byakunu
JF-Expert Member
- Sep 13, 2016
- 511
- 1,140
Wadau wenye magari habari zenu, heri ya xmass na mwaka mpya.
Naomba kushea na ninyi jambo lililonikuta katika pitapita zangu katika magereji mbali mbali hapa Dar es salaam.
Nilikuwa na gari yangu iligongwa na bajaji nikapeleka sehemu X kurekebisha katika maeneo ya magomeni, fundi akaniambia kazi hiyo itachukua takriban siku mbili. (Kunyoosha, kupaka rangi na kupiga polish) maana gari iliumia kidogo kwenye bonet, na ilipinda kwenye mwamba wa mbele (toyota ist) sasa hawa jamaa kumbe ukiwaachia gari yako wanafanya kazi ulio wapa na wanafanya kazi ya kufungua exhaust na kukata catalytic convertor wenyewe wanaita vibuyu wanatoa unga mweupe upo mle ndani na madini ya platinum aisee hii kitu inasemekana dili sana na wanauza dakika hiyo hiyo baada ya kukata that means kuna mteja anakua anasubiri kuchukua huo unga.
Gari nyingi sana zimekatwa na wanavyo kata kitaalam huwezi jua kama gari yako imekatwa kwani wanakata kwa juu ili sehem iliyo katwa ijifiche kwenye bodi (Ntawatumia picha)
Mimi baada ya gari yangu kukaa siku mbili huko kwa fundi nikaenda kuchukua wakati naondoka tu nilinotice mlio wa engine kuwa umebadilika nikaenda mpaka temeke nikasimama garage nyingine nikaita fundi mwingine anisaidie kujua shida iko wapi ukizingatia gari iligongwa kwa mbele nika assume huenda kuna shida ilikua katika engine ambayo sikuijua, basi nikamwelezea mazingira yote yule fundi na akaniuliza gari umekaa siku ngapi uliko peleka nikamwambia siku mbili bas akawa kama ameshapata majibu basi akachukua gari aiendeshe na kusikia kelele iko vipi, aliporudi akasema bas tukaikague ebwaneee si ndo akalala chni na kuniita tukakuta exhaust limekatwa limechomelewa kwa juu, nilimind kinoma na nilitukana matusi yote, palepale nililazimika kwenda kituo cha polisi kuwashtaki jamaa nilio wapa gari wanyooshe na kupiga rangi, na hapo ilikuwa saa mbili usiku, kesho yake asubuh na mapema nikaenda kituon kuchukua askari na kwenda pale walipo jamaa nikamwita fundi njoo nchekie gari naskia inashida bado akaja bila kujua nimeweka mtego (hapo askari wapo ndani ya gari) nikawa naongea na fundi taratib nasogea nae kwenye gari,askari akachomoka fasta akamtia kabali jamaa na kumtupia kwenye gari jamaa alitetemeka akapanic mpaka kujikojolea akaambiwa amwite na mwenzake nae akaja wakakamatwa wote, kwenda kituoni wakaenda kunyea debe na wametoka kwa dhamana, kazi wanayofanya saizi wanatembea kama machinga kunitafutia exhaust mpya ya ku replace kwenye gari yangu ndo tuachane salama. Kituon wanatakiwa kuripoti jumatatu kwa mujibu wa taratibu.
Sasa basi nyie watu Naomba kuwashauri mambo ya kuzingatia katika gari yako pale unapotaka kwenda garage.
1. Kwanza kabisa Ikague gari yako kama bado haijachezewa mchezo huu huko kipindi cha nyuma kabla hujaskia au kusoma uzi huu
2. Ukipeleka gari kwa fundi usikubali gari ilale kwake au uiache kwa masaa kadhaa bila kuwepo
3.Ukimkabidh fundi bas mwambie kabisa baba hii gari exhaust yangu haijawah guswa ikibidi muoneshe kabisa na mchimbe mkwara mzito incase ukikuta imekatwa basi ni yeye utaruka nae kwanza.
4.Msinunue magari ya mkononi kwa mtu bila kukagua mambo kama haya
5. Kuwa na garage yako permanent unapo servicia gari yako usihame hame garage. Wakikuchezea mchezo huu ukaja kustuka badae hutojua ni nani kafanya
6.Kama hujapata tatizo kubwa katika gari yako usipeleke garage ita fundi nyumbani kwako atengenezee hapo.
7. Ijue gari yako vizuri sana hasa mlio wa engine ya gari yako wakati wote, sio kuendesha tu gari.
8. Usiazimishe ovyo gari yako kwa kila mtu unae mjua
Magari mengi sana yamesha katwa bila wamiliki kujua kama yamekatwa nashauri watu tutajahidi sana kuyajua magari yetu vzuri na tusipende kuazimisha gari maana wakienda kukata hizo mambo ni hela ya fasta wanapata na kazi haichukui mda mrefu ni kukata kuunga na kufunga angalia link hii wanavyofanya
Naomba kushea na ninyi jambo lililonikuta katika pitapita zangu katika magereji mbali mbali hapa Dar es salaam.
