Kunani watanzania?

Kaniki1974

JF-Expert Member
Dec 2, 2008
352
22
Huu upole wa watanzania, umetoka wapi? Una maana kweli kwa maendeleo ya nchi? Utatutoa kimaendeleo?

Ukiwa mwanasiasa unaweza kuwaahidi uongo, ukawadharau na hata kuwanyanyasa na watakuangalia tu na hata kuzidi kukuchagua/kukupigia kura;

Rais anayumbisha na kuharibu uchumi wa nchi kwa utawala mbovu usio na maono, umejaa rushwa, urafiki, kufahamiana, ufisadi, matumizi yasiyo ya lazima, yasiyozingatia vipaumbele, serikali kubwa kupita uwezo n.k na bado watamchagua kwa awamu nyingine azidi kuharibu nchi;

Dereva katika basi anaweza kuendesha atakavyo, kutukana, kusababisha ajali, kuwashusha abiria njiani n.k lakini watanzania watakaa kimya na kuogopa kumkemea;

Baa medi anaweza kuamua kutomrudishia mteja wake chenji au kurudisha chenji pungufu lakini mteja atamwangalia tu au kuondoka zake;

Viongozi mbalimbali wanatukana watu hovyo, wanawanyanyasa, hawafanyi kazi ipasavyo yet, watanzania watabaki kimya na kuogopa tu;

Makeshia katika mabenki hawafanyi kazi, wanatukana wateja, wanazembea na kusababisha mafoleni, yet wateja wapo kimya na hata kuongea kwa sauti wanaogopa!;

Wazungu kila kukicha wanatuibia almasi Mwadui, dhahabu kule Shinyanga, Tanzanite Arusha, uranium Dodoma n.k na kunyanyasa wazawa kwa kila jinsi lakini hawapati upinzani wowote;

Baadhi ya wawekezaji wanatukana na kunyanyasa raia hovyo hovyo tu katika mahoteli, madukani na katika biashara zao lakini hawapati upinzani wowote;

Walimu wananyanyasa hovyo wanafunzi mashuleni na vyuoni;

Watu wanahukumiwa vifungo vya maisha kwa sababu dhaifu/za uongo na hakuna hata wanaopinga;

Na mengine mengi tu.

Huu sijui upole, ujinga , ukarimu n.k UNA MAANA KWELI kwa maendeleo ya Tanzania na watu wake? Kwa nini watu hawa hawatiwi adabu na nguvu ya umma? Kwa nini blah blah hizi zinaachwa kuendelea?
 
So twastahili kila aina ya hujuma! God have mercy!
Hivi besti hukufanikiwa kusoma habari ya mwizi aliyefanikiwa kuingia kwenye viunga vya IKULU ya JK na kuiba maua kibao yenye thamani ya tshs 5000, na wakati anatoka ndipo alipowasogelea askari, na kwa aibu wakamshika na kuanza kumshughulikia...Huoni kwamba we are good for nothing?
 
Hivi besti hukufanikiwa kusoma habari ya mwizi aliyefanikiwa kuingia kwenye viunga vya IKULU ya JK na kuiba maua kibao yenye thamani ya tshs 5000, na wakati anatoka ndipo alipowasogelea askari, na kwa aibu wakamshika na kuanza kumshughulikia...Huoni kwamba we are good for nothing?

Kwi kwi kwiiiiii.... nilisikia, tusikate tamaa any way. Hope best hukubali tubaki kama hivi daima!
 
Huu upole wa watanzania, umetoka wapi? Una maana kweli kwa maendeleo ya nchi? Utatutoa kimaendeleo?

Ukiwa mwanasiasa unaweza kuwaahidi uongo, ukawadharau na hata kuwanyanyasa na watakuangalia tu na hata kuzidi kukuchagua/kukupigia kura;

Rais anayumbisha na kuharibu uchumi wa nchi kwa utawala mbovu usio na maono, umejaa rushwa, urafiki, kufahamiana, ufisadi, matumizi yasiyo ya lazima, yasiyozingatia vipaumbele, serikali kubwa kupita uwezo n.k na bado watamchagua kwa awamu nyingine azidi kuharibu nchi;

Dereva katika basi anaweza kuendesha atakavyo, kutukana, kusababisha ajali, kuwashusha abiria njiani n.k lakini watanzania watakaa kimya na kuogopa kumkemea;

Baa medi anaweza kuamua kutomrudishia mteja wake chenji au kurudisha chenji pungufu lakini mteja atamwangalia tu au kuondoka zake;

Viongozi mbalimbali wanatukana watu hovyo, wanawanyanyasa, hawafanyi kazi ipasavyo yet, watanzania watabaki kimya na kuogopa tu;

Makeshia katika mabenki hawafanyi kazi, wanatukana wateja, wanazembea na kusababisha mafoleni, yet wateja wapo kimya na hata kuongea kwa sauti wanaogopa!;

Wazungu kila kukicha wanatuibia almasi Mwadui, dhahabu kule Shinyanga, Tanzanite Arusha, uranium Dodoma n.k na kunyanyasa wazawa kwa kila jinsi lakini hawapati upinzani wowote;

Baadhi ya wawekezaji wanatukana na kunyanyasa raia hovyo hovyo tu katika mahoteli, madukani na katika biashara zao lakini hawapati upinzani wowote;

Walimu wananyanyasa hovyo wanafunzi mashuleni na vyuoni;

Watu wanahukumiwa vifungo vya maisha kwa sababu dhaifu/za uongo na hakuna hata wanaopinga;

Na mengine mengi tu.

Huu sijui upole, ujinga , ukarimu n.k UNA MAANA KWELI kwa maendeleo ya Tanzania na watu wake? Kwa nini watu hawa hawatiwi adabu na nguvu ya umma? Kwa nini blah blah hizi zinaachwa kuendelea?

K 1974,
Sababu kubwa ya uoza ulioorodhesha hapo juu ni kuwa Nchi haina Utawala wa sheria. Mahakama yenyewe haijitambui inaendeshwa na wanasiasa. Angalia mfano huo wa Polisi kumpiga huyo Mwizi wa maua...........na Taasisi nyigine zote zinakwenda kimungu mungu tu. Na isiposimama sheria hakuna haki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom