SILENT ACtOR
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 627
- 181
Ni wazi sasa ni suala la muda tu kabla ya ccm kuondoka madarakani na nafasi yake kuchukuliwa na chama mbadala chenye nguvu, na hapa tz ni Chadema. Kuchukua uongozi (mamlaka) ni jambo moja na uongozi uliotukuka ni jambo jingine. Ndiyo maana nawaomba chadema wajifunze namna wazambia walivyoamua kuzuia uuzwaji wa madini yao nje ya nchi mpaka sheria mpya ya madini ipitishwe. Hii ni kutokana na tuhuma za kuuza madini bila kufuata taratibu kunakofanywa na wafanyabiashara na hivyo kuikosesha mapato serikali (source BBC). Hapa kwetu imeshindikana, hivyo chadema mmeona inawezekana, Zambia wameweza nasi tunaweza na madini ni mfano mmoja tu.