Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,733
- 5,490
Jana Lissu na wenzake baada ya kufikishwa kituo cha Polisi Karatu mambo yalikua hivi;
LISSU: Mheshimiwa OCD mmetukamata kwa kosa gani?
OCD: Uchochezi.
LISSU: Lina dhamana au halina dhamana?
OCD: Unajua tatizo lenu Chadema ni kujifanya mnajua sana.
LISSU: Sio kujifanya. Soma sheria ya uchochezi namba 18 sura 455, kiifungu kidogo cha 2. Sheria inasemaje kuhusu kosa la uchochezi? Lina dhamana au halina dhamana?
OCD: Lina dhamana. Lakini leo ni jumapili, itabidi mtoke kesho.
LISSU: Fungua Police General Orders (PGO) ukurasa wa 16. Je inazuia mtu kupewa dhamana kwa sababu ni jumapili?
OCD: Hapana.
LISSU: Sasa hiyo ya kusema tutadhaminiwa kesho umeitoa wapi?
OCD: Unajua Mheshimiwa....
LISSU: Sikiliza bwana mkubwa. Hii PGO ndio muongozo wenu wa kazi kama ilivyo Biblia kwa Wachungaji/Mapadre na Quran tukufu kwa Masheikh. Mnatakiwa muijue vizuri.
OCD: Basi tafuta wadhamini wawili waje kukudhamini utoke.
LISSU: Nitajidhamini mwenyewe.
OCD: Haiwezekani.
LISSU: Fungua PGO ukurasa wa 7 kifungu cha 13 usome kuhusu makosa ambayo mtu anaweza kujidhamini mwenyewe. Na hili lipo. Sio?
OCD: (huku akicheka) sawa bwana, nendeni mrudi kesho saa 4 asubuhi.
Hivyo ndivyo Lissu na viongozi wenzie walivyoachiwa huru jana. Leo wameenda kituoni kuripoti kama OCD alivyoelekeza. Kujua sheria ni jambo muhimu sana. Watu wengi huonewa na kupoteza haki zao kwa kutokujua sheria
LISSU: Mheshimiwa OCD mmetukamata kwa kosa gani?
OCD: Uchochezi.
LISSU: Lina dhamana au halina dhamana?
OCD: Unajua tatizo lenu Chadema ni kujifanya mnajua sana.
LISSU: Sio kujifanya. Soma sheria ya uchochezi namba 18 sura 455, kiifungu kidogo cha 2. Sheria inasemaje kuhusu kosa la uchochezi? Lina dhamana au halina dhamana?
OCD: Lina dhamana. Lakini leo ni jumapili, itabidi mtoke kesho.
LISSU: Fungua Police General Orders (PGO) ukurasa wa 16. Je inazuia mtu kupewa dhamana kwa sababu ni jumapili?
OCD: Hapana.
LISSU: Sasa hiyo ya kusema tutadhaminiwa kesho umeitoa wapi?
OCD: Unajua Mheshimiwa....
LISSU: Sikiliza bwana mkubwa. Hii PGO ndio muongozo wenu wa kazi kama ilivyo Biblia kwa Wachungaji/Mapadre na Quran tukufu kwa Masheikh. Mnatakiwa muijue vizuri.
OCD: Basi tafuta wadhamini wawili waje kukudhamini utoke.
LISSU: Nitajidhamini mwenyewe.
OCD: Haiwezekani.
LISSU: Fungua PGO ukurasa wa 7 kifungu cha 13 usome kuhusu makosa ambayo mtu anaweza kujidhamini mwenyewe. Na hili lipo. Sio?
OCD: (huku akicheka) sawa bwana, nendeni mrudi kesho saa 4 asubuhi.
Hivyo ndivyo Lissu na viongozi wenzie walivyoachiwa huru jana. Leo wameenda kituoni kuripoti kama OCD alivyoelekeza. Kujua sheria ni jambo muhimu sana. Watu wengi huonewa na kupoteza haki zao kwa kutokujua sheria