Kuondolewa kwa 'Presidential dentetion Order' ni sababu kubwa kwa ongezeko la Wizi Ufisadi nk.

Nakioze

JF-Expert Member
Aug 11, 2014
329
170
Wanajamii,
Nimewasalimu.
Nimeanzisha Mada hii tuitafakari na tujaribu kuijadili kwa kina.
Katika mfumo wa Legislature mapema tu baada ya Uhuru, pamoja na Sheria zingine za nchi, Rais alikuwa na uwezo kisheria kumkamata na kumweka ndani mtu yeyote bila kufikishwa mahakamani endapo Angeridhika mtu huyu ni hatari kitabia, kiusalama au vyovyote vile na kwamba alikuwa hafai kuishi na jamii.

Sheria hii ilimpa nguvu Rais kudhibiti makosa ya Ufisadi, ubadhirifu wakati mwingine ulanguzi wa madawa ya kulevya hata pombe haramu!

Sababu baada ya Tume ya Rais wakati ule ingekubaini kuwa wewe ni miongoni katika washiriki wa matendo hayo na kukufikisha mezani kwa Baba wa Taifa ulikuwa umekwisha!

Mzee Ruksa alipoingia madarakani baada ya kusumbuliwa na tume za haki za binadamu ikabidi aiondoe sheria hii. Hapa Ndipo mapapa wa Bahari walipopata mwanya wa kutamba na kupora pesa za wavuja jasho sababu mahakama ndio ilipitishwa kuwa chombo muafaka kutatua maswala ya ubadhirifu, rushwa, mihadarati n.k. kitu ambacho hakikuwatisha wengi sababu wengi wao walikuwa na uwezo au mbinu ya kupenya.

Kwa nini sheria hii isirudishwe tukapata amani na usalama wa Mali za umma na rasilimali za nchi?
 
sidhani kama ina umuhimu!tume ya nyalali ilitoa pendekezo la kufuta sheria kandamizi 40+,hiyo hapo ikiwemo,pia tume ilishauri madaraka ya raisi yapunguzwe...ukitaka turudi miaka ya 80 huoni kuwa haki nyingi za kiraia zitakuwa zimevunjwa?mbona kuna sheria nyingi za kumaliza ilo tatizo,pasipo kumtegemea raisi:pccb,dpp et al
 
Mimi nadhani kwa hapa ilipofikia nchi yetu hii sheria inafaa sana....kwani hata wezi na mafisadi pamoja na walanguzi wa mihadarati wana athiri haki za binaadamu......
Hebu chukulia kiongozi anayehujumu mradi wa maji kijijini kwa manufaaa yake na familia anawaathiri vipi wananchi kupata maji safi na salama na hivyo kuhatarisha usalama wao na wengi wao kufa kutokana na magonjwa ya milipuko kama taiphodi na kipindu pindu...je kiongozi kama huyu anastahili vipi kubaki uraiani wakati hata kwa matendo yake na tamaa zake anaathiri haki za binaadamu wenzake kuishi....???

Chukulia mfano kigogo anayefahamika kuingiza madawa ya kulevya...je kigogo huyo anaathiri na kuharibu maisha ya vijana wangapi....kila mmoja wetu ni shahidi wa utitiri wa mateja huko mitaani na wengine ni ndugu zetu kabisa......je wewe ungefurahia kumuona nduguyo akiwa katika hali ile ya uteja....sasa mlanguzi wa madawa ya kulevya anastahili kukaa mahakamani kusikiliza kesi wakati tunafahamu ni jinsi gani mahakama zetu zinavyonuka rushwa......mtu kama huyu anatakiwa akamatwe mara moja na kuwekwa kizuizini.....kwa kuwa kukamatwa kwake kutazuia usambaaji wa madawa mitaani hasa kwa yale yaliyokuwa kwenye imaya yake na pengine anaweza akasaidia kupatikina kwa mtandao wote wa madawa na hivyo kuondosha kabisa kadhia hiyo......

