Kuna utani unaweza kuvunja ndoa

Kuna utani unaweza kuvunja ndoa

Sio kila anyeposti ana kitambi kama wewe
Hapa kinachotokea ni roho mbaya uchoyo na kukosa adabu Chakula ni mavi tu Badilisha tabia yako
Sawa ila kitambi ni kula kula tu. Hakuna shaka ke hata me vitambi its a result of over feeding aisee. Wenzetu wanapunguza vitambi kwa kupunguza kufakamia
 
Ila unene mwingine si wa kula ni kuridhika jamani....Kuna mtu mnene lkn ukiona anachokula utashangaa kilivyo kidogo....NDIO MAANA ISSA MATONA AKAIMBA : MTU MWENYE TUMBO DOGO KWA KULA HAWEZEKANI...
Wasiokuwa na matumbo ndio walaji wakuu ila miili hairidhiki...

Umenena kweli bhana mtu kuwa bonge sio kwamba ndo anakula sana wengine amani ya nafsi tu inamfanya anenepe
 
Sasa huyo rafiki yako mi nlidhani atafurahi mkewe akisema anaondoka ili ajibebee kipotabo kwa raha zake
 
Dah! hata wangu ni bonge sijawah mtania ila huwa namwabia madhara ya ubonge nikiwa naye tunafanya mazoez ili kupunguza, lazima mtu ajisikie vibaya wengine ni mabonge wa asili hawez pungua hata akiwa na mawazo mia cha msingi ni kupunguza uzito tu!
 
Sasa huyo rafiki yako mi nlidhani atafurahi mkewe akisema anaondoka ili ajibebee kipotabo kwa raha zake
Mabonge watamu wewe, halaf wanaridhika haraka, hawana na makuu ninachowapendea ni wepesi wa kusamehe na kusahau
 
ha ha ha imenichekesha ila sijafurahia kauli ya mshikaji.

Nakumbuka kunajamaa fulani he was school mate alikuwa na uso mwembamba, rangi ya ngozi nyeusi macho nayo ile sehemu nyeupe ya macho nayo yake ni nyeusi nyeusi hivi, macho yametumbukia kwa ndani na hana kidevu na mdomo wake mrefu kiaina..

Yaani ukimwangalia hivi huwezi kurudia lazima ukwepeshe macho na vicheko vikubane...similar to monkey (Mungu anisamehe) jamaa mmoja akamwambia mbona anawaacha ndugu zake wanahangaika huko porini...dah mtiti wa hapo ulikuwa balaa.
 
Mabonge watamu wewe, halaf wanaridhika haraka, hawana na makuu ninachowapendea ni wepesi wa kusamehe na kusahau

Hahahaa....kumbeee ila mi nataka huyo mama H amkazie kabisaa ili atie akili
 
Mi nashauri Jando na Unyago virudishwe kama Jk alivyorudisha Jeshi baada ya F6. Wanandoa wengi hawajakua na hawana uelewa wowote juu ya ndoa na hata heshima kwa jamii. Yani ni weupe kabisa kichwani!!!
Mtu mwenye akili timamu anawezaje kushushia heshima mkewe kiasi hicho? Tena mbele ya mgeni!
Halafu huyo mkewe akijapata rafiki wa kiume anayemkubali alivyo na kumsifia akachepuka mtarudi hapa kutuomba ushauri. Kila mtu hustahili kuthaminiwa na kuheshimiwa...na mwanandoa ndiye mstari wa mwisho kwenye hayo mambo. Sasa mtu ulalala naye na kumhudumia kisha humthamini, akichepuka kwenda kutafuta usichompa utamlaumu nani?


ndo hawa wa miaka 23 wanataka kuoa.. wavulana wanataka kuingia kwenye ndoa
 
Lakini kuna wanawake wanapakia sana jamani khaaa? mtu unanunua chakula ndani cha mwezi, kinakaa wiki na nusu!! huyo ni mke au pipa? halafu anafutuka balaa na magonjwa ya moyo hayoo!!

Hayo masimango sasa mkuu, ulipomuoa hukujua anakula sana? umempenda kubali yote
 
kama ujamalizia hapo..... asingemtania mbele yako? badae labda ila na unakulaje mpaka uvimbe vimbe hovyo......ha ha ha ha yani nimetafakari jamani huyu mnyama anashape mbaya ningejiua loh....... jamaa hakutenda haki kabisa
View attachment 197418View attachment 197420View attachment 197421

Picha iliyopo kichwani mwangu siku zote juu yako Miss Chagga ni kuwa wewe ni kibonge flani hivi.
Yani mwenye minyama ya uzembe
Ama najidanganya?- Usiniambie kuwa wewe ni kimbaumbau.
 
Siyo kwenye ndoa tu mkuu,mi nilikuwa na mwanangu
tukaenda ofisi fulani,sasa wakati nawatambulisha wale wafanyakazi kuwa huyu ni mwanangu.
mmama mmoja akamwambia mwanangu kwamba mimi ndo mchepuko wa baba yako,huku akijua sijawahi kuongea naye chochote.
Kwa kweli nilijisikia vibaya.Hivyo ni muhimu kupima unataka kumtani mtu katika jambo gani na ni mazingira yapi.

kuna uropokaji haufai kabisa aisee ni basi tu watu hutofautiana makuzi waliyopitia zamani kwenye jamii/familia zao.
 
Picha iliyopo kichwani mwangu siku zote juu yako Miss Chagga ni kuwa wewe ni kibonge flani hivi.
Yani mwenye minyama ya uzembe
Ama najidanganya?- Usiniambie kuwa wewe ni kimbaumbau.

Siwezi kuwa kimbau mbau
 
Mshenzi wa tabia huyo Rafiki yako,na hana malezi kwao ivi mkeo unaelalanae na kumka nae na nimama wa mtoto wako unawezaje kumwambia pumba kama hizo? afadhali huyo mwanamke mungu kampa subra mpaka sasa yupo anaimba kuondoka lakini yupo,angenikuta Mtanga mie mbona saahizi ningekua Sahare nakula mihogo kwa uonooo...
 
Hivi nyie wanaume wa dot.com mbona wavivu namna hii?? hata kutafauta chakula cha kula mkeo unalalamika. Huko kwa vibanda hasara vyenu mbona vinakula ka mchwa na hamsemi?? hebu komeni ala!
 
Jana jioni nimemtembelea rafiki yangu mmoja. Huyu jamaa huwa haishi kulalama kuhusu tabia ya ulaji ya mkewe na kujiachia jambo linalofanya avimbiane kuliko kawaida. Sasa wakati tunapiga story, kulikuwa na ka-documentary fulani kwa Tv kanazungumzia maisha ya viboko (Wengi huwaita boko).

Basi jamaa akamuita mkewe kama ana jambo fulani muhimu vile; "We mama H njoo mara moja".

Wife kafika jamaa anamuonesha Tv eti "Si unawaona ndugu zako hao wanavyojiachia hapo." Sokomoko lililoanguka ilibidi niage, jamaa ananimbia hadi sasa ushwari haujarejea. Wife anadai jamaa akaoe hao vipotabo ye aondoke.

Jamani busara zizingatiwe yanapokuja masuala ya mizaha haya.

Ndoa si kufanya mapenzi tu, ni pamoja na kuvumilia mapungufu ya mwenzako na kuepukana na kauli zisizofaa hasa za vijiweni.
 
Back
Top Bottom