Kupandishwa vyeo JWTZ

Kupandishwa vyeo JWTZ

gabriel sanya

Member
Joined
Jan 15, 2014
Posts
6
Reaction score
1
Takribani miaka minne iliyo pita upandishwaji vyeo vya maafisa wakuu ( Brig Gen )umekuwa ukifanyika bila kufuata !!MUUNDO WA JWTZ'' Muundo kwa maana ya ukubwa wa jeshi idadi ya nguvu kazi iliyopo, ikijumuisha askari na silaha.

Tafsiri iliyopo inaonekana vyeo vinatolewa kama zawadi na sio kwa kufuata Merits. Inashangaza kuona jeshi linakuwa na majenerali wengi ambao hawafiti kwenye muundo., athari zake ni serikali kujibebesha Mzigo wa fadhila uchwara. Baadhi au wengi wao wanaishi kwenye nyumbani za kupanga uswahilini ambazo pengine hazina hadhi ya chao chake na huenda pia hazipo katika maeneo yenye usalama. Kwa maana nyingine watahitaji nyumba zilizo kwenye maeneo salama.

Kwa ukubwa na idadi hiyo watahitaji magari aina ya mashangingi yeye nyota za shaba kwa ajili ya utambulisho. Mishahara minono, ofisi, samani za ndani kwa entitlement zao. Sura ya kupandisha vyeo kama zawadi au fadhila inakuja kuonekana pale afisa mkuu huyo anatumika kwa muda wa mwaka mmoja tangu apate cheo anafikia kikomo cha mda wake wa kustaafu utumishi jeshini. Baadhi ya magazeti yameandika wakistaafu watalipwa billion 3 kwa mkupuo.

Kama mfumo ni huo je askari wetu na maafisa wadogo tutawapa fadhila gani wakikaribia kustaafu?
Na hawa ndio watendaji halisi.

Tutafakri !!!!
 
gabriel sanya Kwani maafisa wakubwa sio watendaji halisi? Anayewafundisha na kuwaelekeza na kuwasimamia kazi zao za kila siku hao maafisa wadogo ni nani katika muundo wa Jeshi.Unajua kazi za ma-brigadia na magenerali wewe au unaandika tu? Unajua mishe mishe na mikiki mikiki ya kufikia hivyo vyeo vya juu? Au unadhani vyeo vya JWTZ vinaokotwa barabarani kaokote na wewe kama vinaokotwa.

Umesikia hao wadogo wakistaafu hela na fadhila za kuwalipa hazipo?

Wewe kama ni mwanajeshi yawezekana kabisa ni wale walioingia jeshini ikiwa ni last resort baada ya kukosa kwingine kwa kwenda na hujiendelezi umekaa tu kupiga domo tu.Na kama unadhani Jeshi linakuonea kama sifa unazo acha rudi uraiani kama unauzika.Lakini nahisi huna sifa hata za kwenda uraiani.
 
Last edited by a moderator:
Huyu anajua muundo? Anajua position gani zinatakiwa kukaliwa na watu wa vyo gani? Anajua jeshi limepanuka tofauti na wakati yeye alipokuwepo kabla hajafukuzwa/kuachishwa? Anajua kuwa Jeshi ni kutokana na sifa? Amtaje yoyte hapo ambaye anadhani hakustahili kupata cheo. Wivu, uvuvi wa kufikiri na kuingilia mambo usiyoyajua ndiyo vinakusumbua.
 
