Kumekucha: Kampuni za simu kuanza kuuza hisa Tanzania

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Hivi karibuni tumesikia taarifa kwamba makampuni ya siku yataorodhesha hisa zake katika Soko la Hisa la Dar es Salaam na ningependa tuangalie aina hii ya uwekezaji. Tumesikia pia kwamba Klabu ya Simba itafanya marekebisho ya Katiba iwe Kampuni na kuanza kuuza hisa mashabiki.

Tufahamu kwanza Hisa ni nini? Hisa ni sehemu ya mtaji wa kampuni inayomilikiwa na wanahisa. Makampuni hugawanya mitaji yao katika vipande yenye thamani sawa ambapo kila kipande huitwa hisa na huuzwa kwa thamani fulani.

Mtu yeyote mwenye umri kuanzia miaka 18 anaweza kununua Hisa. Wazazi au walezi pia wanaweza kununua hisa kwa niaba ya watoto wao. Unaweza kununua kiasi chochote cha hisa kulingana na uwezo wako kifedha. Unaweza kununua kuanzia hisa 100 na kuendelea.

Mfano: Kama kampuni ina hisa 500,000 na mwekezaji anamiliki hisa 50,000, mwekezaji huyu anamiliki 5% ya kampuni hiyo.

Hizi ni baadhi ya Sifa za Hisa

• Hisa zina thamani

• Hisa zinaweza kukua au kupungua thamani

• Hisa ndio huunda mtaji wa kampuni

• Hisa zinaweza kufa pindi kampuni inapofilisika

• Hisa inamilikiwa kisheria kama sehemu ya mali anayoweza kuwa nayo mtu yeyote kihalali.

• Unaponunua hisa unakuwa na haki ya umiliki katika kampuni.

Nakaribisha maoni, unaionaje aina hii ya uwekezaji?
 
Mmmh siku zote walikuwa wapi, hawa wanataka tununue hisa ili tuwasaidie kupiga kelele kuhusu makodi, imekula kwao
 
Ni mwanzo mzuri, Makampuni ya simu yanaingiza faida. Ni vipi tutajua kwamba hesabu wanazoweka ni sahihi? Kumekuwa na kesi za Makampuni kufake mahesabu ili wasitoe gawio kubwa.
 
Mkuu una habari kama tayari wametoa Company prospectus?
Mkuu Prospectus waliyoitoa haina fund's strategies, fee structure wala financials statements ila kuna orodha ya brokers na authorized agents na Licensed Investment Advisors

Fununu nyingine ni kwamba share moja itakuwa kati ya 600 - 900 TZS.
 
Watanzania Kea kina hatujapewa darasa la kina ktk masuala ya hisa. Hisa ni nzur sana ila panatakiwa ELIMU sana.
 
Mkuu Prospectus waliyoitoa haina fund's strategies, fee structure wala financials statements ila kuna orodha ya brokers na authorized agents na Licensed Investment Advisors

Fununu nyingine ni kwamba share moja itakuwa kati ya 600 - 900 TZS.

Nashukuru mkuu at least kwa kunipa mwanga kuhusu bei ya hisa inayotegemewa.

Wakati huu ni mgumu sana, sijui kama watapatikana watu wengi wa kununua hizo hisa!
 
Nashukuru mkuu at least kwa kunipa mwanga kuhusu bei ya hisa inayotegemewa.

Wakati huu ni mgumu sana, sijui kama watapatikana watu wengi wa kununua hizo hisa!

Tusubiri tuone, nina imani watapatikana considering Makampuni ya simu yamekuwa yakiingiza faida kubwa kwakweli.
 
Mkuu Prospectus waliyoitoa haina fund's strategies, fee structure wala financials statements ila kuna orodha ya brokers na authorized agents na Licensed Investment Advisors

Fununu nyingine ni kwamba share moja itakuwa kati ya 600 - 900 TZS.
Hivi nitakua nimekosea au maana nafaham walishapeleka prospectus kwa CMSA sasa haijapitishwa ili iwe published??? Maana tunasubiri kwa hamu opportunity hii
 
Nunueni hisa za TTCL najua zitakua bei ndogo sana lakin future yake ipo so bright. Si umeskia lile la kuhamia mtandao bila kubadilisha namba.
 
Back
Top Bottom