Kuomba na kunyimwa?

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
17,277
Reaction score
40,928
Umewahi kuomba jambo fulani ukanyimwa, ilhali unajua kabisa yule mtu alikuwa nalo ila akaamua tu kutokukupa?
(wengine husema akakaza ,akadinda)

Kuomba aibu no uno
Kunyimwa aibu no two
kutangazwa aibu no 3

Kuomba halafu ukanyimwa ni aibu 🤣🤣
Ni kama umejidhalilisha halafu bado husaidiki
Yaani umejianika, umeweka wazi hitaji lako, lakini mwisho wa siku hupewi ng'oo 🤪

Wewe umewahi kuomba nini ukanyimwa? Na ulijisikiaje?

Mara nyingi muombaji akinyimwa hujuta na kutamani asingethubutu kuomba kabisa lakini ni too late 😁

Lakini pia kuna msemo unasema, Ukinyimwa, unajifunza kutafuta vya kwako ( Wahenga🤔)

Lakini sasa najiuliza...
Hivi kweli kila kitu kinaweza kupatikana bila kuomba? 🤪

Au kuna mambo ambayo bila kuomba huwezi kuyapata kamwe? 🤔

Weekend hiyoooo

NB : Kulombana sio anasa

ShesRise_1 🖐
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…