yellow eyes
JF-Expert Member
- Mar 6, 2018
- 2,904
- 3,353
Ujumbe mzuri sana mkuu,Unajikuta unaanza kumpenda mtu, taratibu mnaanza ukaribu. Unamchukulia kama ni mtu special kwako. Unampa attention yote.
.
Mnafanya mengi ya kukumbukwa, maisha ya mahusiano unaona matamu. Kwake unaona ndio umetua mzigo.
.
Lakini, katikati ya safari mambo yanaanza kubadilika.
.
Mawasiliano yanapungua, uaminifu unapotea na mapenzi yanapoa. Masikini, unajitahidi kwa hali na mali kurudisha mapenzi, unajitahidi ku-fix mambo yasiharibike, unaweka jitihada kuokoa mapenzi lakini jitihada ni zako peke yako, mwenzako yuko mbali.
.
Unachoka na kukata tamaa. Unalia kila siku iitwayo leo, huna raha, moyo unauma, akili imesimama, chakula hakipandi. Vidonda vya tumbo vimechachamaa.
.
Unatamani umsahau lakini akili na moyo unagoma kabisa.
.
Unatakiwa uelewe hili, toka mwanzo yale hayakuwa mapenzi. Ilikuwa ni infatuation. Tena shukuru umejua mapema. Kwa sababu Mwenye upendo huvumilia, hufadhili; mwenye upendo hana wivu, hajidai, wala hajivuni.
.
Mwenye upendo hakosi adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya, hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli. Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote. Upendo hauna kikomo kamwe.
.
Kubaliana na hali, kuteleza sio kuanguka. Ipo siku utapata mtu atakaekupenda kweli na hapo ndipo utakapoamini kuwa kuna watu wanajua kupenda.
.
GOD BLESS YOU!
Sent using Jamii Forums mobile app
Haya mapenzi bwana unaweza kujikuta umempenda mtu kumbe siyo chaguo lako. Anakutenda na kukufanyia mabaya ya kila aina. Ila kumbe hayo yanakuwa kama darasa au daraja la kukuvusha kuelekea kwa mtu sahihi.
Sent using Jamii Forums mobile app
