Kuna watu hufanya mapenzi yachukiwe

Kuna watu hufanya mapenzi yachukiwe

Chrix_Tz

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2015
Posts
880
Reaction score
1,101
Unajikuta unaanza kumpenda mtu, taratibu mnaanza ukaribu. Unamchukulia kama ni mtu special kwako. Unampa attention yote.
.
Mnafanya mengi ya kukumbukwa, maisha ya mahusiano unaona matamu. Kwake unaona ndio umetua mzigo.
.
Lakini, katikati ya safari mambo yanaanza kubadilika.
.
Mawasiliano yanapungua, uaminifu unapotea na mapenzi yanapoa. Masikini, unajitahidi kwa hali na mali kurudisha mapenzi, unajitahidi ku-fix mambo yasiharibike, unaweka jitihada kuokoa mapenzi lakini jitihada ni zako peke yako, mwenzako yuko mbali.
.
Unachoka na kukata tamaa. Unalia kila siku iitwayo leo, huna raha, moyo unauma, akili imesimama, chakula hakipandi. Vidonda vya tumbo vimechachamaa.
.
Unatamani umsahau lakini akili na moyo unagoma kabisa.
.
Unatakiwa uelewe hili, toka mwanzo yale hayakuwa mapenzi. Ilikuwa ni infatuation. Tena shukuru umejua mapema. Kwa sababu Mwenye upendo huvumilia, hufadhili; mwenye upendo hana wivu, hajidai, wala hajivuni.
.
Mwenye upendo hakosi adabu, hatafuti faida yake binafsi, wala hana wepesi wa hasira; haweki kumbukumbu ya mabaya, hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli. Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote. Upendo hauna kikomo kamwe.
.
Kubaliana na hali, kuteleza sio kuanguka. Ipo siku utapata mtu atakaekupenda kweli na hapo ndipo utakapoamini kuwa kuna watu wanajua kupenda.
.
GOD BLESS YOU!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Teh teh teh teh teh
naijatwittersavages-20190104-0001.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani mkuu ila nimejufunza mengi kupitia hayo pia.... Kwangu ni km shule ilikua....

Sent using Jamii Forums mobile app
Me nakupa hongera,hilo ulilopitia sio baya ni jambo zuriii mnooo kwa mustakabali wa mahusiano yako yajayo,ulikiwa tuu darasani kujifunza sasa umefuzu,.hongera sana!!!!

Muda ndio jibu la kila kitu.
 
Me nakupa hongera,hilo ulilopitia sio baya ni jambo zuriii mnooo kwa mustakabali wa mahusiano yako yajayo,ulikiwa tuu darasani kujifunza sasa umefuzu,.hongera sana!!!!

Muda ndio jibu la kila kitu.
Axante sana mamaa now nimekua wa tofaut kupitia somo hilo.... Unajua kuna watu wapo kwaajili ya kuwapa watu fulani challenge ktk mahusiano km hivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
yani mwanaume mzima unalia kuachwa hawa madem waliojaa mtaani visu namna hio afu unalia lia.... mkishauriwa mtafute michepuko mara ooh ukimwi ooh sijui huyu nampenda..... sasa angalia unalia lia kama mtoto wa kike michepuko ina umuhimu sana kwenye kizazi chetu

W, G, S na D popote mlipo michepuko yangu mnasaidia sana hamjui tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom