Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,352
- 9,810
Nawasalimu wakuu wangu,
Kumekuwa na mahusiano ya muda mrefu sana kati ya binadamu na mwezi (moon). Hii imepelekea mpaka baadhi ya dini kuziweka kama alama za utambulisho wake. Pia kumekua na kuhusishwa kwa matukio mengi kati ya binadamu na mwezi.Baadhi yake ni kama ifuatavyo;
Wendawazimu na mwezi (lunatic) -Kumekuwa na mahusiano kati ya uendawazimu na mwezi,hasahasa mwezi uliokomaa (full moon), kutokana na utafiti uliofanywa huko nchi za ulaya,kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wenye magonjwa ya akili pale inapokuwa full moon. Lakini pia vichaa au wenye matatizo wa akili wamekuwa wakorofi zaidi na wagomvi katika kipindi hiki cha full moon kuliko siku zingine zozote! Kuna kuwa na ongezeko la 1.8% la aggressiveness na violence kwa wagonjwa wenye matatizo ya akili .Lakini pia hata huku uswahilini kwetu huwa tunawaona vichaa ambao hawana shida, kuna kipindi wanacharuka kwelikweli na kukimbia hovyo,kurusha mawe na kutukana matusi makubwa..lakini kipindi hiki cha full moon kikipita wanakuwa wastaarabu tena. Pia mwezi huwa unahusishwa na mtu ambae kichwa chake kinarukaruka/fyatu,watu wamekuwa wakiwaita watu hawa "mwezi mchanga".Kuonyesha tena mwezi una mahusiano na watu wa aina hiyo..japo haijawa wazi ni kivipi.
Hedhi/ "kwenda mwezini" (menstruation)- Tukio hili la dada zetu na wapenzi wetu kwenda mwezini linahusishwa na mwezi pia.Haijawa wazi ni kwa sababu gani..lakini hasa nadhani kwa sababu ya mzunguko sawa na ule wa mwezi ambapo na wao wanaona siku zao kipindi hicho. Bado haijajulikana ni wanawake wengi kiasi gani wanaona siku zao mwisho wa mwezi (kipindi cha full moon),lakini sitoshangaa kukuta ni zaidi ya asilimia 60.
Kupotea kwa wingi kwa damu (Blood loss) kipindi cha full moon - Kutokana na tafiti iliyofanywa huko Barcelona Hispania umeonyesha kuwa madaktari wengi wamekuwa wakiogopa kufanya upasuaji kipindi cha full moon kwasababu ya risk kubwa ya watu kufa kutokana na upotevu wa damu kwawingi kipindi cha upasuaji.Hivyo inafikiriwa inawezekana mwezi mkomavu unakuwa na effects kwa watu wanaovuja damu..kitu kinachofanya iwe ngumu kudhibiti utokaji wa damu hiyo..
Ghasia na machafuko (violence/aggressiveness) - Kumekuwa na ghasia na ukorofi mwingi kipindi cha full moon,kipindi hiki watu wengi wanakuwa na mood mbaya na kujisikia hasira kwa vitu vidogo.Afisa wa ngazi ya juu wa Polisi wa mji wa Brighton-UK alitangaza mnamo june 2007 kuwa wanapanga kuwa wanaongeza askari zaidi mitaani kipindi cha full moon kwasababu case za watu kufanya ukorofi na kujeruhiana huwa kunaongezeka kwa idadi kubwa,ambapo alihusisha na full moon. Pia polisi wa mji wa Sussex -UK pia walitangaza kuwepo kwa ongezeko kubwa la ghasia kipindi cha full moon kuliko kipindi kingine chochote.
Lakini pia ,kipindi cha full moon kumekuwa na ongezeko kubwa la vifo,watu kujiua,kulipuka kwa magonjwa ya moyo na magonjwa ya vifafa.Watafiti wamekuwa wakijiuliza kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya mwezi na binadamu..
Ongezeko la wanyama kuwa wakorofi (animal gone wild)-kwa mujibu wa British Medical Journal 2001,waliripoti kuwa kipindi cha full moon kumekuwa na ongezeko la mara mbili la case za wanyama kuwauma binadamu,na wanyama wanakuwa wakorofi tofauti na tabia zao za kawaida..Kuna siri gani kati ya mwezi na binadamu....?
