Kuolewa SIO bahati...USIBAHATISHE!

Kuwa mtoto wa mama na kuona kua kuoa/olewa ni bahati kunahusiana vipi?
Maana yake mtoto wa mwanamke mwenye Jinsia ya Kiume lazima apate bahati kutoka kwa MUNGU.
Mwanamke mwema anatoka kwa MUNGU au unasemaje?
 
Hua nashangazwa sana na kauli isemayo "kuolewa ni bahati" toka kwa wanaume na hata wanawake. Kauli hii hua inatoka kwa watu wanaoamini kwamba kwa kuolewa, mwanamke anakua amefanyiwa FAVOUR, AMESAIDIWA au AMEPEWA ZAWADI kana kwamba mwanamke pekee ndie anaefaidika na hiyo ndoa. Na hiyo bahati yenyewe inayotokana na kuolewa huko sio kupata mume ambae anastahili kuitwa mume bali ni kupata mahali pa kulala, chakula na mavazi. Wengine hua wanafika mbali kiasi cha kuwauliza wenzi wao moja kwa moja "unalalamika nini wakati unakula, unalala na unavaa vizuri?" pale mwanamke anapoonyesha kutoridhisha na namna mahusiano yao ndani ndoa yanavyoenda mf. mume kutokua mwaminifu, kutokuwepo nyumbani muda wa kutosha, kulewa sana, kumdharau mkewe n.k .

Ina maana wanawake wanaolewa ili wale, walale na wavae? Walipokua kwa wazazi wao au wakijitegemea waliishi bila kula, kuvaa na kulala ndani ya nyumba?

Kinachonisikitisha ni kuwa baadhi ya wanawake wanaunga mkono mawazo haya. Wanakubali kuchukuliwa kama watu wanaopewa msaada kwa kuolewa.

Binafsi siamini wala sioni ni kwa namna gani "kuolewa ni bahati". Kwangu mimi bahati ipo kwenye kumpata mtu ambae anaelewa nini maana ya ndoa na kuiheshimu ndoa yake, anaempenda mwenzi wake, anaemheshimu mwenzi wake pamoja na mawazo yake, anaemsikiliza mwenzake, anaejielewa na kujitahidi kumwelewa mwenzake, aliye tayari kujitoa kwa mwenzake, anaejua na kutimiza majukumu yake, anaejitahidi kumfurahisha mwenzake kwa maneno na matendo. Vivo hivyo kwa wanaume. . . . wenye bahati sio waliooa bali ni waliooa wanawake wenye sifa nilizotanguliza hapo juu.

Kuoa/kuolewa sio bahati hivyo usibahatishe.


Kitendo cha kuolewa ni bahati hayo mengine ni matokeo tu. Na mara nyingi husababishwa na tamaa na uchu wa mali wa akina dada wengi. Wachumba wazuri wanaojiheshimu ila wasio na uwezo hukataliwa kwa misingi ya kukosa mali. Mifani ninayo mingi sana.
 
Kuolewa ni bahati ukimpata mtu ambae anaelewa nini maana ya ndoa na kuiheshimu ndoa yake, anaempenda mwenzi wake, anaemheshimu mwenzi wake pamoja na mawazo yake, anaemsikiliza mwenzake, anaejielewa na kujitahidi kumwelewa mwenzake, aliye tayari kujitoa kwa mwenzake, anaejua na kutimiza majukumu yake, anaejitahidi kumfurahisha mwenzake kwa maneno na matendo. Vivo hivyo kwa wanaume. . . . wenye bahati sio waliooa bali ni waliooa wanawake wenye sifa nilizotanguliza hapo juu.

Tunasema ni bahati kwa kuwa wenye sifa ulizotaja hapo juu hawako wengi,hivyo ukibahatika kumpata lazima ujione mwenye bahati.

Tena Lizzy kuna wanawake wanatamani tu harusi nae eti avae shela,afanyiwe send off,mawazo ya ndoa na changamoto zake wala hayamuumizi kichwa.....mradi naye katoka kwa wazazi kahamia kwa mwanaume, akazae huko na kuishi huko....!!
 
kuolewa ni bahati 2 pale ambapo utakuwa umebahatika kuishi na m2 anayekupenda!
 
Kuolewa ni bahati ukimpata mtu ambae anaelewa nini maana ya ndoa na kuiheshimu ndoa yake, anaempenda mwenzi wake, anaemheshimu mwenzi wake pamoja na mawazo yake, anaemsikiliza mwenzake, anaejielewa na kujitahidi kumwelewa mwenzake, aliye tayari kujitoa kwa mwenzake, anaejua na kutimiza majukumu yake, anaejitahidi kumfurahisha mwenzake kwa maneno na matendo. Vivo hivyo kwa wanaume. . . . wenye bahati sio waliooa bali ni waliooa wanawake wenye sifa nilizotanguliza hapo juu.

