Kuna mtu wakati wowote mnaweza kusikia kaingia tena katika kashifa nyingine ya rushwa

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Huyu mheshimiwa anaeonekane kupambana kwa hali na mali katika jukumu alilopewa, ukimchunguza utagundua anafanya kazi zaidi kama mtu binafsi na sio msimamizi wa wengine wanaopaswa kufanya kazi aliyoamua kujitwika.

Na wakati huo huo, ama kwa kujua au kutokuja, mtu huyu anajiweka katika mazingira ya kupewa kitu kidogo maana ni yeye sasa ndio anaonekana kageuka kila kitu katika ufanyaji maamuzi.

Kwa mtazamo wangu, mheshimiwa huyu akiendelea hivi, ni swala la muda tu kabla hatujasikia kwa mara nyingine tena kuwa kaingia katika mtego wa rushwa kutokana na yeye kuwaita watu ofisini kwake badala ya kuziachia taasisi zinazohusika huku akijenga mazingira ya yeye kuonekana ndio mwamuzi wa kila kitu.

Inawezekana kabisa anaowatuhumu nao wameshasoma mchezo na soon watamuingiza majaribuni na sijui kama ataweza ishinda nafsi yake.
 
Kipindi tetesi za kusema kua kigamboni imenunuliwa ilikua tukikaa vijiweni tunakubaliana kua Tz imeshauzwa.

Kama una upenyo wa kuchukua rushwa we chukua tu ndiyo maduhuli yako kwenye ile biashara
 
Kabisa huyo jamaa alishawahi kukamatwa kwa kuomba rushwa ya mil 30.

IMG-20160331-WA0004.jpg
 
Back
Top Bottom