Kumekuwa na mahusiano ya muda mrefu sana kati ya binadamu na mwezi (moon). Hii imepelekea mpaka baadhi ya dini kuziweka kama alama za utambulisho wake. Pia kumekua na kuhusishwa kwa matukio mengi kati ya binadamu na mwezi.Baadhi yake ni kama ifuatavyo;
Wendawazimu na mwezi (lunatic) -Kumekuwa na mahusiano kati ya uendawazimu na mwezi,hasahasa mwezi uliokomaa (full moon), kutokana na utafiti uliofanywa huko nchi za ulaya,kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wenye magonjwa ya akili pale inapokuwa full moon. Lakini pia vichaa au wenye matatizo wa akili wamekuwa wakorofi zaidi na wagomvi katika kipindi hiki cha full moon kuliko siku zingine zozote! Kuna kuwa na ongezeko la 1.8% la aggressiveness na violence kwa wagonjwa wenye matatizo ya akili .Lakini pia hata huku uswahilini kwetu huwa tunawaona vichaa ambao hawana shida, kuna kipindi wanacharuka kwelikweli na kukimbia hovyo,kurusha mawe na kutukana matusi makubwa..lakini kipindi hiki cha full moon kikipita wanakuwa wastaarabu tena. Pia mwezi huwa unahusishwa na mtu ambae kichwa chake kinarukaruka/fyatu,watu wamekuwa wakiwaita watu hawa "mwezi mchanga".Kuonyesha tena mwezi una mahusiano na watu wa aina hiyo..japo haijawa wazi ni kivipi.
Hedhi/ "kwenda mwezini" (menstruation)- Tukio hili la dada zetu na wapenzi wetu kwenda mwezini linahusishwa na mwezi pia.Haijawa wazi ni kwa sababu gani..lakini hasa nadhani kwa sababu ya mzunguko sawa na ule wa mwezi ambapo na wao wanaona siku zao kipindi hicho. Bado haijajulikana ni wanawake wengi kiasi gani wanaona siku zao mwisho wa mwezi (kipindi cha full moon),lakini sitoshangaa kukuta ni zaidi ya asilimia 60.
Kupotea kwa wingi kwa damu (Blood loss) kipindi cha full moon - Kutokana na tafiti iliyofanywa huko Barcelona Hispania umeonyesha kuwa madaktari wengi wamekuwa wakiogopa kufanya upasuaji kipindi cha full moon kwasababu ya risk kubwa ya watu kufa kutokana na upotevu wa damu kwawingi kipindi cha upasuaji.Hivyo inafikiriwa inawezekana mwezi mkomavu unakuwa na effects kwa watu wanaovuja damu..kitu kinachofanya iwe ngumu kudhibiti utokaji wa damu hiyo..
Ghasia na machafuko (violence/aggressiveness) - Kumekuwa na ghasia na ukorofi mwingi kipindi cha full moon,kipindi hiki watu wengi wanakuwa na mood mbaya na kujisikia hasira kwa vitu vidogo.Afisa wa ngazi ya juu wa Polisi wa mji wa Brighton-UK alitangaza mnamo june 2007 kuwa wanapanga kuwa wanaongeza askari zaidi mitaani kipindi cha full moon kwasababu case za watu kufanya ukorofi na kujeruhiana huwa kunaongezeka kwa idadi kubwa,ambapo alihusisha na full moon. Pia polisi wa mji wa Sussex -UK pia walitangaza kuwepo kwa ongezeko kubwa la ghasia kipindi cha full moon kuliko kipindi kingine chochote.
Lakini pia ,kipindi cha full moon kumekuwa na ongezeko kubwa la vifo,watu kujiua,kulipuka kwa magonjwa ya moyo na magonjwa ya vifafa.Watafiti wamekuwa wakijiuliza kuna mahusiano ya moja kwa moja kati ya mwezi na binadamu..
Ongezeko la wanyama kuwa wakorofi (animal gone wild)-kwa mujibu wa British Medical Journal 2001,waliripoti kuwa kipindi cha full moon kumekuwa na ongezeko la mara mbili la case za wanyama kuwauma binadamu,na wanyama wanakuwa wakorofi tofauti na tabia zao za kawaida..Kuna siri gani kati ya mwezi na binadamu....?