Kumbe bungeni wapo wapo walale wasilale sawa

onjwayo

JF-Expert Member
Apr 8, 2020
1,346
1,303
Nimejisikia vibaya baada ya spika Ndugai kuwauliza wabunge kuwa ni lini walipitisha Sheria mbaya na kandamizi ya kutaifisha mifugo pale wanapoingia katika hifadhi. "Hivi hii Sheria ilipitishwa Lini..tulikuwa tumesinzia au ilipitishwa wakati sipo".

Jamani nchi hii Kuna baadhi ya watu wametumia vibaya madaraka yao kuwaumiza wenzao. Eti mifugo ikikanyaga tu kwenye hifadhi inataifishwa na kupigwa Bei! Kama aliyekuwepo na mtu anayesimamia na kuona Sheria zenye manufaa zinajadiliwa na kupiitishwa ndio anaanza kujishangaa, Sasa sisi wananchi tufanye lipi.

Kumbe mle bungeni wapo tu kwa kivuli Cha CCM na hakuna lolote linalofanyika. Kujishangaa ni dalili za wehu. Pesa zetu zinaliwa bure na watu wasio na hili Wala lile.

Hata hivyo ukiwa mtenda maovu siku ukianza kujitambua kuwa unayoyatenda siyo sahihi ujue God anakuhitaji ili akuhifadhi. Katiba mpya inahitajika Sana ili tusiweze kujishangaa.
 
ndungai amebadilika siku hizi, yaonekana anatumia uweredi kidogo sio kaa wakati wa jiwe, hata nafikiria hii swala la wale covid 19 viti maalum ako na baraka zote za bibi mkubwa na ndio hajachukua hatua yeyote licha ya kuwa wako mbungeni kinyume na katiba
 
Supika nadhani anawaonea! Wao wangefanyaje wakati kazi yao nikupiga madawati kumpongeza Mwendazake?
 
Wale jamaa wanaosafirisha ng'ombe ukiwauliza umebeba mzigo gani wanasemaje wamebeba wabunge.
Kazi ya mifugo hiyo nikugonga bodi bila sababu sawa na hao wabunge wanavyogonga meza. Aliye wafananisha ng'ombe na wabunge atafutweeeeee
 
Nani Alikuwa Spika
Wabunge hawakusema NDIOOO
Walijua ndiooo nizanini
Tunaelekea kubaya sana
 
Lakini na huko kwenye hifadhi wafugaji wanafuata nini? Hao wafugaji mbona wanatetewa sana,ugomvi na wakulima ni wao,hifadhini ni wao tena,kupitisha mifugo kwenye barabara ni wao tena.Kuitaifisha ni lugha nzuri na laini sana.....dunia yote tunataka wanyama wengine wasiishi?

Sheria ikiwekwa tuitii hata kama ni ya kuuliwa ilimradi iwe ya manufaa kwa binadamu wengine pamoja na viumbe hai vingine na hata vitu visivyo hai.
 
Ndugai huyo mwenye kirapa ndio anazinduka
E2crFWzWQAQ3bBp.jpg
 
Nimejisikia vibaya baada ya spika Ndugai kuwauliza wabunge kuwa ni lini walipitisha Sheria mbaya na kandamizi ya kutaifisha mifugo pale wanapoingia katika hifadhi. "Hivi hii Sheria ilipitishwa Lini..tulikuwa tumesinzia au ilipitishwa wakati sipo".

Jamani nchi hii Kuna baadhi ya watu wametumia vibaya madaraka yao kuwaumiza wenzao. Eti mifugo ikikanyaga tu kwenye hifadhi inataifishwa na kupigwa Bei! Kama aliyekuwepo na mtu anayesimamia na kuona Sheria zenye manufaa zinajadiliwa na kupiitishwa ndio anaanza kujishangaa, Sasa sisi wananchi tufanye lipi.

Kumbe mle bungeni wapo tu kwa kivuli Cha CCM na hakuna lolote linalofanyika. Kujishangaa ni dalili za wehu. Pesa zetu zinaliwa bure na watu wasio na hili Wala lile.

Hata hivyo ukiwa mtenda maovu siku ukianza kujitambua kuwa unayoyatenda siyo sahihi ujue God anakuhitaji ili akuhifadhi. Katiba mpya inahitajika Sana ili tusiweze kujishangaa.
Prof Asad ,wakati ule aliwaambia Bunge Ni dhaifu
 
Back
Top Bottom