Kuna Uwezekano Sitapiga Kura

Kuna Uwezekano Sitapiga Kura

TANURU

Senior Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
162
Reaction score
9
Wakuu,

Kama hali ya mambo itaendelea kuwa mbaya zaidi sitegemei kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu. Pamoja na hali ya mambo kuendelea kuwa mbaya, Jambo pekee ambalo litanishawishi nipige kura ni iwapo tu wahusika halisi wa KAGODA watafikishwa mahakamani kabla ya mwaka huu wa fedha (2009/2010) kuisha.
 
Sikujua kama kuna wapuuzi duniani wa aina hii . kama unataka kubadili mambo lazima uwe katika duru.Nini kagoda wewe kuna makubwa zaidi. Lakini huwezi kukurupuka tu na kusema kama vile unafuata maji ya bahari ambayo uwa yanakupwa na kupwelea wakati huo huo lakini yakighaiori ujazo kwa kuelemea upande mmoja kubalansi dunia. Haki hupatikana ama kwa kura ama bunduki na siku zote bunduki haitoi haki kwa kuwa aliyeua hudhani wapow atakamkamua na kumuuliza kwanini umeua.Nyie mnaokataa kuingia katika kiulinge cha kupiga kura msiwafadhaishe wenzenu waache waamua.Nyie mnatufanya tusiwe na sauti hapa nchini.Plato alisema wanaume ndio wanaoamua mambo ya Athens na lazima wapige kura. Usikimbie kivuli chako ukabaki unahema siku ukionyeshwa mwanga kamili.Usipotumia kura unataka kugeuza somalia kwa kujaza hasira zisizokuwa na ukomo?Kura yako hata kama haitatosha itawapa watu salamu za heri au shari.Nenda kapige kura iwe Kagoda au kijigoda bila kuingiza wa kutosha bungeni utaendelea kuwa chizi mpaka kiama
 
Sikujua kama kuna wapuuzi duniani wa aina hii . kama unataka kubadili mambo lazima uwe katika duru.Nini kagoda wewe kuna makubwa zaidi. Lakini huwezi kukurupuka tu na kusema kama vile unafuata maji ya bahari ambayo uwa yanakupwa na kupwelea wakati huo huo lakini yakighaiori ujazo kwa kuelemea upande mmoja kubalansi dunia. Haki hupatikana ama kwa kura ama bunduki na siku zote bunduki haitoi haki kwa kuwa aliyeua hudhani wapow atakamkamua na kumuuliza kwanini umeua.Nyie mnaokataa kuingia katika kiulinge cha kupiga kura msiwafadhaishe wenzenu waache waamua.Nyie mnatufanya tusiwe na sauti hapa nchini.Plato alisema wanaume ndio wanaoamua mambo ya Athens na lazima wapige kura. Usikimbie kivuli chako ukabaki unahema siku ukionyeshwa mwanga kamili.Usipotumia kura unataka kugeuza somalia kwa kujaza hasira zisizokuwa na ukomo?Kura yako hata kama haitatosha itawapa watu salamu za heri au shari.Nenda kapige kura iwe Kagoda au kijigoda bila kuingiza wa kutosha bungeni utaendelea kuwa chizi mpaka kiama

Mkuu matusi ya nini? Bahati mbaya huo ndiyo msimamo wangu.
 
SIO UPUUZI
kupiga kura kuna maana kama
mpigaji kura anapata choice ya kuchagua,kama
anaona hakuna right choice,kutopiga kura pia ni aina
nyingine ya kutoa maamuzi.....
kama kuna pepsi na coca unaambiwa uchague,unaweza sema sichagui yeyote..
which is very understandable.......
 
Tanuru,

Kaka jitahidi twende si busara kususia uchaguzi - maana ukisusa wenzako wanakula - hawatakuonea huruma hata kidogo, please change your mind and move on.... Kumfikisha kagoda mahakani ni sawa na kuifikisha serikali yetu kwa pilato - jambo hili halitawezekana kabisa. kumbuka Bunge limeshindwa kumjua Kagoda ni nani? Chief haya ya kagoda, Richmond, Mwananchi gold, Melemeta, Tangold, Buzwagi, TRL na mengineyo yasituvunje moyo - Lets go guys...

Ambao hamjajiandikisha kupata kipande cha kupigia kura kama mimi please do that before saturday 27th.
 
Mi mwenzako misururu ya kujiandikisha kwenye daftar ndo inantia kichefchef.

Kadi yangu siioni. Kwanza niende polisi nikaandikishe card ilipotea. Nitoke hapo nikapange foleni ndefuuu. Siku zenyewe za kuhakiki majina kidogo sana.

Ok, mfano naamua kupiga moyo konde naenda kujiandikisha, najua ntachagua watu ambao mwisho wa siku hamna lolote. Maneno matamu kutaka kura (kula) tu. Viini macho vingii utafikiri maisha ya bongo ni mazingaombwe flani.

Argh!
 
Tanuru,

Kaka jitahidi twende si busara kususia uchaguzi - maana ukisusa wenzako wanakula - hawatakuonea huruma hata kidogo, please change your mind and move on.... Kumfikisha kagoda mahakani ni sawa na kuifikisha serikali yetu kwa pilato - jambo hili halitawezekana kabisa. kumbuka Bunge limeshindwa kumjua Kagoda ni nani? Chief haya ya kagoda, Richmond, Mwananchi gold, Melemeta, Tangold, Buzwagi, TRL na mengineyo yasituvunje moyo - Lets go guys...