Sio siri yapo mambo ya ajabu mengi ndani ya taifa hili ambayo yamewekwa mizizi na mifumo yetu mibovu ya kiuongozi na kiutawala......hivyo inatakiwa kiongozi mwenye maamuzi magumu na ya busara kwa faida kwa taifa ili kuweka mambo sawa.....ule muda wa kuchekeana na kubembelezana mahakamani usiwepo tena kwani ndio uliotufikisha hapa tulipo....kama ikiwezekana hizo sheria zifumuliwe upyaaa...hao watu watakaokutwa na hatia za kuhujumu mali za umma wachinjwe kabisa hadharani.......tumechoka sasa...
 
sidhani kama ina umuhimu!tume ya nyalali ilitoa pendekezo la kufuta sheria kandamizi 40+,hiyo hapo ikiwemo,pia tume ilishauri madaraka ya raisi yapunguzwe...ukitaka turudi miaka ya 80 huoni kuwa haki nyingi za kiraia zitakuwa zimevunjwa?mbona kuna sheria nyingi za kumaliza ilo tatizo,pasipo kumtegemea raisi:pccb,dpp et al
Mkuu,
Hizo zote zipo hatukatai lakini zimetusaidia nini?
Kweli be realistic! Pesa inaletwa msaada kwa ajili ya taifa watu wachache wa naidivert ni billions of dollers hizo tasisisi unazitaja zina uwezo wa kuwadhibiti watu hawa? Don't you think a person with wealth more than normal is immune to the law?
Mimi sijui wewe ni mtu gani na wa Umri gani lakini nitakukumbusha tu mambo yaliopita katika Tabaka za utendaji na oungozi.
Baada ya Uhuru taifa letu lilitegemea sana Marekani wakati wa J.F.Kennedy, alipouwawa 1963 Nyerere alipannic afanye nini! Akaenda Russia masharti walimpa ili watukumbatie yalikuwa magumu ya kikommunism alipoenda China, wakamwambia ni vigumu kumwongoza tajiri au bepari na mwenyewe elimu nyingi ubane hivi vitu vitagain memontum taratibu! Akataifisha mabenki na kuleta mfumo mpya wa elimu..Universal Primary Education namshukuru Mungu Mimi nilimuuliza Standard VIII so after that nchi ilifuata new discipline of Socialism na tukawa na mwenendo nzuri wa kitabia na kiutendaji.
Nani alithubutu kula rushwa na kukomba pesa ya serikali wakati wa Nyerere na kusema hivyo ni vijisenti?
Ukisema tunarudi miaka ya 80 hapana! Sheria INA mlingano na tuna kitu kinaitwa Customary Law we can alter this or repeal it in accordance to the environment! Uliona serikali inatafuta shera mpya albino sheria yoyote inaweza tungwa na ikapitishwa na Bunge hali kadhalika ya ufisadi hata madawa! Uchafu nchi hii umezidi ndugu yangu tena wa pesa zetu.
China rushwa,dawa ni kifo far east, Bulgaria just to mention a few.
Kuna nchi nyingi madaraka haya ya Rais bado wanayo hakuna unyanyasaji nchi kama Rwanda, Angola, Namibia hata rais wake juzi amepata Tuzo.
Angalia mienendo ya nchi hizi tuache kufikiri pumba kama mwanajamvi mmoja anadiriki kusema kwamba eti hiyo itamfanya Magufuli kuwa full Dictator, tunapozungumzia Facts and Law tujaribu kuweka individuality kando.
 
Mimi nadhani kwa hapa ilipofikia nchi yetu hii sheria inafaa sana....kwani hata wezi na mafisadi pamoja na walanguzi wa mihadarati wana athiri haki za binaadamu......
Hebu chukulia kiongozi anayehujumu mradi wa maji kijijini kwa manufaaa yake na familia anawaathiri vipi wananchi kupata maji safi na salama na hivyo kuhatarisha usalama wao na wengi wao kufa kutokana na magonjwa ya milipuko kama taiphodi na kipindu pindu...je kiongozi kama huyu anastahili vipi kubaki uraiani wakati hata kwa matendo yake na tamaa zake anaathiri haki za binaadamu wenzake kuishi....???

