Tetesi: Kuna taasisi moja nasikia Mukulu kaamua hakuna kupandishana vyeo na mishahara ubaki huo huo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,464
108,620
Za chini ya Kapeti kutoka katika Taasisi moja ni kwamba kumbe ' Mukulu ' mwenyewe kwanza alitaka mishahara yao ipunguzwe kwakuwa ni mikubwa halafu hata tija yao si kubwa kivile ila watangulizi wake wakamshauri kuwa asifanye hivyo kwani ingeweza kumletea shida kidogo hata yeye kwa ' ustawi ' wake kama ambavyo ilishawahi kutaka kumtokea mtangulizi wake namba mbili ( katikati ya kwa Mwalimu na kwa Warioba ) na akakubali kwa yeye pia kuwapa sharti ( hiyo taasisi ) kuwa kuanzia sasa hakuna ' Watumishi ' wake kupandishwa Vyeo na kwamba ameagiza hata mishahara yao ya sasa ibaki kuwa hii hii kwa muda wa miaka mitano ( 5 ) ijayo ndipo atawafikiria.

Baada ya kulisikia hili binafsi nikafanya ' kajiuchunguzi ' kangu kadogo tu na kuweza kuona dalili za ' kutukuka ' kabisa ya hizo taarifa nilizopewa za chini ya kapeti kwani ni ukweli sasa kuwa hao Watu sasa hivi......

  1. Hawatongozi tena hovyo.
  2. Hawalewi hovyo.
  3. Hawapigi wenzao hovyo kwa jeuri yao ya pesa.
  4. Nyuma walikuwa wakihonga Mipesa ila sasa wanahonga Vijihela tu vya ngama.
  5. Wana adabu zote kwa wanajamii wanaowazunguka.
  6. Wanatulia majumbani mwao sana na wanawaheshimu mno Wake zao kuliko zamani.
  7. Wamekuwa ' wabahili ' sana na wamegeuka kuwa wapangaji ' bajeti ' wazuri mno.
Nichukue tu fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mukulu kwa maamuzi yake haya kwani huku ' mitaani ' tulikuwa tunanyanyasika na ' kukanyagiwa ' mno Mademu kama siyo Wake zetu hali ambayo ilikuwa inatukera hadi sasa tukaanza kuwaza kuwa kwakuwa hatuwawezi kwa Ngumi basi ' tuwaroge ' tu kwa kuwatoa ' mishipa ' au kuwatupia ' majini ' ili tuheshimine vizuri.

Akhsante Mukulu na hii ndiyo Tanzania ya usawa ambayo siku zote sisi tulikuwa tunaitaka. Heko!
 
TRA hahahahahaha.....nawaza tu kwa sauti! Hii ndiyo kada inayoongoza kwa kuhonga Na kupiga watu baa, wale wenye mabakabaka mambo yao yamekuwa safi tu majuzi, kabla ya hapo ilikuwa ni punguzo kwenye maji yetu Yale mazaga zaga ya jikoni na......
 
kama bado unaificha hainamana kuweka hum hum tuweke tarifa ambazo zimekamilika broo
 
Kumbe ndio maana juzi kati kulisikika milipuko toka maeneo ya mjini? Bilashaka ilikuwa ni pale ngome kuu, Upanga...
 
Toa taarifa inayoeleweka vinginevyo ni majungu.

Ukituliza vizuri kabisa akili zako na ukarudia tena kusoma nilichokiandika haraka sana utaweza kuwajua ninawasema akina nani au taasisi ipi ILA kama umetega ' misikio ' yako hiyo mikubwa kama ' mapaja ya tembo ' nikutajie ni akina nani utasubiri mno Mkuu kwani siwezi kuwataja ng'o. Yaani hapo katika namba 1,4 na 7 bado tu umeshindwa kuwajua ni akina nani Mkuu? Kweli akina ' Bashite ' mpo wengi nchini Tanzania hakyanani.
 
kama bado unaificha hainamana kuweka hum hum tuweke tarifa ambazo zimekamilika broo

Unataka niitaje mara ngapi Mkuu? Fuatilia kwa umakini wako wote hivyo Vigezo saba ( 7 ) hapo kisha utawajua au utaijua hiyo taasisi Mkuu. Hapa ni mwendo wa ' mafumbo ' na ukisubiri kutafuniwa kisha Wewe umeze tu utasubiri sana tu.
 
Za chini ya Kapeti kutoka katika Taasisi moja ni kwamba kumbe ' Mukulu ' mwenyewe kwanza alitaka mishahara yao ipunguzwe kwakuwa ni mikubwa halafu hata tija yao si kubwa kivile ila watangulizi wake wakamshauri kuwa asifanye hivyo kwani ingeweza kumletea shida kidogo hata yeye kwa ' ustawi ' wake kama ambavyo ilishawahi kutaka kumtokea mtangulizi wake namba mbili ( katikati ya kwa Mwalimu na kwa Warioba ) na akakubali kwa yeye pia kuwapa sharti ( hiyo taasisi ) kuwa kuanzia sasa hakuna ' Watumishi ' wake kupandishwa Vyeo na kwamba ameagiza hata mishahara yao ya sasa ibaki kuwa hii hii kwa muda wa miaka mitano ( 5 ) ijayo ndipo atawafikiria.

Baada ya kulisikia hili binafsi nikafanya ' kajiuchunguzi ' kangu kadogo tu na kuweza kuona dalili za ' kutukuka ' kabisa ya hizo taarifa nilizopewa za chini ya kapeti kwani ni ukweli sasa kuwa hao Watu sasa hivi......

  1. Hawatongozi tena hovyo.
  2. Hawalewi hovyo.
  3. Hawapigi wenzao hovyo kwa jeuri yao ya pesa.
  4. Nyuma walikuwa wakihonga Mipesa ila sasa wanahonga Vijihela tu vya ngama.
  5. Wana adabu zote kwa wanajamii wanaowazunguka.
  6. Wanatulia majumbani mwao sana na wanawaheshimu mno Wake zao kuliko zamani.
  7. Wamekuwa ' wabahili ' sana na wamegeuka kuwa wapangaji ' bajeti ' wazuri mno.
Nichukue tu fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mukulu kwa maamuzi yake haya kwani huku ' mitaani ' tulikuwa tunanyanyasika na ' kukanyagiwa ' mno Mademu kama siyo Wake zetu hali ambayo ilikuwa inatukera hadi sasa tukaanza kuwaza kuwa kwakuwa hatuwawezi kwa Ngumi basi ' tuwaroge ' tu kwa kuwatoa ' mishipa ' au kuwatupia ' majini ' ili tuheshimine vizuri.

Akhsante Mukulu na hii ndiyo Tanzania ya usawa ambayo siku zote sisi tulikuwa tunaitaka. Heko!
Haya ni majungu tu na si vinginevyo
 
Back
Top Bottom