Mtoa mada apewe nafasi ya kufunguka zaidi, ninahisi ana point. Huenda kuna maafisa wamepandishwa vyeo bila kuwa na sifa na yeye anawajua. Na pia kama ni askari kwa jeshi la Tanzania lenye 4 star general muundo wake unajulikana na hata idadi ya askari inajulikana pia. Mtoa mada embu funguka zaidi
 
. Na pia kama ni askari kwa jeshi la Tanzania lenye 4 star general muundo wake unajulikana na hata idadi ya askari inajulikana pia. Mtoa mada embu funguka zaidi


Kwa kukujibu tu ni kuwa muundo wowote wa Jeshi lolote Duniani haujulikani kwa undani kwa watu nje ya maamiri jeshi na wakuu wa majeshi

Muundo wa majeshi yote duniani hauishii kwenye organization structue kama za mashirika zilivyo ulivyosoma vyuoni. Majeshi huwa ndani na nje ya box la published organization structure.Majenerali na mabrigadia kote duniani hawaishii kwenye makambi na mabrigedi tu wako wenye kazi maalumu iwe makambini au nje ya makambi kwenye mabrigedi au nje ya mabriged..Anayejua yule ni brigedia au generali wa nini ni Amiri Jeshi mkuu aliyewapa hivyo vyeo.Sasa kama ukikariri kuwa kuna brigade mbili hivyo zinahitaji mabrigedia wawili utajijua shauri yako.Duniani kote wala haiko hivyo.Unaweza shangaa Bregedi ziko mbili mabrigedia wako ishirini.Wengine wana-brigedi kitu gani hayakuhusu!

.
 
Na hili la kupandisha maafisa vyeo analaumiwa JK?

Damned if you do...
 
Nashukuru kwa hizi taarifa japo binafsi sijaelewa nini maana ya kuzileta hapa. Kupindishwa vyeo karibu na kustaafu ni jambo la kawaida sana kwa kipindi hiki. utakuwa hutendi haki ukiwa angalia JWTZ peke yao. Labda katiba mpya yaweza kupunguza adha hii kwa kiasi fulani.
 
Wakuu! Huu uzi utakuwa mzuri mkiacha kuzodoana... nitarudi badae, naenda jukwaa la Teknolojia.
 
Bila shaka yule aliyekuwa kwa Bwana Mkubwa hajafurahia hicho cheo kwa mwaka huu, pengine ingelikuwa mwaka kesho baada ya kuwa wameshazunguka duniani kuaga. Mafao ya kuzunguka ughaibuni sidhani yanalingana na yale ya kuketi pale Ngome. Pengine angeulizwa kabla, angeshauri abaki hapo hapo na cheo kile kile cha awali hadi Oktoba 2015! ni mtazamo tu!
 
Bila shaka yule aliyekuwa kwa Bwana Mkubwa hajafurahia hicho cheo kwa mwaka huu, pengine ingelikuwa mwaka kesho baada ya kuwa wameshazunguka duniani kuaga. Mafao ya kuzunguka ughaibuni sidhani yanalingana na yale ya kuketi pale Ngome. Pengine angeulizwa kabla, angeshauri abaki hapo hapo na cheo kile kile cha awali hadi Oktoba 2015! ni mtazamo tu!

Kaka naomba kuuliza inamaana yule jamaa akiwa brigedia hawezi kumlinda mkulu tena? Mm nilijua wanaomlinda rais ndio makomandoo wa ngazi za juu karibia na mkuu wa majeshi? Na kama anabadirishiwa majukumu mbona hatafikia hata nusu ya alichokuwa anakiingiza maana ziara za rais ndani na nje ya nchi perdiem yake sio mchezo.
 
Hilo hata sisi huku Israel tumeliona kuna dosari kubwa sana katika upandishaji vyeo aina hii, hata hivyo Mods weka hii katika jamii Intergence tufunguke kwa uwazi zaidi athari zake.
 
Hilo hata sisi huku Israel tumeliona kuna dosari kubwa sana katika upandishaji vyeo aina hii, hata hivyo Mods weka hii katika jamii Intergence tufunguke kwa uwazi zaidi athari zake.

Kuna daladala nililikuta lina maandishi makubwa yameandikwa KONGO SIO KONGOWE.Humu Jamii forums ISRAEL KUNAWEZA KUWA KONGOWE !!!! anything is possible here.
 
unamaanisha nini unaposema wamepewa fadhila? ni fadhila ya nini? Je ni kweli walikuwa hawastahiki kupandishwa vyeo kwa mujibu wa taratibu zilizopo? unamaanisha nini unaposema maafisa wadogo ndo wanafanya kazi? hii gongo itatuharibia vijana maana wanamawazo yakufikirika.


Takribani miaka minne iliyo pita upandishwaji vyeo vya maafisa wakuu ( Brig Gen )umekuwa ukifanyika bila kufuata !!MUUNDO WA JWTZ'' Muundo kwa maana ya ukubwa wa jeshi idadi ya nguvu kazi iliyopo, ikijumuisha askari na silaha.

Tafsiri iliyopo inaonekana vyeo vinatolewa kama zawadi na sio kwa kufuata Merits. Inashangaza kuona jeshi linakuwa na majenerali wengi ambao hawafiti kwenye muundo., athari zake ni serikali kujibebesha Mzigo wa fadhila uchwara. Baadhi au wengi wao wanaishi kwenye nyumbani za kupanga uswahilini ambazo pengine hazina hadhi ya chao chake na huenda pia hazipo katika maeneo yenye usalama. Kwa maana nyingine watahitaji nyumba zilizo kwenye maeneo salama.

Kwa ukubwa na idadi hiyo watahitaji magari aina ya mashangingi yeye nyota za shaba kwa ajili ya utambulisho. Mishahara minono, ofisi, samani za ndani kwa entitlement zao. Sura ya kupandisha vyeo kama zawadi au fadhila inakuja kuonekana pale afisa mkuu huyo anatumika kwa muda wa mwaka mmoja tangu apate cheo anafikia kikomo cha mda wake wa kustaafu utumishi jeshini. Baadhi ya magazeti yameandika wakistaafu watalipwa billion 3 kwa mkupuo.

Kama mfumo ni huo je askari wetu na maafisa wadogo tutawapa fadhila gani wakikaribia kustaafu?
Na hawa ndio watendaji halisi.

Tutafakri !!!!
 
Mkuu gabriel sanya heshima sana,

Rais Kikwete ni amiri jeshi mkuu kwa mujibu wa katibu ya JMT anayo mamlaka kamili ya kupandisha cheo wanajeshi.Mpaka hapo sioni kosa alililofanya.

Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali Tanzania inakisiwa kuwa na idadi ya wanajeshi (active personnel) 27,000 - 30,000 tu.Tanzania pia inakisiwa kuwa na jeshi la akiba (reserve personnel) 80,000 - 100,000 tu hawa ni wale waliopitia jeshi la mgambo,JKT na askari wastaafu wenye nguvu.

Ukubwa wa jeshi ni kigezo muhimu sana unapotaka kupandisha vyeo askari.Kigezo kingine ni uwezo wa kiuchumi pia uangaliwa sana.Kama uchumi wako si mzuri sana kuweza kuhimili matumizi yasiyoweza kuepukwa kama mishahara inayokidhi mahitaji muhimu,vifaa vya kisasa na nk.Kigezo kingine ni hali ya usalama,ikiwa nchi iko katika hali yakuweza kuvamiwa ni lazima bajeti iongezeke mara dufu hapa nazungumzia vifaa na kuongeza idadi ya wanajeshi.

Ukiangalia idadi ya wanajeshi wetu na idadi ya mageneral haziendani hata kidogo, unapokuwa na Lt General 4. kama kumbukumbu zangu ziko sana kuna mkuu wa utawala jeshini Lt Gen S Ndomba, kuna Lt Gen mwingine yuko ofisi ya waziri mkuu (maafa) kuna Lt Gen Mwingine ni mkuu wa chuo cha taifa cha ulinzi kuna mwingine sikumbuki akapachikwa wapi.Ukienda kwa Major General labda sasa wanaweza kufikia 20 ukishuka ngazi ya Brig General wanaweza kufikia 50 au zaidi.Mfano chief of personnel ni Major General na director wake ni Major General.Ukijakutazama idadi ya Brig General utakuta wengi hawana kazi zinazoendeana na majukumu yao sana sana utakumbana na siasa mtindo mmoja
 