Chukulia mfano kigogo anayefahamika kuingiza madawa ya kulevya...je kigogo huyo anaathiri na kuharibu maisha ya vijana wangapi....kila mmoja wetu ni shahidi wa utitiri wa mateja huko mitaani na wengine ni ndugu zetu kabisa......je wewe ungefurahia kumuona nduguyo akiwa katika hali ile ya uteja....sasa mlanguzi wa madawa ya kulevya anastahili kukaa mahakamani kusikiliza kesi wakati tunafahamu ni jinsi gani mahakama zetu zinavyonuka rushwa......mtu kama huyu anatakiwa akamatwe mara moja na kuwekwa kizuizini.....kwa kuwa kukamatwa kwake kutazuia usambaaji wa madawa mitaani hasa kwa yale yaliyokuwa kwenye imaya yake na pengine anaweza akasaidia kupatikina kwa mtandao wote wa madawa na hivyo kuondosha kabisa kadhia hiyo......

Sio siri yapo mambo ya ajabu mengi ndani ya taifa hili ambayo yamewekwa mizizi na mifumo yetu mibovu ya kiuongozi na kiutawala......hivyo inatakiwa kiongozi mwenye maamuzi magumu na ya busara kwa faida kwa taifa ili kuweka mambo sawa.....ule muda wa kuchekeana na kubembelezana mahakamani usiwepo tena kwani ndio uliotufikisha hapa tulipo....kama ikiwezekana hizo sheria zifumuliwe upyaaa...hao watu watakaokutwa na hatia za kuhujumu mali za umma wachinjwe kabisa hadharani.......tumechoka sasa...
Asante mkuu.
 
Inategemea na aina ya rais, nyerere hakuwa mfanyabiashara wala kuwa na tamaa ya pesa/mali ndio maana alichukia ufisadi na hakuwa tayari kuona mtu anachota pesa za umma na kusema ni vijisenti au hela ya mboga.
 
Mkuu umenena vyema sana....ubaya ni kwamba watu wanapofushwa macho na propaganda za mabeberu kwenye kichaka cha HAKI ZA BINAADAMU WAKATI WAO WENYEWE HAWAHESHIMU HATA CHEMBE YA HAKI ZA BINAADAMU.....
Katika mataifa ambayo yako makini sana na masuala yanayohusu jamii zao na tena kuyatungia sheria kali kabisa ni hayo yanayojiita au kujinasibu kutetea haki za binaadamu....yaani kwao haki za binadamu zinakuwa issue kama zikivunjwa kwenye mataifa mengine lakini sio kwrnye mataifa yao......unaweza kuniambia kuwa wale wafungwa wote waliokuwa Guantanamo walihukumiwa kwenye mahakama zipi...?? Lakini kikubwa kilichowafanya mpaka wakawa pale ni kwa kuwa tishio kwa usalama wa taifa la Marekani nikiwa na maana wananchi wa Marekani......sasa kule kuwasweka watu kama wale ndani hakuvunji haki za binaadamu....au haki za binadamu zinakuwa zimevunjika kwa kumuweka fisadi au mlanguzi wa madawa ya kulevya ndani...???

Hata kwa akili ya kawaida unaweza kuona ni jinsi gani hawa watu weupe hawatutakii mema......

Bado nasisitiza kuwa hapa ilipofikia nchi yetu anahitajika kiongozi dikteta hata zaidi ya Hitler ili kuweka mambo sawa.....kwani ni dhahiri kuwa kila jipu litakaloibuka ukilikamua sana ndani unakutana sura ya kiongozi mkubwa wa umma....sasa hapo kama hutaiondoa aibu na kuweka maslahi ya taifa mbele huwezi kulikamua jipu kana hilo......siku hizi mtu akishahamiana na viongozi kadhaa wa serikalini basi imeshakuwa shida hata kama akivunja sheria na akikamatwa analeta dharau kwa jeshi la polisi kwani anajua kuwa ana kinga.....