Tunasema ni bahati kwa kuwa wenye sifa ulizotaja hapo juu hawako wengi,hivyo ukibahatika kumpata lazima ujione mwenye bahati.

Tena Lizzy kuna wanawake wanatamani tu harusi nae eti avae shela,afanyiwe send off,mawazo ya ndoa na changamoto zake wala hayamuumizi kichwa.....mradi naye katoka kwa wazazi kahamia kwa mwanaume, akazae huko na kuishi huko....!!
kuolewa ni nini?
 
Tatizo nyie wanawake good husband ni yule mwenye pesa. Ingekuwa kweli mnatafuta good husband msinge lialia hivi.
Tatizo la baadhi ya wanawake, kama ambavyo ni tatizo la baadhi ya wanaume kutumia kigezo cha sura kuchagua mke.
 
Maana yake mtoto wa mwanamke mwenye Jinsia ya Kiume lazima apate bahati kutoka kwa MUNGU.
Mwanamke mwema anatoka kwa MUNGU au unasemaje?
Kama kupata mwanamke mwema kutoka kwa Mungu ndio bahati basio KUOA sio bahati ila KUMUOA MWANAMKE ALIYETOKA KWA MUNGU ndio bahati.
 
Tatizo la baadhi ya wanawake, kama ambavyo ni tatizo la baadhi ya wanaume kutumia kigezo cha sura kuchagua mke.
Duh sasa uwe na mwanamke ambaye humtamani?
Sura lazima ndio vitu vya ndani. Unajua kila mtu huwa na kitu anachovutiwa kwa mwanamke.
 
Tatizo la baadhi ya wanawake, kama ambavyo ni tatizo la baadhi ya wanaume kutumia kigezo cha sura kuchagua mke.

Sura ni kigezo muhimu sana, haswa ukipata mwenye Sura nzuri na tabia nzuri, dunia utaiona tamu. Lakini akiwa na sura mbovu sana na tabia nzuri ndi mwanzo wa nyumba ndogo.
 
Kitendo cha kuolewa ni bahati hayo mengine ni matokeo tu. Na mara nyingi husababishwa na tamaa na uchu wa mali wa akina dada wengi. Wachumba wazuri wanaojiheshimu ila wasio na uwezo hukataliwa kwa misingi ya kukosa mali. Mifani ninayo mingi sana.


Uzuri wa mtu haupo kwenye kuwa na mali ama kutokua na mali. Wapo wanaume wasio hata na uwezo wa kununua suruali ya tatu ila tabia zao haziwezi kumfanya mwanamke aone alibahatika kuolewa nae.
 
kuolewa ni nini?

Hata sijui...ningesema kukubali kwa sababu anazojua mhusika kuishi na mwanaume kwa taratibu zinazotambulika kidini,kiserikali,kijamii etc,...but siku hizi nasikia wanawake wanaoa wanaume na wanawake wenzao, wanaume nao wanaoa wanaume wenzao....jitahidi tu na wewe Smile kutafsiri....lol....umefanikiwa ile ishu??? he he he...tukutane mailisita!
 
Kuolewa ni bahati ukimpata mtu ambae anaelewa nini maana ya ndoa na kuiheshimu ndoa yake, anaempenda mwenzi wake, anaemheshimu mwenzi wake pamoja na mawazo yake, anaemsikiliza mwenzake, anaejielewa na kujitahidi kumwelewa mwenzake, aliye tayari kujitoa kwa mwenzake, anaejua na kutimiza majukumu yake, anaejitahidi kumfurahisha mwenzake kwa maneno na matendo. Vivo hivyo kwa wanaume. . . . wenye bahati sio waliooa bali ni waliooa wanawake wenye sifa nilizotanguliza hapo juu.

Tunasema ni bahati kwa kuwa wenye sifa ulizotaja hapo juu hawako wengi,hivyo ukibahatika kumpata lazima ujione mwenye bahati.

Tena Lizzy kuna wanawake wanatamani tu harusi nae eti avae shela,afanyiwe send off,mawazo ya ndoa na changamoto zake wala hayamuumizi kichwa.....mradi naye katoka kwa wazazi kahamia kwa mwanaume, akazae huko na kuishi huko....!!

Hehehehe I know dearest. Wenyewe bahati ipo kwenye kuonekana nae kaolewa na sio kwenye maisha yatakavyoenda baada ya hizo chereko chereko za siku moja.
 
Back
Top Bottom