mimi situmii Luku natumia mita tu, hayo maluku ni wizi wakuu, kwani bila kuwa na kuanzia na 10000 hupati umeme, lakini mita hata 4000 umeme unao.
wape tu hiyo m1.2,sasa tutafanyajeMie wamekuja nyumbani mafundi wakapachika kiwaya kwenye luku na kumlazimisha h/girl asaini na kupiga picha meta na H/girl eti tumeiba umeme. mimi najiuliza huo waya ameweka nani? anayenunua umeme ni mimi sasa iweje mtu aweke waya ili matumizi yapungue? na kama ni hivyo mbona matumizi hayajapungua wakati natumia pia mkaa na jiko la gasi. halafu wamenidai 1.2 eti nimechezea luku. Mimi naona ni ujanja wanatafuta pesa kwa nguvu. nasema hivi " Mungu wa Mbinguni ameona".
Kwani kwenye kulipa umeme hata wa elfu,hawakati vat na rea?haya endelea kuibiwa, tulikuwa tunatumia meter na kujidai kujiona wajanja, siku tuliletewa bill laki 9 ndio tulipokoma.
luku unanuna umeme hata wa buku, eti unasema luku mpaka elfu10 ndio unakuwa na umeme? acha uwongo
usije kutuletea thread nyingine ya kulalamika, already warned!
Huyu hana hata haja ua kupiga kelele, kwani matatizo ya conversion meter ndiyo hayo, huwa Tanesco hawaji kusoma readings, wanakadilia tu, tena mala nyingi huwa wana underestimate, wanakuletea bill ndogo tofauti na matumizi yako halisi, we unajiona bonge la mjanja!! Sasa balaa watapo kuja kusoma actual readings, ndio pale unapoibuka na kudai unaibiwa kumbe hamna, sasa wanataka pesa yao, mi zamani nilikuwa na tatizo kama hilo, ikabidi nijue matumizi yangu halisi ya mwezi hata wakileta bill ya 20,000 mi nakwenda kulipa 50,000, ilinisaidia sana kwani baada ya kuja kusoma nilikuwa naida tanesco kama laki 190,000/!!!hivyo nilitumia umeme kama miezi 4!kufidia hiyo pesa yangu. Sasa wewe unaletewa bill ya 5000,unacheka tu kwanza hiyo mbona ndogo watu huwa wanaletewa hadi za milioni,!! Kama vipi atumie LUKU tu.Mkuu inaonyesha walikuwa wanakusahau kwenye bill zako za nyuma maana hiyo 5000 haitoshi hata service charge za mwezi. Watakuwa walikuwa hawasomi meter yako. Jaribu kuwaona upate ufafanuzi.
Bill ya umeme ya mwezi wa Kwanza ambayo imekuja mwanzoni mwa mwezi huu wa pili imewaacha watu hoi na nilidhani matumizi ya nyumbani kwangu ndo yamekuwa makubwa na kuanza kuwafokea watoto, kumbe ni kila kona ni kilio, kila mwezi bili yangu ya umeme ilikuwa inarange 5000-5500, LAKINI cha kushangaza bill imekuja 85,600/= nikajaribu kuuliza wenzangu kwa maana ya majiarani wakasema na wao imekuja kubwa sana, mmoja imekuja 94,650/= na mwingine 59,700/-
Huu ni uhuni wa serikali kwa Tanesco, yawezekana pesa ya uchaguzi inatafutwa sana hapa, au, kwa kuwa pesa ya kununulia vifaa vya BVR kits haipo na serikali imefirisika sasa inajaribu kufa na wananchi wake.
Acheni huu mchezo.
Kwani kwenye kulipa umeme hata wa elfu,hawakati vat na rea?