Kuna wabunge bora wangekuwa wapiga debe stand

Kuna wabunge bora wangekuwa wapiga debe stand

UKAWA imeingiza mambo ya vyama vyao Bungeni kwa kuamini kuwa ndio mahala pekee pa kushawishi viongozi wa kitaifa. Ni nidhamu mbaya sana kumzomea mtu aliye kuzidi umri, achilia mbali mtu huyo kuwa kiongozi wa taifa ama lah. Hivyo kitu ambacho UKAWA walikifanya jama akisameheki, akivumiliki na wote wenye akili tumekilaani kile kitendo cha kuzomea Bungeni.

Mkuu HAMY-D;
Mbona unaufuata ule msemo wa kwetu; Nyani haoni kundule?? Katika maono yako, ni nani kati ya UKAWA na CCM wanaleta mambo yao mle bungeni?
Nakuomba uwe mkweli tu mkuu:
Unaunga mkono Dr Shein na mwenzake Kificho kuingia mle bungeni kwa nyadhifa walizo ingia nazo?? Naomba tu uwe mkweli. Hata mtoto wa darasa la nne anajua wazi kuwa Zanziba kuna mgogoro wa kisiasa. Mh. rais amekiri kuwa kuna "Majaribu ya kisiasa kule zenj"
Jiulize swali; Kumuingiza Dr na Kificho bungeni, kwenye bunge la JMT ndio kuyamaliza hayo majaribu ya kisiasa au kuyakuza?
Nadhani, endapo utayajibu kiufasaha hayo maswali, utaunga mkono UKAWA kutoka nje. Hawana njia nyingine kuelezea hisia zao baada ya weye kuunga mkono Spika aikanyage katiba
 
Ninapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wabunge kuwa zama za kutaka kujikweza na kuitwa "WAHESHIMIWA" wakati wanafanya mambo ya kipumbavu mbele ya macho ya wananchi wa Tanzania zimepitwa na wakati.

Ninaandika makala hii ili Watanzania wenzangu na hata baadhi ya wabunge mtakaoipata makala hii "muifoward" hadi iwafikie walengwa. Sioni haya kusema bunge la 11 lina wabunge wa aina mbili, yaani wabunge wenye busara na Wabunge "Malofa na wapumbavu" na wasio na busara. Hii inatokana na sababu zifuatazo:-

Utamaduni uliojengeka wa kusimama na kuzomea, kupiga mayowe unadhalilisha hadhi ya bunge na hata kama unaofanywa Nchi nyingine sio wa kuigwa maana hauna tija kwa jamii. Juzi katika mchakato wa kupata Naibu Spika tulishuhudia wabunge wakisimama na kupiga mayowe, Kubweka na kubwabwaja Ovyo kuzuia usikivu na utulivu. Hali hiyo ilizuia usikivu na kutunyima uhondo wa kusikia majibu ya maswali mazito toka kwa Mh. Silinde kwenda kwa Dr. Tulia.

Lakini pia wakati ndg Nape Nnauye ana uliza swali kwa mgombea u Spika wa UKAWA ndg. Ole Medeye wabunge wengine bila sababu walianza kupayuka kama walevi na kubwatuka Ovyo kuzuia Ole Medeye asijibu maswali. Hizo ni tabia za kihuni, Kipuuzi na kijinga.

Jambo lilioonyesha kiwango cha juu cha upumbavu wa baadhi ya wabunge ni baada ya Jana kutoka Bungeni tena kwa kufanya fujo. Ninasema ni upumbavu bila kuona haya ili mjue kuwa hatuna sababu ya kuheshumu na kufumbia macho tabia za kihuni kama zile.

Ni wazi kuwa wananchi tumewachagua ili mtuwakilishe na kutetea maslahi Yetu na wala sio kuleta ushabiki wa vyama vyenu.Pia mkumbuke kuwa hatukuwachagua kwa kuwa nyinyi mpo peke yenu katika jamii.

Wananchi tusimame kidete kukemea mambo mawili. La kwanza tukemee utovu wa nidhamu wa kuzomea Ovyo na utaratibu mbovu wa "Ndiyo Mzee"...

Kwa Leo naishia hapa.

Hivi unafikiri kuzomea kumeanza Tanzania? Dunia nzima hata huko Uingereza tulikoiga mfumo huu wa uongozi wabunge huzomea wanapoona haki inapindishwa. Acha kucram mambo!
Nchi zingine hata ngumi zinapigwa!
CCM lazima mheshimu katiba!
 
Mtoa mada jaribu kukuza weledi na ufahamu wako ktk masuala ya siasa za vyama vingi ndio uje utoe mada.

Kumbukumbu za bunge la 10 la jamhuri ya muungano zinatuonyesha kuwa Mh SUGU ni mmoja wa wabunge waliotolewa nje na askari wa bunge kichwa chini miguu juu. Sababu iliyotolewa ni "kutotii kiti na kufanya fujo bungeni".
Je, ni mbunge gani alipata KURA nyingi zaidi ya Mh SUGU katika uchaguzi uliopita?
Kama kuzomea, kupiga mayowe na kutoka nje ya bunge si lolote, kwa nini idadi ya wabunge wa vyama vya upinzani imeongezeka bungeni?
 
Pamoja na kwamba nimewapa UKAWA kura kwa hat trick level katika uchaguzi mkuu lakini kitendo cha juzi kwenye mchakato wa kupata naibu spika na jana vimenishusha imani juu yao.

Style hii wakiendelea nayo kwakwel sitauona uzalendo wao ulipo zaidi ya kufanya mambo kwa ajili ya public tension lakini isiyo na tija kwa taifa wala upinzani wenyewe.

Lazma itafutwe mbinu nyingine, haiwezekani kila bunge mnatoka na kuzomea matokeo yake mnapoteza muda lakini mnachokizomea kinaendelea na kupitishwa kama kilivyopangwa na kibaya zaidi posho mnachukua. #insanity
 
Back
Top Bottom