Kuota ndoto unaongea na mtu ambaye tayari ameshafariki dunia

Kurutu wa Mungu

JF-Expert Member
Oct 23, 2017
366
571
Habari za sasa hivi Wana JF,

Bila kupoteza muda niko hapa kuomba USHAURI Juu ya ndoto inayonitesa. Huu ni mwaka wa 4 sasa, iko hivi kuna jamaa tulikua nae na kucheza pamoja toka utotoni huko kijijini kwetu, hata shule ya msingi tulisoma pamoja, tukaachana mwaka 2005 nikiwa darasa la 6 ambapo mimi nilihamia mkoa mwingine

Toka hapo nilikuwa sina mawasiliano naye wala ukaribu wa aina yoyote maana sikurudi tena kijijini hadi mwaka 2015 mwezi wa 8 nilipoenda kwa dharura ya msiba wa mjomba kwa vile nilienda kwa dharura nilikaa siku moja asubuhi nikaondoka kurudi ninapoishi, na huyo jamaa nilionana nae nikiwa naelekea kupanda gari kurudi.

Kwa vile alikuwa rafiki yangu mkubwa utotoni alinisihi nisiondoke siku hiyo alinitaka nilale niondoke asubuhi yake tuongee na kukumbushana story zetu za utotoni hadi akawa ananiahidi kuna jogoo nyumbani kwao nikikubali kulala atanichinjia na atanitafutia zawadi ya samaki nirudi nao mjini, maana Kijiji kiko kandokando ya ziwa Victoria

ilimkatalia maana nilikuwa nimepewa ruhusa ya siku 5 kazini na kutoka ninapoishi hadi kufika huko nilikua nimeshapoteza siku 2. Tulipeana tu namba za simu nikaondoka baada ya hapo niliwasiliana nae kama mara 3. Ilipofika mwaka 2016 mwezi wa7 nilipata taarifa kuwa huyo jamaa amefariki kwa kuanguka juu ya mti wa mwembe. Kwa vile nilimfahamu nilisikitika sana, cha kushangaza toka huo mwaka wa 2016 nimekuwa nikimuota mara kwa mara yaani haupiti mwezi bila kumuota

Mwanzoni nilijua hali hiyo ingepotea lkn imekuwa sivyo, nilijaribu kuwashirikisha ndugu wa karibu wakaniambia niwe ninasali, nimejaribu kufanya hivyo lkn bado nimekuwa naota tuko pamoja tunaongea. Mwaka Jana mwezi wa 9 nilienda kusalimia kijijini nikafika hadi kwao kuwapa pole na kuona kaburi lake pia nilijaribu kuuliza juu ya kumuota mara kwa mara. Wanakijijini nilioongea nao wakaniambia kifo chake kimejaa utata na kuna mauzauza mengi yanawatokea toka siku ya msiba wanadai alikuwa anawagongea milango usiku na kujitambulisha kuwa ni yeye kama wamebakisha chakula wampe ale ana njaa

Mara ya mwisho kuota nijuzi nimeota niko nae namuuliza "" kwanini tuko pamoja wakati wewe ulishakufa?"" yeye alianza kulia sasa Kuna sauti ikawa inanijibu lkn simuoni huyo anayeninibu ""Huyu hajafariki na usiwe unamuuliza hilo swali anajisikia vibaya"" ghafla upepo ukavuma halafu wakashuka watu wa3 kumchukua na mimi wakanishika tukaanza kupaa yaani tunaenda kwa spidi kali tukawa tunaelekea ziwani nikawa naona mazingira ya kijijini napita juu ya mapaa ya nyumba za nyasi nikawa napiga kelele ghafla, nikashituka nikawa natoka jasho na moyo unaenda mbio

Kiukweli nikitoka usingizini huwa nakosa amani na inanichukua mda kupata tena usingizi, Je ni nini kinafanya niwe namuota?

Na suluhisho ni nini?
 
Pole mkuu. kuna mambo matatu ya kufanya yabaweza kukusaidia pia inaonekana jamaa ako aliumia sana kukataa wewe kwenda kwao alikuwa na ile bond nzuri ya kirafiki kati yako nawewe so alipata kinyongo na hii inaweza kuwa ni sababu pia ya wewe kuota hivyo.....

1: jitahidi sana kupunguza dhambi zako kabla hujasali , yani muda fulani unaweza jikuta tu hujibiwi maombi yako sababu ya mzigo wa dhambi unazobeba iwe chuki, usaliti n.k

2: jitahidi kwenda kwao bila kupelekwa na tukio lingine mfano hapo umesema ulifika kwao kwasababu ulienda msibani ukaona ukawape pole.....safari hii nenda kwao bila sababu ya kando wabebee zawadi kiasi unachoweza, ukifika wakabidhi ongea nao kiasi omba kwenda peke ako kaburini huko unaweza sembua na kuomba dakika kadhaa wala hautadhurika....

3: jitahidi sana kujua ulikosea wapi au ulimkosea wapi huyo rafiki yako alafu jitahidi kufunga walau siku

3 ...ukiomba na kuvunja muunganiko uliopo baina yako nayeye....
 
Huyo jamaa kwao dini gani?
Au ndio wale ambao hawajui mlango wa kanisa unafanana vip?
 
Kawaida kabisa hiyo. Baba yangu alifariki zaidi ya miaka 30 iliyopita. Kuna wakati naota naongea naye. Kuna wakati naota ndio amekufa. Nikiamka toka ndotoni nakuta nina machozi kabisa. Mimi huchukulia kuwa ni ndoto tu isiyokuwa na maana yoyote. Maisha yanaendelea mpaka siku Muumba wangu atakaponiita na mimi.
 