Sisi kama wananchi na wazalendo wa taifa hili tunataka mambo haya yakome na kuisha kabisa.....

YAANI IMEFIKIA KIPINDI SASA WATU WANAONA KERO KUISHI NDANI YA NCHI YAO...MPAKA WENGINE WANATAMANI WANGEZALIWA PAKA AU MBWA ULAYA...
 
Usinisahihishe ujinga hiyo typographic error na smart phone sio Mimi if you can't Contribute on the thread don't pose your noisense here. Mimi nimeenda shule sina elimu ya photocopy au vyeti vya kugushi. Respect yourself.

= nonsense
= kughushi

Inaonesha hiyo shule ulienda kusomea ujinga.

Nimekuuliza swali juu huko kutokana na mada yako hujajibu. Kulikoni?
 
Hahaha kuna shule inafundisha mtu ujinga?isipokuwa yule anakalia kukosoa keyboard ya phone ndio mjinga.

Sote tunatumia hiyo "keyboard ya phone". Upuuzi uandike wewe usingizie keyboard, labda hujuwi kuitumia.

Naam, kuna shule zinafundisha ujinga, mojawapo ni hiyo uliyokwenda wewe.
 

Naam, hiyo ni habari ya kweli kabisa na hata ukienda kwenye mainstream [credible] media ipo.

Ipo CNN, ipo FOX News, ipo USA Today, ipo WSB-TV, ipo AJC, ipo AP, ipo Reuters, ipo Yahooo News, na kadhalika.

Uwepo wa hiyo habari kwenye hicho chanzo chako haimaanishi hicho chanzo kuwa si cha tashtiti.

Soma hapa chini [kama unaweza kusoma na kuelewa].

Celebtricity.com is the most notorious entertainment website in the world with the most shocking Satire News to keep its visitors in a state of disbelief.
Please feel free to send us your inquiry or any questions below.
We will contact you shortly !
Thanks !!!


Advertise/Contact Us
 
Naam, hiyo ni habari ya kweli kabisa na hata ukienda kwenye mainstream [credible] media ipo.

Ipo CNN, ipo FOX News, ipo USA Today, ipo WSB-TV, ipo AJC, ipo AP, ipo Reuters, ipo Yahooo News, na kadhalika.

Uwepo wa hiyo habari kwenye hicho chanzo chako haimaanishi hicho chanzo kuwa si cha tashtiti.

Soma hapa chini [kama unaweza kusoma na kuelewa].

Celebtricity.com is the most notorious entertainment website in the world with the most shocking Satire News to keep its visitors in a state of disbelief.
Please feel free to send us your inquiry or any questions below.
We will contact you shortly !
Thanks !!!


Advertise/Contact Us

Na hii pia:

This 19-week old baby lived only minutes after birth, but touched millions
 
Naam, hiyo ni habari ya kweli kabisa na hata ukienda kwenye mainstream [credible] media ipo.

Ipo CNN, ipo FOX News, ipo USA Today, ipo WSB-TV, ipo AJC, ipo AP, ipo Reuters, ipo Yahooo News, na kadhalika.

Uwepo wa hiyo habari kwenye hicho chanzo chako haimaanishi hicho chanzo kuwa si cha tashtiti.

Soma hapa chini [kama unaweza kusoma na kuelewa].

Celebtricity.com is the most notorious entertainment website in the world with the most shocking Satire News to keep its visitors in a state of disbelief.
Please feel free to send us your inquiry or any questions below.
We will contact you shortly !
Thanks !!!


Advertise/Contact Us
Hivi kwanini watu wanakua na ID'S zaidi ya moja ? Halafu mbaya zaidi utumiaji wa hizo ID'S tofauti unalandana ?
Samahani kwa kutoka nje ya mada
 
Back
Top Bottom