Banxbanxson
Senior Member
- Oct 19, 2016
- 125
- 167
Habari ndugu na Jamaa,
Napenda kushare kwa wanajamii forums jinsi ya kunisaidia kusahau au kupata relief ya kumbukumbu ya rafiki yangu..
Hatukusoma pamoja shule ya msingi ingawaje tulitoka kijiji kimoja. Tulibahatika kwenda shule moja ya sekondari wakati huo. Tukawa marafiki wa kushibana kwa kila hali ingawaje sote tulitoka katika familia zenye dhiki. Maisha yetu yalitegemeana na kushare kidogo tulichoweza kupata kwa kufanya vibarua siku za weekend. Napenda kukiri kwamba tuliishi zaidi ya ndugu.
Baada ya kumaliza kidato cha nne Mm nilifanikiwa kuendelea na masomo ya sekondari na yeye alibahatika kujiunga na mafunzo ya jeshi la polisi na hatimae kuajiriwa. Wakati naingia chuo tayari alikuwa ameshapata ajira. Hakika alinisaidia masula yangu kadhaa wakati nikiwa chuoni.
Baada ya kumaliza chuo niliingia kupambana mtaani kutafuta ajira. Alinitia moyo na kunisapport kwa namna alivyoweza. Kwa waliotufahamu ukubwani walijua sisi ni ndugu wa kuzaliwa kwa kuwa mama yake alikuwa mama yangu pia.
Ghafla mwaka 2021 ndiyo kwanza nimepata ajira katika taasisi fulani na kuanza kufurahia maisha pamoja na ndugu yangu tukiwa na matumaini na malengo ya kufanya mambo mengi kwa pamoja, Nikapokea taarifa za kifo chake huko Dodoma bila ya kuugua. Hakuwahi kuwa na tatizo la shinikizo la damu ambalo kutokana na ripoti ya kitabibu ndiyo chanzo cha kifo chake.
Nikiri kuwa nimefiwa na watu wengi ikiwemo wazazi wangu na watu wengine wa karibu lakini kwa ndugu yangu huyu ni miaka zaidi 4 nimeshindwa kabisa kuamini au kukubali kuwa amefariki. Nimekuwa nikimuwaza kupita kiasi, ninaota tukiwa tunapiga stori mara kadhaa. Kuna wakati nikiwa nimekaa mwenye nashika simu yangu kwa lengo la kumpigia tuongee kisha nakumbuka kuwa hayupo duniani..
Hakika machungu ya kumpoteza Cheed bado yamejaa ndani ya kifua kwa kipindi chote hiki.
Labda ndugu na jamaa kutoka hapa kundini mnaweza kuwa na ushauri bora namna ya kuondokana na hili.
Hakika maisha bila ya kuwepo kwake yamenifanya kuwa mpweke sana licha ya kuwa nina Familia na watu wengine wanaonizunguka..
Mungu Ailaze mahali salama rafiki yangu Rashid.
Ahsante
Napenda kushare kwa wanajamii forums jinsi ya kunisaidia kusahau au kupata relief ya kumbukumbu ya rafiki yangu..
Hatukusoma pamoja shule ya msingi ingawaje tulitoka kijiji kimoja. Tulibahatika kwenda shule moja ya sekondari wakati huo. Tukawa marafiki wa kushibana kwa kila hali ingawaje sote tulitoka katika familia zenye dhiki. Maisha yetu yalitegemeana na kushare kidogo tulichoweza kupata kwa kufanya vibarua siku za weekend. Napenda kukiri kwamba tuliishi zaidi ya ndugu.
Baada ya kumaliza kidato cha nne Mm nilifanikiwa kuendelea na masomo ya sekondari na yeye alibahatika kujiunga na mafunzo ya jeshi la polisi na hatimae kuajiriwa. Wakati naingia chuo tayari alikuwa ameshapata ajira. Hakika alinisaidia masula yangu kadhaa wakati nikiwa chuoni.
Baada ya kumaliza chuo niliingia kupambana mtaani kutafuta ajira. Alinitia moyo na kunisapport kwa namna alivyoweza. Kwa waliotufahamu ukubwani walijua sisi ni ndugu wa kuzaliwa kwa kuwa mama yake alikuwa mama yangu pia.
Ghafla mwaka 2021 ndiyo kwanza nimepata ajira katika taasisi fulani na kuanza kufurahia maisha pamoja na ndugu yangu tukiwa na matumaini na malengo ya kufanya mambo mengi kwa pamoja, Nikapokea taarifa za kifo chake huko Dodoma bila ya kuugua. Hakuwahi kuwa na tatizo la shinikizo la damu ambalo kutokana na ripoti ya kitabibu ndiyo chanzo cha kifo chake.
Nikiri kuwa nimefiwa na watu wengi ikiwemo wazazi wangu na watu wengine wa karibu lakini kwa ndugu yangu huyu ni miaka zaidi 4 nimeshindwa kabisa kuamini au kukubali kuwa amefariki. Nimekuwa nikimuwaza kupita kiasi, ninaota tukiwa tunapiga stori mara kadhaa. Kuna wakati nikiwa nimekaa mwenye nashika simu yangu kwa lengo la kumpigia tuongee kisha nakumbuka kuwa hayupo duniani..
Hakika machungu ya kumpoteza Cheed bado yamejaa ndani ya kifua kwa kipindi chote hiki.
Labda ndugu na jamaa kutoka hapa kundini mnaweza kuwa na ushauri bora namna ya kuondokana na hili.
Hakika maisha bila ya kuwepo kwake yamenifanya kuwa mpweke sana licha ya kuwa nina Familia na watu wengine wanaonizunguka..
Mungu Ailaze mahali salama rafiki yangu Rashid.
Ahsante