Kuna haja gani ya kuzika watu?

Nebuchadinezzer

JF-Expert Member
Oct 1, 2018
1,403
2,545
Asalaam Walekum? Bwana Yesu apewe sifa? Mapendo? Mungu ni mwema? Maranatha? Natumaini kila mmoja wetu ni mzima wa afya? Kama sivyo, Mungu awafanyie wepesi mliowagonjwa na mlio katika shida mbalimbali.

Leo sina mengi sana ila naleta kwenu hoja yangu kama kichwa kinavyojieleza hapo juu.

Tangu nilipokuwa mtoto mpaka leo hii mimi ni mtu mzima ninayeweza kutengeneza watoto nimekua nikishuhudia mtu akifa anazikwa, wanaenda kumfukia chini ya ardhi, juu ya ile aridhi wanatengeneza kama msingi hivi na kuweka marumaru (vigae) halafu wanachomeka na msalaba wa mbao au wa chuma.

Badae nimekua na kwenda shule ambako nimefundishwa kutumia akili ya kiutafiti na kuhoji. Leo nimekaa zangu hapa nakula matunda akili ikanambia hakuna umuhimu wa kuzika.

Mimi naona kutokana na uhaba wa aridhi ni vizuri badala ya watu kuzikwa basi wakifa wachomwe moto tu. Wawe majivu halafu tuyamwage baharini au mashambani ili viumbe hai wengine kama mahindi wanufaike . Na pia tulio hai tufurahie maisha.

Mimi nadhani wafu wanachukua ardhi kubwa mno halafu hata hawaiendelezi. Zaidi ya hapo wanakua wanatutisha tu hata kupita maeneo yao usiku tunaogopa.

Halafu naamini wafu wakianza kuchomwa hata hizi imani zingine za kijinga kijinga za kuamini waliokufa na kuanza kuwajali na wakati kipindi wapo wazima tulikuwa tunawachukia zitaisha.

Si busara walio hai wakakosa ardhi halafu wafu wapewe.

Ni hayo tu jamani. Sina mengi leo. Mungu awabariki sana.

Hoja haipigwi rungu.
 
Binadamu ni tofauti na viumbe wengine anahitaji kuthaminiwa na kuheshimika akiwa mzima na akifa.

Ardhi ndogo ukiwa wapi? Bado tuna ardhi ya kutosha kwa shughuli zote. Kuchoma moto hata mataifa makubwa yenye idadi kubwa bado hawafanyi.

Acha roho mbaya ili ufikiri mema zaidi
 
Binadamu ni tofauti na viumbe wengine anahitaji kuthaminiwa na kuheshimika akiwa mzima na akifa.

Ardhi ndogo ukiwa wapi? Bado tuna ardhi ya kutosha kwa shughuli zote. Kuchoma moto hata mataifa makubwa yenye idadi kubwa bado hawafanyi.

Acha roho mbaya ili ufikiri mema zaidi
Sina roho mbaya mkuu hii ni hoja tu.

Halafu mbona India wao wanachoma moto? Au kwa kua sisi bado hatujawa wengi kama wao?
 
ushawahi kujiuliza mabilioni ya watu waliowahi kuishi mika ya nyuma makaburi yao yapo wapi,
 
Wafu wanakula sana ardhi bila faida yoyote!

Mtu akishakufa ndio mwisho wa habari. Tuache kuwapamba pamba wafu kwa marumaru na kupoteza cement nyingi ardhini.

Kuwachoma moto wafu ni faida kubwa kwa wanaobaki!
Na mimi mawazo yangu ni hayo hayo mkuu...unakuta nyumba ya familia ya marehemu haina sakafu ya simenti lakini kaburi la baba wa familia lina marumaru.
 
ushawahi kujiuliza mabilioni ya wstu waliowahi kuishi mika ya nyuma makaburi yao yapo wapi,
Watu wazikwe sustainably ili wadecompose kwa wiki mbili hadi mwezi mmoja tu hakuna cha dawa za kuhifadhi na majeneza wa mwendo wa sanda au any easly decomposable materials
 
Asalaam Walekum? Bwana Yesu apewe sifa? Mapendo? Mungu ni mwema? Maranatha? Natumaini kila mmoja wetu ni mzima wa afya? Kama sivyo, Mungu awafanyie wepesi mliowagonjwa na mlio katika shida mbalimbali.

Leo sina mengi sana ila naleta kwenu hoja yangu kama kichwa kinavyojieleza hapo juu.