Nilikuwa na gari yangu iligongwa na bajaji nikapeleka sehemu X kurekebisha katika maeneo ya magomeni, fundi akaniambia kazi hiyo itachukua takriban siku mbili. (Kunyoosha, kupaka rangi na kupiga polish) maana gari iliumia kidogo kwenye bonet, na ilipinda kwenye mwamba wa mbele (toyota ist) sasa hawa jamaa kumbe ukiwaachia gari yako wanafanya kazi ulio wapa na wanafanya kazi ya kufungua exhaust na kukata catalytic convertor wenyewe wanaita vibuyu wanatoa unga mweupe upo mle ndani na madini ya platinum aisee hii kitu inasemekana dili sana na wanauza dakika hiyo hiyo baada ya kukata that means kuna mteja anakua anasubiri kuchukua huo unga.
Gari nyingi sana zimekatwa na wanavyo kata kitaalam huwezi jua kama gari yako imekatwa kwani wanakata kwa juu ili sehem iliyo katwa ijifiche kwenye bodi (Ntawatumia picha)
Mimi baada ya gari yangu kukaa siku mbili huko kwa fundi nikaenda kuchukua wakati naondoka tu nilinotice mlio wa engine kuwa umebadilika nikaenda mpaka temeke nikasimama garage nyingine nikaita fundi mwingine anisaidie kujua shida iko wapi ukizingatia gari iligongwa kwa mbele nika assume huenda kuna shida ilikua katika engine ambayo sikuijua, basi nikamwelezea mazingira yote yule fundi na akaniuliza gari umekaa siku ngapi uliko peleka nikamwambia siku mbili bas akawa kama ameshapata majibu basi akachukua gari aiendeshe na kusikia kelele iko vipi, aliporudi akasema bas tukaikague ebwaneee si ndo akalala chni na kuniita tukakuta exhaust limekatwa limechomelewa kwa juu, nilimind kinoma na nilitukana matusi yote, palepale nililazimika kwenda kituo cha polisi kuwashtaki jamaa nilio wapa gari wanyooshe na kupiga rangi, na hapo ilikuwa saa mbili usiku, kesho yake asubuh na mapema nikaenda kituon kuchukua askari na kwenda pale walipo jamaa nikamwita fundi njoo nchekie gari naskia inashida bado akaja bila kujua nimeweka mtego (hapo askari wapo ndani ya gari) nikawa naongea na fundi taratib nasogea nae kwenye gari,askari akachomoka fasta akamtia kabali jamaa na kumtupia kwenye gari jamaa alitetemeka akapanic mpaka kujikojolea akaambiwa amwite na mwenzake nae akaja wakakamatwa wote, kwenda kituoni wakaenda kunyea debe na wametoka kwa dhamana, kazi wanayofanya saizi wanatembea kama machinga kunitafutia exhaust mpya ya ku replace kwenye gari yangu ndo tuachane salama. Kituon wanatakiwa kuripoti jumatatu kwa mujibu wa taratibu.
Sasa basi nyie watu Naomba kuwashauri mambo ya kuzingatia katika gari yako pale unapotaka kwenda garage.
1. Kwanza kabisa Ikague gari yako kama bado haijachezewa mchezo huu huko kipindi cha nyuma kabla hujaskia au kusoma uzi huu
2. Ukipeleka gari kwa fundi usikubali gari ilale kwake au uiache kwa masaa kadhaa bila kuwepo
3.Ukimkabidh fundi bas mwambie kabisa baba hii gari exhaust yangu haijawah guswa ikibidi muoneshe kabisa na mchimbe mkwara mzito incase ukikuta imekatwa basi ni yeye utaruka nae kwanza.
4.Msinunue magari ya mkononi kwa mtu bila kukagua mambo kama haya
5. Kuwa na garage yako permanent unapo servicia gari yako usihame hame garage. Wakikuchezea mchezo huu ukaja kustuka badae hutojua ni nani kafanya
6.Kama hujapata tatizo kubwa katika gari yako usipeleke garage ita fundi nyumbani kwako atengenezee hapo.
7. Ijue gari yako vizuri sana hasa mlio wa engine ya gari yako wakati wote, sio kuendesha tu gari.
8. Usiazimishe ovyo gari yako kwa kila mtu unae mjua
Magari mengi sana yamesha katwa bila wamiliki kujua kama yamekatwa nashauri watu tutajahidi sana kuyajua magari yetu vzuri na tusipende kuazimisha gari maana wakienda kukata hizo mambo ni hela ya fasta wanapata na kazi haichukui mda mrefu ni kukata kuunga na kufunga angalia link hii wanavyofanya