share
JF-Expert Member
- Nov 22, 2008
- 6,062
- 10,461
Serikali imejidadavua kuwa imenunua ndege sita kwa fedha taslimu (cash) na kwamba Watanzania tutembee vifua wazi. We are donor country!!!!. Tunajiuliza, fedha hiyo imetoka wapi wakati makusanyo (revenue) yetu ni wastani wa trioni 13 kwa mwaka!! Asimilia zaidi ya 60 ya mapato hayo huenda kwenye matumizi ya kawaida ya serikali (recurrent expenditure). Sasa hizi za kununulia ndege (development expenditure) tena nje ya bajeti iliyopitishwa na bunge imetoka wapi? Tukiangalia deni la taifa, limepaa sana hadi kufikia trioni 61!!!!! Hivyo, hii tutakosea kutafsiri kuwa tulikopa fedha ili kununua, pamoja na mambo mengine, ndege kwa fedha taslimu (cash) ?!?!