Tangu nilipokuwa mtoto mpaka leo hii mimi ni mtu mzima ninayeweza kutengeneza watoto nimekua nikishuhudia mtu akifa anazikwa, wanaenda kumfukia chini ya ardhi, juu ya ile aridhi wanatengeneza kama msingi hivi na kuweka marumaru (vigae) halafu wanachomeka na msalaba wa mbao au wa chuma.

Badae nimekua na kwenda shule ambako nimefundishwa kutumia akili ya kiutafiti na kuhoji. Leo nimekaa zangu hapa nakula matunda akili ikanambia hakuna umuhimu wa kuzika.

Mi naona kutokana na uhaba wa aridhii ni vizuri badala ya watu kuzikwa basi wakifa aachomwe moto tu. Wawe majivu halafu tuyamwage baharini au mashambani ili viumbe hai wengine kama mahindi wanufaike . Na pia tulio hai tufurahie maisha.

Mi nadhani wafu wanachukua aridhi kubwa mno halafu hata hawaiendelezi. Zaidi ya hapo wanakua wanatutisha tu hata kupita maeneo yao usiku tunaogopa.

Halafu naamini wafu wakianza kuchomwa hata hizi imani zingine za kijinga kijinga za kuamini waliokufa na kuanza kuwajali na wakati kipindi wapo wazima tulikuwa tunawachukia zitsisha.

Si busara walio hai wakakosa aridhi halafu wafu wapewe.

Ni hayo tu jamani. Sina mengi leo. Mungu awabariki sana.

Hoja haipigwi rungu.
Ni wapi ardhi imekosekana?
Nchi kama Tanzania hatujakalia hata robo ya ardhi yetu sasa sijui wapi imekosekana
 
Ardhi iliyotumika kuwahifadhi wafu haifiki hata theluthi ya ardhi waliyokuwa wakiimiliki na sasa wametuachia.
 
Ni wapi ardhi imekosekana?
Nchi kama Tanzania hatujakalia hata robo ya ardhi yetu sasa sijui wapi imekosekana
Mara nyingi maeneo ya makaburi yako mijini au sehemu zenye mikusanyiko ya watu.

Ardhi kubwa ambayo haijatumika ni ya vijijini ambako watu ni wachache. Na huko huwezi kukuta makaburi yaliyokula nafasi kubwa kama makaburi ya mijini.

Ardhi za mijini zinaliwa na wafu hectors kwa hectors. Makaburi yamejipanga kweli kweli ukitizama ni misalaba tu huoni hata inapoishia.

Watu wanataka ardhi wajenge majumba, mabarabara, mahospitali na mashule!

Hapo dar es salaam itafika muda mtazika wafu juu ya makaburi ya wafu wengine.
 
Mara nyingi maeneo ya makaburi yako mijini au sehemu zenye mikusanyiko ya watu.

Ardhi kubwa ambayo haijatumika ni ya vijijini ambako watu ni wachache. Na huko huwezi kukuta makaburi yaliyokula nafasi kubwa kama makaburi ya mijini.

Ardhi za mijini zinaliwa na wafu hectors kwa hectors. Makaburi yamejipanga kweli kweli ukitizama ni misalaba tu huoni hata inapoishia.

Watu wanataka ardhi wajenge majumba, mabarabara, mahospitali na mashule!

Hapo dar es salaam itafika muda mtazika wafu juu ya makaburi ya wafu wengine.
Kabisa mkuu...hii ipo town hasa hasa
 
we mzee unaejiita mtu mzima sasa,sio tu kwamba umewaza hayo uliyaandika. Wewe umeona kwa wahindi halafu umependa na unataka uige. Sasa kama hujui kuzika kuna faida kubwa kwa ustawi wa viumbe kuliko kuchoma maiti.
 
we mzee unaejiita mtu mzima sasa,sio tu kwamba umewaza hayo uliyaandika. Wewe umeona kwa wahindi halafu umependa na unataka uige. Sasa kama hujui kuzika kuna faida kubwa kwa ustawi wa viumbe kuliko kuchoma maiti.
Nipe hizo faida mkuu
 
Ni wapi ardhi imekosekana?
Nchi kama Tanzania hatujakalia hata robo ya ardhi yetu sasa sijui wapi imekosekana
Makaburi yakinondoni na yale ya pale malapa yamechukua sehemu kubwa kiasi kwamba hata viwanda vingekaa pale vingeweza kuzalisha product zenye kuinufaisha nchi yetu pomoja na kuajiri vijana.

Lakini vijana wako mtaani hawana ajira kwasababu ardhi yenye kuwafanya waajiriwe inamilikiwa na wafu waliokufa miaka kenda huko...
 
Back
Top Bottom