Kuna kila dalili uchaguzi mkuu 2015 hakuna

Kuna kila dalili uchaguzi mkuu 2015 hakuna

robert deusi

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2014
Posts
399
Reaction score
69
Ikiwa tumebakiza takribani miezi 4 kuingia kwenye uchaguzi mkuu. Sioni na siamini kama uchaguzi utafanyika.
Mpaka leo hii NEC aijafikisha hata nusu ya mikoa ya Tanzania bara kwa uandikishaji wa wapiga kura kwenye daftari la kudumu.

Na hapo hapo bado tume pamoja na viongozi wakuu wa serikali wanasema uchaguzi uko pale pale.Kwa mimi naona hili suala aliwezekani hata kidogo.

Iweje tume ambayo imeshindwa kufanya kazi kwa muda wa miaka zaidi ya mitatu alafu kazi ile ile ifanywe kwa miezi minne.

Hili aliwezekani hata kidogo binafsi yangu naona JK na tume yake wamejiandalia muda wa kuendelea kuwa madarakani
Yaleeee ya Nkurunziza yananyemelea Tanzania
.
 
Jk alishakanusha tuhuma za kijiongezea muda. Lubuva anatekeleza tuhuma hizo zionekane za kweli aidha kwa makubaliano ya tume hiyo na serikali au kwa sababu nyingine azijuazo Lubuva. Changamoto ninayoiona ni kuandikisha watu nusu nusu kila mkoa kwa idadi wanayoitaka wao. Hili litakuwa divide ana rule...ngumu kwa ukawa kulikabili. Jambo jingine walisubili mgawanyo wa majimbo 'yao' iliuandikishaji uende kwa 'kasi' ktk mikoa iliyosalia.

Lakini pia sioni ajabu kama leo jk na team yake ya EA wakija na siluhisho la kuongeza muda wa madaraka wa Ngurunziza aliyekiuka katiba...naye si ajabu akataka hivyo.
 
Hivi wewe nani kakuambia kuwa kama tusipojiandikisha hakuna uchaguzi, na unadhani huyo JK anaondoka madarakani kwa ridhaa yake ama ni katiba ndo inamuondoa madarakani..........

hili suala la kusema kuwa uchaguzi haupo siyo sifa na ni hatari kulidikilizisha masikioni mwa watu..........

halaf mnapolisemasema hivi mnampa kichwa huyo JK kwani anaons kumbe hats anaweza kupindusha sheria.............

hebu tuachane na hoja za kitoto tuwaze kams nchi na si kumuwaza mtu, tujadili masuala mapana ya taifa na tudijadili hisia zq watu, sisi tuendelee kujadili ni kwa jinsi gani tutajipanga kupiga ama kupigiwa kura huku tukiamini hii siyo nchi ya JK ama ccm kwa wao kufanya wanavyotaka............

ka nchi kama burundi tuu limewashinda ndo itakuwa kwa Jk.?............
 
Katika watu wenye upeo mdogo unaweza kuwa kiranja wao pole sana.
 
yatatokea ya ngurunzinza hapa wasifanye mchezo
 
Watu wengine sijui wanawaza nini Taifa linaongozwa na katiba halafu mtu mwingine anakuja na mawazo yake mepesi tu ambayo hayana maana.

mambo kama haya ya kufikirika ni vema ukawa unazungumza na watoto wenzako kwenye viwanja vya michezo.
 
Mods ondoeni huu uchafu,mtu akiishiwa cha kupost kinachofuata ni kuandika uharo,nan kakuambia uchaguzi utaahirishwa?na alivyokuambia ulishindwa kuchanganya na zako?ptuuuuu,rais wetu sio mlafi wa madaraka kama mbowe.
 
Ikiwa tumebakiza takribani miezi 4 kuingia kwenye uchaguzi mkuu. Sioni na siamini kama uchaguzi utafanyika.
Mpaka leo hii nec aijafikisha hata nusu ya mikoa ya tanzania bara kwa uandikishaji wa wapiga kura kwenye daftari la kudumu
Na hapo hapo bado tume pamoja na viongozi wakuu wa serikali wanasema uchaguzi uko pale pale.kwa mimi naona hili suala aliwezekani hata kidogo.
Iweje tume ambayo imeshindwa kufanya kazi kwa muda wa miaka zaidi ya mitatu alafu kazi ile ile ifanywe kwa miezi minne
Hili aliwezekani hata kidogo binafsi yangu naona jk na tume yake wamejiandalia muda wa kuendelea kuwa madarakani
Yaleeee ya nkurunziza yananyemelea tanzania
Uchaguzi upo hamasisheni watu wajiandae mtapigwa bao dakika za majeruhi halafu mseme mmeibiwa kura kumbe mliandaa watu kufanya fujo uchaguzi ukiahirishwa badala kuandaa watu kupiga kura
 
Watu wengine sijui wanawaza nini Taifa linaongozwa na katiba halafu mtu mwingine anakuja na mawazo yake mepesi tu ambayo hayana maana.

mambo kama haya ya kufikirika ni vema ukawa unazungumza na watoto wenzako kwenye viwanja vya michezo.

unganisha hayo ya mawazo mepesi ya kufikirika na hali halisi iliyopo
 
Back
Top Bottom