Kulikoni Power Breakfast ya Clouds FM?

Kulikoni Power Breakfast ya Clouds FM?

mafutamingi

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
2,775
Reaction score
2,198
Mimi ni mpenzi mkubwa wa kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa kila siku asubuhi na Clounds FM. Sijui kimetokea nini siku za hivi karibuni kwa kuwa magwiji wa kipindi hiki wakiwemo Fetty, Caesar chini ya kiongozi Masoud Kipanya siwasikii tena.

Nasikia sauti za watangazaji wengine ambao wanapwaya sina na kufanya kipindi kikose ladha. Je Masoud na wenzie wamekwenda wapi? Kama wamepelekwa vitengo vingine namsihi Boss Kussaga awarudishe haraka maana kipindi pendwa kinakufa.
 
Mimi ni mpenzi mkubwa wa kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa kila siku asubuhi na Clounds FM. Sijui kimetoke nini siku za hivi karibuni kwa kuwa magwiji wa kipindi hiki wakiwemo Fetty, Caesar chini ya kiongozi Masoud Kipanya siwasikii tena. Nasikia sauti za watangazaji wengine amabo wanapwaya sina na kufanya kipindi kikose ladha. Je Masoud na wenzie wamekwenda wapi? Kama wamepelekwa vitengo vingine namsihi Boss Kussaga awarudishe haraka maana kipindi pendwa kinakufa.
Wamepigwa ban mkuu wote hao watatu na serikali.

Na sio hao tu hata Maulid kitenge hayupo n.k
 
Wamepigwa ban mkuu wote hao watatu na serikali.

Na sio hao tu hata Maulid kitenge hayupo n.k
Sasa hao Clouds wangekuwa wanawaita hao wakina Kipanya na wenzake waliopigwa ban kama wageni waalikwa na wachambuzi sio watangazaji kipindi kinaenda ,wanakuwa wanachambua na kuhoji wageni aaah aaah akili akili akili alafu wanawapiga posho
 
Mimi ni mpenzi mkubwa wa kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa kila siku asubuhi na Clounds FM. Sijui kimetokea nini siku za hivi karibuni kwa kuwa magwiji wa kipindi hiki wakiwemo Fetty, Caesar chini ya kiongozi Masoud Kipanya siwasikii tena.

Nasikia sauti za watangazaji wengine ambao wanapwaya sina na kufanya kipindi kikose ladha. Je Masoud na wenzie wamekwenda wapi? Kama wamepelekwa vitengo vingine namsihi Boss Kussaga awarudishe haraka maana kipindi pendwa kinakufa.
Farhan ni kijana ambaye anaianza career yake. Bado anahofu nyingi sana kwa future yake. Ni kijana mchapakazi na mwenye bidii ya kujifunza mengi sana. Tumpe muda.

Philip Mwihava anatakiwa kupewa mic, anaweza kuwa sub sahihi
 
Wako VETA mkuu
Screenshot_20250314-075844.jpg
 
Wamepigwa ban mkuu wote hao watatu na serikali.

Na sio hao tu hata Maulid kitenge hayupo n.k
Duh, nashindwa kuelewa ukweli ni upi maana majibu yanatofautiana - mara wamepigwa ban, mara hawana vyeti n.k. Kwa maoni yangu sababu zote hizo hazina mashiko. Kama ni suala la vyeti basi itakuwa sababu dhaifu sana. Waajiri wengi sikuu hizi ni kuwa na uwezo(skills) katika kazi fulani na siyo vyeti. Masoud na wenzie walikuwa na vipaji vikubwa katika fani ya utangazaji. Ukiangalia hata kwenye mainstream media za kimataifa utakuta baadhi ya watangazaji kama Anderson Coooper au Piers Morgan wa CNN, wote hawa hawakasomea journalism. Lakini ni magwiji wa utangazaji huko waliko. Hapa nyumbani mchukue mtu kama Jenerali Ulimwengu. Hajasomea uandishi wa habari lakini anaheshimika katika hiyo fani hapa nyumbani na kimataifa.

Kama wamepigwa spana kwa namna ambavyo walikuwa wanahoji uozo uliopo basi hili litakuwa linasikitisha. Je serikali inataka vyombo vya habari navyo viwe vinasifia tu. Kazi ya kusifia tuwaachie TBC, na magazeti ya Mzalendo, Uhuru na Habari leo.
 
Back
Top Bottom