Kulinganisha gharama za tofali

Kulinganisha gharama za tofali

Tofali za kununuw shida n kwamba mchanga unakua
Mwingi kuliko cement

Triple A
Tofali nzuri zinajulikana. Uliza wanaojua wakusaidie wapi utapata tofali nzuri kwenye eneo lako.
 
Unazungumzia Dar ama mkoani?
Kama mkoani labda utanishawishi...

Ulitumia siku ngapi na hiyo mashine ukalipa 50,000 tu?
Je ni mashine ya mkono au vibrated?
Na je, kama ni mkono uimara wa tofali una uhakika nao kiasi gani?tu
Unaposema maji bure ulikuwa unachota mtoni? Na je mchotaji ni huyo huyo fundi au we mwnyewe?

Hakuna kisicho na gharama Boss.
Muda uliopoteza kusimamia unaweza kadiria Tsh ngapi?
Kwa Dar es salaam kufyatua tofali mwenyewe inaweza kuwa ni gharama kubwa kuliko haya ya kununua.
Binafsi nimefanya option zote hizi. Ila sitathubutu kufyatua mwenyewe tena. Maana ni presha na hasara sana nilipata
Mapendo.

Mkuu gharama zinategemea mahali ulipo. Mimi nilikuwa najenga fensi ambayo ilihitaji matofari elfu kumi kwa hiyo kila tofari elfu moja nilihitaji milion 10.
Nikampata wapiga tofari na kunishauri kununua mifuko 250@sh 12000 jumla milion tatu usafiri wa simenti 200,000/=.
Kupiga tofari kila mfuko elfu 4 jumla 1,000,000/=
Kusomba mchanga nilitumia trekta langu mafuta na dreva 150,000/. kumwagilia nilikuwa natumia kisima changu tank moja hutumia unit tatu na niliweka umeme wa 30,000/. wamwagiliaji 50,000/jumla 4,430,000/

 
Mkuu gharama zinategemea mahali ulipo. Mimi nilikuwa najenga fensi ambayo ilihitaji matofari elfu kumi kwa hiyo kila tofari elfu moja nilihitaji milion 10.
Nikampata wapiga tofari na kunishauri kununua mifuko 250@sh 12000 jumla milion tatu usafiri wa simenti 200,000/=.
Kupiga tofari kila mfuko elfu 4 jumla 1,000,000/=
Kusomba mchanga nilitumia trekta langu mafuta na dreva 150,000/. kumwagilia nilikuwa natumia kisima changu tank moja hutumia unit tatu na niliweka umeme wa 30,000/. wamwagiliaji 50,000/jumla 4,430,000/
Hapo naona ulisave sana mkuu, vp ubora wa tofari zako.
 
Nakupa gharama zangu, nimefyatua tofali 2400.
Kukodi mashine 50000/=
Fundi kila tofali kufyatua ni tsh. 150/=(tulivyoelewana) jumla ni 360,000/=
Mifuko ya cement ilikuwa 71 jumla yake 923000/=
Usafiri mifuko ya cement sh.50,000/=
Mchanga Lorry 8 kubwa jumla sh, 420,000/=
Gharama ya maji ilikuwa bure.
gharama zote ni kama sh.1,803,000/=

Kama ningeamua kununua moja moja, tofali 2400.
Kila tofali linauzwa sh.1000, hivyo jumla ingekuwa 2,400,000/=
Kubeba na kushusha kila tofali ni sh.200/= ingekuwa jumla ni 480,000/=
Usafiri wa tofali zote trip kama 8 hivi kila trip sh.50,000/= ingekuwa 400,000/=
Jumla gharama zote kununua ingekuwa 3,280,000/=

Hivyo kwa ujenzi wangu niliokoa kama kiasi cha sh.1,477,000/=Hela ya fundi kunijengea boma

Conclusion: gharama hizi inategemea location, ulinzi nk. piga mwenyewe hesabu lakini kufyatua mwenyewe ni nafuu, kwa vile unaponunua, hata anayekuuzia gharama zake ameingiza humo kwenye bei yake.
Upo Sawa ila kwa huku kwetu ni 1200 hadi site......Kupiga Mwenyewe ni nafuhu ila changamoto ipo kwenye Maji kuyamwagilia na mafundi kuchanganya vizuri na kuyakandamiza vizuri na machine Ile manual.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo naona ulisave sana mkuu, vp ubora wa tofari zako.
Kwa ujumla nilisevu zaidi ya nusu na nilitumia karibu milion nane kumaliza kabisa ujenzi wa fensi . Matofari ni bora sana unajua haya matofari ya kununua hayana simenti nyingi ila yanakandamizwa zaidi.
 
Kwa ujumla nilisevu zaidi ya nusu na nilitumia karibu milion nane kumaliza kabisa ujenzi wa fensi . Matofari ni bora sana unajua haya matofari ya kununua hayana simenti nyingi ila yanakandamizwa zaidi.
Umezungumza suala la Msingi sana mkuu!

Tofali hata ukandamize vipi kama imepelea sementi na maji basi hesabia maumivu tuu
 
Mimi kuna mtu eti alinishauri wakati wa kupaua nikanunue miti halafu nipasue mbao eti garama itapungua, mpaka leo sitaki kumuona machoni mwangu!

Hahahahahhaaa umenifanya nicheke kwanguvu bila kutarajia hahahahahaa polee.
 
Ukipata site yenye mchanga hapohapo ni bora kufyatua mwenyewe,lile shimo LA mchanga unatengeneza LA choo.
 
Kwa ujumla nilisevu zaidi ya nusu na nilitumia karibu milion nane kumaliza kabisa ujenzi wa fensi . Matofari ni bora sana unajua haya matofari ya kununua hayana simenti nyingi ila yanakandamizwa zaidi.
Asante mkuu, nitalifanyia kazi mkuu.
 
Naomba kuchomekea swali dogo, hivi kujenga kwa Block (za cement+mchanga) na kwa kutumia tofali za kuchoma Ni zipi imara kwa ujenzi.Zipi zenye maisha marefu? Kama unanunua zote zipi ambazo Ni rahisi (cheap). Samahani kwa kuingilia mada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kuchomekea swali dogo, hivi kujenga kwa Block (za cement+mchanga) na kwa kutumia tofali za kuchoma Ni zipi imara kwa ujenzi.Zipi zenye maisha marefu? Kama unanunua zote zipi ambazo Ni rahisi (cheap). Samahani kwa kuingilia mada

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha Kuchomekea Kwenye Post Za Wenzako, Anzisha Ya Kwako Utapata Majibu Ya Kutosha Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom