Zitto Kabwe
Kwa Madiba " waliomwita gaidi leo wanamlilia. Waliomwita mkombozi wanamlilia. Aliunganisha maadui na marafiki" maneno yangu ya utangulizi Leo Bungeni. Naongeza....
Wakati anaanza mazungumzo ya siri na makaburu, wenzake ndani ya ANC walimwita msaliti (a compromised sell out). Leo hawathubutu maana Taifa lao, licha ya changamoto, ni moja ya mataifa bora Afrika.
Uthubutu wake ulidhihirisha ambayo wengi hawakuyaona. Uvumilivu, kusamehe na kusonga mbele ni tunu adimu alizokuwa nazo Madiba. Hamba kahle, Tata!