Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,908
- 30,249
Sheikh Ilunga akiendesha darsa Thakafa Mwanza 2010
Nilikuwapo siku ya kwanza katika mhadhara wake wa mwanzo mjini Tanga na alikuwa anazungumza baada ya Sala ya Isha.
Ghafla baada ya Sala ya Isha nikiwa ndani naona watu wakiingia kwa wingi haukupita muda msikiti ule mdogo ukawa umejaa pomoni na watu wengine wamejazana nje ya msikiti hadi barabarani wengine wanachungulia madirishani.
Ikabidi Sheikh Ilunga aombwe asubiri kuanza kuzungumza ili kuwapa nafasi Waislam wanaotoka misikiti ya mbali wafike na ikabidi ziwekwe taa za kutosha nje ya msikiti.
Waislam walikuwa wanampenda Sheikh Ilunga na wanaelewa ujumbe aliokuwa anawafikishia.
Mwaka wa wa 2011 nilikuwa Geneva Switzerland kijana mmoja akanialika nyumbani kwake.
Kijana huyu baada ya kusalimiana na kutulia akaniuliza endapo kama namjua Sheikh Ilunga.
Akanyanyuka alipokaa akaweka DVD ya Iliunga na kuniomba nimwangalie.
Nimeweka picha ya Geneva ya jioni ile.
Picha ya tatu inaonyesha sura ya Sheikh Ilunga katika screen ya TV na mimi nikiwa pembeni.
Hii ni picha nilipiga nyumbani kwa kijana yule siku ile nikiwa mbali sana na Tanzania.
Nilimuomba mwenyeji wa anipige picha ili nichukue kumbukumbuka ya Sheikh Ilunga nikiwa Geneva.
Wakati ule sikujua kama nitakuja kuikumbuka picha hii na nitaiweka kama kumbukumbu baada ya kifo chake.
Sheikh Ilunga