Kununua laptop mtandaoni ebay

Kununua laptop mtandaoni ebay

Asclepius

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
694
Reaction score
730
Wakuu nimekutana na hii laptop ebay mtandaoni ina specs nzuri mno kama core i7 hdd 1tb inauzwa kama usd 150 katika malipo imeonekana inatakiwa niwapatie kadi yangu ya benki pamoja na namba ya siri...... Hapo nimekwama kidogo naombeni uhakika juu ya hili suala na usalama wa pesa yangu maana wamesema shipping tc free from spain
 
Nasikia Ebay wamefungua branch yao pale Masaki
 
tegemea io mashine kuwa dual core na siyo i7
kwa roho ya huruma HDD itakuwa 320gb
spana za kutosha
na imechoa kila kila kitu
 
Wakuu nimekutana na hii laptop ebay mtandaoni ina specs nzuri mno kama core i7 hdd 1tb inauzwa kama usd 150 katika malipo imeonekana inatakiwa niwapatie kadi yangu ya benki pamoja na namba ya siri...... Hapo nimekwama kidogo naombeni uhakika juu ya hili suala na usalama wa pesa yangu maana wamesema shipping tc free from spain
Tumia paypal!
 
i7 for 150? Malipo ya eBay si yana ulinzi? Weka link ya hiyo laptop. Mwuzaji ana reputation gani? Ana reviews gani?
 
Wakuu nimekutana na hii laptop ebay mtandaoni ina specs nzuri mno kama core i7 hdd 1tb inauzwa kama usd 150 katika malipo imeonekana inatakiwa niwapatie kadi yangu ya benki pamoja na namba ya siri...... Hapo nimekwama kidogo naombeni uhakika juu ya hili suala na usalama wa pesa yangu maana wamesema shipping tc free from spain
Habari mkuu,

Sio kukupinga, ila kwa kawaida (kwa sheria za eBay) wauzaji wengi sana wanatumia mfumo wa kulipia wa PayPal.
Na wengi unakuta wanaweka wazi kabisa "ONLY PAYPAL ACCEPTED"

Wa kulipia na Kadi bado wapo, ila kwa wengi wao hawatahitaji PIN yako (wanaofanya hivyo ni wezi). Watakachohitaji sana sana ni card number, expiration date, na CVC bas. Ambazo hizi zinatumika kuhakikisha uhalisia (authenticity) wa kadi yako. Wewe mwisho wa siku ndio una'authorize pesa itoke kwenye account kwenda kwa muuzaji.

Halafu, mkuu kuwa makini na kununua bidhaa kisa umeona bei iko chini.
Jaribu hata kuangalia ITEM DESCRIPTION upate kujua kama bidhaa ni mpya/used/sold for parts. Items zingine unakuta bado ziko kwenye listings lakini seller hayuko behind that anymore, au seller yuko kiwasiwasi (shady).
Angalia pia "Approval Ratings" za huyo muuzaji. Mara nyingi binafsi nimejiwekea imani na Seller mwenye ratings kwanzia 96%

IMG_20171112_112049.jpg


Angalia hapo utaona Seller wa bidhaa hii ana approval ratings ya kuaminika kabisa 100%.

IMG_20171112_112211.jpg


Then click hapo, utaona ratings from Positive, Neutral to Negative ndani ya Mwezi mpaka Miezi 6 iliyopita.
Sasa angalia Neutral na Negative comments, angalia kama kuna hata moja inahusiana na "Item Number" ya bidhaa unayotaka kuinunua.
Pia jinsi unavyoona malalamiko mengi changanya na akili zako ufanye maamuzi ya busara kabla hujaamua kununua toka kwa huyo muuzaji.

IMG_20171112_112243.jpg


Hii ndio item namba ya bidhaa. Angalia hii then cheki kwenye reviews kama item number yako (ambayo ndio bidhaa) imetajwa kokote (iwe kwenye positive, neutral, au negative reviews).

Screenshot_2017-11-12-11-23-17-365_com.ebay.mobile.png


Angalia reviews za wanunuzi waliowahi nunua toka kwa muuzaji huyo. Wanaongeleaje huduma/bidhaa zake.

Zaidi ya hayo, WASILIANA na muuzaji. Na soma vizuri Item Description, usije agiza parts/scrap au used items kisa kufurahia bei che.

Yangu ni hayo tu.
 
Habari mkuu,

Sio kukupinga, ila kwa kawaida (kwa sheria za eBay) wauzaji wengi sana wanatumia mfumo wa kulipia wa PayPal.
Na wengi unakuta wanaweka wazi kabisa "ONLY PAYPAL ACCEPTED"

Wa kulipia na Kadi bado wapo, ila kwa wengi wao hawatahitaji PIN yako (wanaofanya hivyo ni wezi). Watakachohitaji sana sana ni card number, expiration date, na CVC bas. Ambazo hizi zinatumika kuhakikisha uhalisia (authenticity) wa kadi yako. Wewe mwisho wa siku ndio una'authorize pesa itoke kwenye account kwenda kwa muuzaji.

Halafu, mkuu kuwa makini na kununua bidhaa kisa umeona bei iko chini.
Jaribu hata kuangalia ITEM DESCRIPTION upate kujua kama bidhaa ni mpya/used/sold for parts. Items zingine unakuta bado ziko kwenye listings lakini seller hayuko behind that anymore, au seller yuko kiwasiwasi (shady).
Angalia pia "Approval Ratings" za huyo muuzaji. Mara nyingi binafsi nimejiwekea imani na Seller mwenye ratings kwanzia 96%

View attachment 629268

Angalia hapo utaona Seller wa bidhaa hii ana approval ratings ya kuaminika kabisa 100%.

View attachment 629272

Then click hapo, utaona ratings from Positive, Neutral to Negative ndani ya Mwezi mpaka Miezi 6 iliyopita.
Sasa angalia Neutral na Negative comments, angalia kama kuna hata moja inahusiana na "Item Number" ya bidhaa unayotaka kuinunua.
Pia jinsi unavyoona malalamiko mengi changanya na akili zako ufanye maamuzi ya busara kabla hujaamua kununua toka kwa huyo muuzaji.

View attachment 629273

Hii ndio item namba ya bidhaa. Angalia hii then cheki kwenye reviews kama item number yako (ambayo ndio bidhaa) imetajwa kokote (iwe kwenye positive, neutral, au negative reviews).

View attachment 629274

Angalia reviews za wanunuzi waliowahi nunua toka kwa muuzaji huyo. Wanaongeleaje huduma/bidhaa zake.

Zaidi ya hayo, WASILIANA na muuzaji. Na soma vizuri Item Description, usije agiza parts/scrap au used items kisa kufurahia bei che.

Yangu ni hayo tu.
Nashukuru sana mkuu asante sana
 
Back
Top Bottom