 50
Swala la kupenda ni jambo muhimu sana katika maisha ya binadamu na ni mojawapo kati ya mahitaji muhimu sana ya kijamii kwa mwanadamu. Kila mtu anahaki ya kupenda na kupenda. Kwa upande wa upendo wa jinsia tofauti hasa ule wa kimapenzi swala la kupenda ni tofauti na upendo wa kawaida, na umekuwa na mikanganyiko mingi hasa katika hatua zake. Je ukweli ni upi..kipi kinatangulia kati ya kupenda au kutamani? Je, Unaweza kumpenda mtu bila kumtamani?