East Africa, soma na uelewe kilicho andikwa hapa sio swala la wivu wala kukosa cheo. Ninaamini ulicho andika hakuna facts wala data hivyo maoni yako yana mkusanyiko wa mawazo yasiyo kidhi mjadala huu. Kama hujui dadisi ujue zaidi. Hata hivyo nakushukuru sana kwa kauli zako.
 
Adha ipi, ya kuwapandisha wanajeshi vyeo? Watanzania bwana, mnadhani hawa wanajeshi watakuwa na vyeo hivyo hivyo toka waingingie jeshi hadi wastaafu? Mkuu wa majeshi ajae atapatikana vipi kama hakuna watu wanaopandishwa vyeo?

Nashukuru kwa hizi taarifa japo binafsi sijaelewa nini maana ya kuzileta hapa. Kupindishwa vyeo karibu na kustaafu ni jambo la kawaida sana kwa kipindi hiki. utakuwa hutendi haki ukiwa angalia JWTZ peke yao. Labda katiba mpya yaweza kupunguza adha hii kwa kiasi fulani.
 
Kama ulivyojishitukia, kumbukumbu zako huenda si za kweli. Rudia tena uambiwe.

Mkuu gabriel sanya heshima sana,

Rais Kikwete ni amiri jeshi mkuu kwa mujibu wa katibu ya JMT anayo mamlaka kamili ya kupandisha cheo wanajeshi.Mpaka hapo sioni kosa alililofanya.

Kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali Tanzania inakisiwa kuwa na idadi ya wanajeshi (active personnel) 27,000 - 30,000 tu.Tanzania pia inakisiwa kuwa na jeshi la akiba (reserve personnel) 80,000 - 100,000 tu hawa ni wale waliopitia jeshi la mgambo,JKT na askari wastaafu wenye nguvu.

Ukubwa wa jeshi ni kigezo muhimu sana unapotaka kupandisha vyeo askari.Kigezo kingine ni uwezo wa kiuchumi pia uangaliwa sana.Kama uchumi wako si mzuri sana kuweza kuhimili matumizi yasiyoweza kuepukwa kama mishahara inayokidhi mahitaji muhimu,vifaa vya kisasa na nk.Kigezo kingine ni hali ya usalama,ikiwa nchi iko katika hali yakuweza kuvamiwa ni lazima bajeti iongezeke mara dufu hapa nazungumzia vifaa na kuongeza idadi ya wanajeshi.

Ukiangalia idadi ya wanajeshi wetu na idadi ya mageneral haziendani hata kidogo, unapokuwa na Lt General 4. kama kumbukumbu zangu ziko sana kuna mkuu wa utawala jeshini Lt Gen S Ndomba, kuna Lt Gen mwingine yuko ofisi ya waziri mkuu (maafa) kuna Lt Gen Mwingine ni mkuu wa chuo cha taifa cha ulinzi kuna mwingine sikumbuki akapachikwa wapi.Ukienda kwa Major General labda sasa wanaweza kufikia 20 ukishuka ngazi ya Brig General wanaweza kufikia 50 au zaidi.Mfano chief of personnel ni Major General na director wake ni Major General.Ukijakutazama idadi ya Brig General utakuta wengi hawana kazi zinazoendeana na majukumu yao sana sana utakumbana na siasa mtindo mmoja
 
Takribani miaka minne iliyo pita upandishwaji vyeo vya maafisa wakuu ( Brig Gen )umekuwa ukifanyika bila kufuata !!MUUNDO WA JWTZ'' Muundo kwa maana ya ukubwa wa jeshi idadi ya nguvu kazi iliyopo, ikijumuisha askari na silaha.