Ambao hamjajiandikisha kupata kipande cha kupigia kura kama mimi please do that before saturday 27th.

Ushauri wako ni mzuri. Lakini haya mambo yasiyofaa tutaendelea nayo mpaka lini? Naomba pia tumsome Tripo9 hapo juu.

Pia naomba tujiulize wale watu ambao tunajiita wasomi wa nchi hii kwa nini hatujitokezi waziwazi na kuvisaidia vyama vya upinzani kuwa imara zaidi ili kuleta ushindani thabiti na kuhakikisha kuwa nchi yetu inaongozwa muda wote kwa kuweka utaifa mbele na si vinginevyo.
 
sisi wenzio tutapiga, tena tutapigia upinzani wala si sisiemu. wewe mwenye msimamo wa kukubali kushindwa vitani, endelea na msimamo wako, ila jua watu wa aina yako wanaweza kuwa ni wachache sana, kiasi kwamba hawana effect yoyote kwenye taifa letu. bye.
 
Hivi Watanzania wote wakishawishika kutokupiga kura, kutakuwa na uchaguzi?

Silaha ya mlalahoi ni kura yake. Akiamua kuitumia vema, akasema, sipigi kura mpaka hiki, na hiki, na hiki, na hiki, kifanyike, je, atakuwa amefanya sahihi ama la? Je, mlalahoi wa Tanzania ana ujasiri huo wa kususia uchaguzi?

./mwana wa haki
 
sisi wenzio tutapiga, tena tutapigia upinzani wala si sisiemu. wewe mwenye msimamo wa kukubali kushindwa vitani, endelea na msimamo wako, ila jua watu wa aina yako wanaweza kuwa ni wachache sana, kiasi kwamba hawana effect yoyote kwenye taifa letu. bye.

Ubungoubungo,

Post yako ni nzuri na wala usinielewe vibaya kuwa nawashawishi watu wasiende kupiga kura. Najizungumzia mimi mwenyewe. Ila ikitokea DR. SLAA akipitishwa na chama chake kuwa mgombea Urais, msimamo wangu unaweza kubadilika.
 
Hivi Watanzania wote wakishawishika kutokupiga kura, kutakuwa na uchaguzi?

Silaha ya mlalahoi ni kura yake. Akiamua kuitumia vema, akasema, sipigi kura mpaka hiki, na hiki, na hiki, na hiki, kifanyike, je, atakuwa amefanya sahihi ama la? Je, mlalahoi wa Tanzania ana ujasiri huo wa kususia uchaguzi?

./mwana wa haki

MwanaHaki

Umetoa changamoto nzuri sana.
 
sisi wenzio tutapiga, tena tutapigia upinzani wala si sisiemu. wewe mwenye msimamo wa kukubali kushindwa vitani, endelea na msimamo wako, ila jua watu wa aina yako wanaweza kuwa ni wachache sana, kiasi kwamba hawana effect yoyote kwenye taifa letu. bye.

Umejuaje kama yuko peke yake au wachache? Kwa taarifa yako wananchi wengi wamekosa imani na serikali na upinzani na mtu anaona bure aendelee na shughuli zake za maisha badala ya kupoteza muda na siasa. Kimsingi Tanuru ana pointi kama hakuna wala uadilifu kuna pointi gani ya kumchagua kiongozi ashike utawala? Na kama viongozi wanajali familia zao na jamaa zao mie mkulima kuna haja gani ya kumpa kura yangu? Na hata kama nikimpa kura yangu na mfumo dhaifu uliopo itafaa nini wakati watawala wanataka kutawala milele na hawataki kukosolewa?

We have lost hope in short sie walalahoi!!!!
 
Ni ushauri tu best, binafsi sitaweza kupiga kura kwakuwa bado niko nje ya nchi na ningependa sana kupiga kura. Ni hivi, Usipopiga kura unaruhusu viongozi WABOVU tulio nao waendelee kuongoza katika ubovu na uovu wao. Best piga kura!
 
Ni ushauri tu best, binafsi sitaweza kupiga kura kwakuwa bado niko nje ya nchi na ningependa sana kupiga kura. Ni hivi, Usipopiga kura unaruhusu viongozi WABOVU tulio nao waendelee kuongoza katika ubovu na uovu wao. Best piga kura!

Mkuu ushauri mzuri, lakini..........
 
SIO UPUUZI
kupiga kura kuna maana kama
mpigaji kura anapata choice ya kuchagua,kama
anaona hakuna right choice,kutopiga kura pia ni aina
nyingine ya kutoa maamuzi.....
kama kuna pepsi na coca unaambiwa uchague,unaweza sema sichagui yeyote..
which is very understandable.......

Wa kumpigia kura mwenyewe ni yupi? Kama huna chaguo ni bora tu kutoshiriki kuliko kupoteza muda wako bure.
 
R.I.P
Hivi Watanzania wote wakishawishika kutokupiga kura, kutakuwa na uchaguzi?

Silaha ya mlalahoi ni kura yake. Akiamua kuitumia vema, akasema, sipigi kura mpaka hiki, na hiki, na hiki, na hiki, kifanyike, je, atakuwa amefanya sahihi ama la? Je, mlalahoi wa Tanzania ana ujasiri huo wa kususia uchaguzi?

./mwana wa haki
 
Back
Top Bottom