Inaumiza Sana, huyo jamaa yako alishachukuliwa kichawi, na inaonekana huko aliko anakukumbuka Sana wewe, na Kama ataendelea kuwasumbua hao wachawi, wanaweza kukufuata ili mkawe pamoja na rafiki yako huyo mfu!

Hii Ni kweli, usipuuze!

Kuna njia kuu mbili tu za kuepuka hi zahama,

Mosi, muombe Sana Mungu.

Tafuta mganga anayeweza akufungie hiyo ndoto.
 
Inaumiza Sana, huyo jamaa yako alishachukuliwa kichawi, na inaonekana huko aliko anakukumbuka Sana wewe, na Kama ataendelea kuwasumbua hao wachawi, wanaweza kukufuata ili mkawe pamoja na rafiki yako huyo mfu!

Hii Ni kweli, usipuuze
Asante mkuu hiyo ya kuomba Sana naona itafaa
 
Inaumiza Sana, huyo jamaa yako alishachukuliwa kichawi, na inaonekana huko aliko anakukumbuka Sana wewe, na Kama ataendelea kuwasumbua hao wachawi, wanaweza kukufuata ili mkawe pamoja na rafiki yako huyo mfu!

Hii Ni kweli, usipuuze!

Kuna njia kuu mbili tu za kuepuka hi zahama,

Mosi, muombe Sana Mungu.

Tafuta mganga anayeweza akufungie hiyo ndoto.
Sure

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Nenda kanisani haraka Sana. Pia waweza ingia You Tube kisha type : JOHN ECKHART: PRAYERS FOR DEFEATING DEMONS. It is a very strong and powerful deliverance prayer and trust me utafunguliwa without a doubt na ndoto hiyo hutoiota tena
 
Naamini kuwa weye ni mkristu na unasali sala zako kila siku kama tulivyo amriwa na kanisa. Ila, natamani nikusaidie haswa hapo kwenye hizo ndoto zako. Ni hivi; Ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi, maneno mengi au mawazo mengi. Huyu jamaa mlikua pamoja, mkakaa sana pamoja. Ila siku alipokuona baada ya muda mrefu, hukumchangamkia kama zamani. Yeye alishangaa kwamba umeweza kufika nyumbani kwako ukalala bila hata kuulizia habari zake! Haya ni maajabu sana kwake. Akakukaribisha hadi kwake, na jogooo na samaki. Ukavidharau vyote. Hata alipokufa, hukuenda kumzika. Huo si urafiki bali usaliti. Nenda kamwombe radhi kwa kumtolea sadaka nzuri ya misa takatifu
 
huyo bado mzima narudia tena huyo bado mzima yashanitokea kwa ndugu yangu kwakuwa mimi mpambanaji ndugu yangu akarudi kama hufatilii mambo ya kiroho unaweza niona mimi mjinga ila namaanisha
 
Naamini kuwa weye ni mkristu na unasali sala zako kila siku kama tulivyo amriwa na kanisa. Ila, natamani nikusaidie haswa hapo kwenye hizo ndoto zako. Ni hivi; Ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi, maneno mengi au mawazo mengi. Huyu jamaa mlikua pamoja, mkakaa sana pamoja. Ila siku alipokuona baada ya muda mrefu, hukumchangamkia kama zamani. Yeye alishangaa kwamba umeweza kufika nyumbani kwako ukalala bila hata kuulizia habari zake! Haya ni maajabu sana kwake. Akakukaribisha hadi kwake, na jogooo na samaki. Ukavidharau vyote. Hata alipokufa, hukuenda kumzika. Huo si urafiki bali usaliti. Nenda kamwombe radhi kwa kumtolea sadaka nzuri ya misa takatifu
Asante mkuu Ila Siyo kwamba nilimdharau ratiba ilibana Sana nanilipofika msibani nilimuulizia Ila wakasema ameenda kuvua samaki asubuhi angerudi, kuhusu kuhudhuria msiba nilikua bize ata Kama niruhusa nisingepata nilituma tuu mchango na kutoa pole kwakuwasiliana na wazazi wake
 
Alikua mkatoliki na tulibatizwa nae mwaka mmoja 2004 nakumnio na kipaimara tukapewa pamoja
Hili swala linahitaji maelezo marefu sana,
Shida ya wanadamu wengi, hatua ya kwanza ya kumwamini Mungu tunaichukua kwa urahis sana... Lakini swala la kutaka kujifunza mambo na kanuni za Mungu, hasa jinsi ya Kusali huo muda huwa hatuna
 
Naamini kuwa weye ni mkristu na unasali sala zako kila siku kama tulivyo amriwa na kanisa. Ila, natamani nikusaidie haswa hapo kwenye hizo ndoto zako. Ni hivi; Ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi, maneno mengi au mawazo mengi. Huyu jamaa mlikua pamoja, mkakaa sana pamoja. Ila siku alipokuona baada ya muda mrefu, hukumchangamkia kama zamani. Yeye alishangaa kwamba umeweza kufika nyumbani kwako ukalala bila hata kuulizia habari zake! Haya ni maajabu sana kwake. Akakukaribisha hadi kwake, na jogooo na samaki. Ukavidharau vyote. Hata alipokufa, hukuenda kumzika. Huo si urafiki bali usaliti. Nenda kamwombe radhi kwa kumtolea sadaka nzuri ya misa takatifu
Sala za kanisa hazitosh hata kidogo, kuna Mengi ya kujifunza ambayo jinsi ya kusali sala hiyo haipo kabisa kweny sala ya kanisani.
 
Back
Top Bottom