Tafsiri iliyopo inaonekana vyeo vinatolewa kama zawadi na sio kwa kufuata Merits. Inashangaza kuona jeshi linakuwa na majenerali wengi ambao hawafiti kwenye muundo., athari zake ni serikali kujibebesha Mzigo wa fadhila uchwara. Baadhi au wengi wao wanaishi kwenye nyumbani za kupanga uswahilini ambazo pengine hazina hadhi ya chao chake na huenda pia hazipo katika maeneo yenye usalama. Kwa maana nyingine watahitaji nyumba zilizo kwenye maeneo salama.

Kwa ukubwa na idadi hiyo watahitaji magari aina ya mashangingi yeye nyota za shaba kwa ajili ya utambulisho. Mishahara minono, ofisi, samani za ndani kwa entitlement zao. Sura ya kupandisha vyeo kama zawadi au fadhila inakuja kuonekana pale afisa mkuu huyo anatumika kwa muda wa mwaka mmoja tangu apate cheo anafikia kikomo cha mda wake wa kustaafu utumishi jeshini. Baadhi ya magazeti yameandika wakistaafu watalipwa billion 3 kwa mkupuo.

Kama mfumo ni huo je askari wetu na maafisa wadogo tutawapa fadhila gani wakikaribia kustaafu?
Na hawa ndio watendaji halisi.

Tutafakri !!!!

mbona poa tu, kama wengi wengine watakuwa wanakuja kusoma magazeti na wengine watakuwa food members
 
Ninachofahamu ni kwamba kwa muundo wa jeshi la Tanzania, ambao umefuata mfumo wa Uingereza (Jumuiya ya Madola), hakuna cheo kama brigedia jenerali. Ni brigedia tu. Kwa hiyo mabrigedia ni mabrigedia tu, na wala si majenerali. Haya mambo ya mabrigedia kuitwa mabrigedia jenerali yalianza ghafla wakati wa awamu ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa. Vyeo vya jenerali kwa muundo wa majeshi ya nchi za Jumuiya ya Madola ni meja jenerali, luteni jenerali na jenerali. Ili uwe jenerali ni lazima uwe na ule 'mkasi' mabegani. Mabrigedia hawana 'mkasi' huo na alama ya cheo chao ni ngao na nyota tatu. Cheo cha brigedia jenerali kipo katika jeshi la Marekani na nchi nyingine zinazotumia mfumo huo. Mabrigedia jenerali wanajulikana nchini Marekani kama majenerali wa nyota moja (one star general). Meja generali ana nyota mbili; luteni jenerali nyota tatu na jenerali nyota nne (four star general). Kwa hiyo si kweli kwamba jeshi letu lina majenerali lukuki.
 
Hii nayo Kaali. Kujaza majenerali nako ni janga tuu. kama kweli hawatakuwa na kazi, si mnajua wasiokuwa na kazi wanakuwa ni workshop ya shetani. Hii naweza kusema ni tatizo la ki sera na mikakati. kama career planning iko kizungumkuti, basi inafikia tu wapewe ma vyeo hayo. Huwezi kuendelea kukaa na kuwaangalia disgruntled colonels, japo nayo hiyo si suluhisho. mlolongo wa kupandisha vyeo utaendelea to hadi cheo cha mwisho kabisa chini. Majeshi mengine yalishaliona hilo na wakaweka msimamo wa kuwa muundo siku zote utasimamimiwa bila kufinya macho. Merits na nafasi zitatumika. Sasa, kama wengi wanazosifa basi huitwa na kuelezwa wako over due, lakini hawatavaa manyota, bali watalipwa kiwango cha cheo hicho. baada ya muda kama hawakupandishwa vyeo wanastaafishwa na kulipwa haki zao zote. hii husababisha system/jeshi kupumua. bila hivyo. ni kuahirisha tatizo.
 
Back
Top Bottom