Jimjuls
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 484
- 161
Ni miezi iliyopita tu wataalamu kutoka mamlaka hali ya hewa walitutahadharisha kwamba kutakuwapo na mvua nyingi mno hivyo tujihadhari.Shirika la Umeme Tz wakaanza pia kazi yao ya kubadilisha zile nguzo mbovu za umeme kuepusha madhara zaidi kutokana na taarifa hizo.Hivi majuzi wakasema kwamba mvua zilizotarajiwa hazitakuwa nyingi tena.Hii imesaidia kwani hata huku mtaani kwetu walibadilisha nguzo ambayo ilikuwa haifai(imeoza) kwani tulikuwa tunapiga kelele kila siku lakini jamaa wakawa wanajidai hawsikii.Walau huu utabiri umewafanya kuikumbuka hii nguzo yetu na kuibadilisha!