godson Lomayani
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 538
- 711
Kwa kweli nimecheka sana huu mpambano wa boxing mizunguko mitatu kati ya Floyd Mayweather Jr na Tenshin Nasukawa, dogo huyu kutoka Tokyo Japan, aliingia ulingoni kwa mbwembwe akijiamini kupita kiasi kuking'oa kisiki kukata ngebe za Mayweather.
Lakini haikuwa rahisi kama alivyofikiri mzunguko wa kwanza unaanza baada ya kutambulishwa dogo alianza kwa kujihami na kuwa makini na ngumi za Mayweather zinazotoka kwa kasi kubwa.
Dogo alijitutumua akafanikiwa kumpiga mpinzani wake ngumi moja usoni lakini Mayweather hakujali akawa anacheza pambano lile kimasikhara! alikuwa anapiga ngumi kama hataki vile na zisizokuwa na kasi kama ilivyo kawaida yake, Nasukawa akapata imani anang'oa mwamba ulioshindikana ghafla kibano kikamgeukia alipigwa combination zilizomfanya alambe sakafu mara ya kwanza alihesabiwa na kuamka faster! na kusema yuko timamu kuendelea.
Game liliendelea alijaribu kujibu mapigo lakini alidhibitiwa na Floyd ambaye alimpeleka kwenye angle na kumpiga ya chembe na kumalizia na uppercut iliyompeleka chini dogo kwa mara nyingine, Mayweather alirudi kwenye angle yake na kuanza kucheza rhumba. Dogo alihesabiwa kama kawaida alinyanyuka faster na kusema anaendelea lakini sura ikionyesha dhahiri amepata maumivu makali
Mzunguko wa mwisho Floyd aliamua kummaliza kabisa dogo Tenshin Nasukawa kwa kumpiga konde zito kichwani lililomlambisha sakafu kwa mara nyingine, dogo alihesabiwa kila akijaribu kunyanyuka alikuwa akipepesuka na kwenda chini. Team Nasukawa ilibidi warushe taulo kumusuru kijana wao aliyekuwa akilia kutokana na kisago cha nguvu.
Huku akiendelea kububujikwa na machozi Floyd alikwenda kumpongeza na kumnyanyua mkono wake juu kuashiria kwamba dogo ni mshindi huo ndio ukawa mwisho wa mpambano, lakini niconclude kwa kusema sometimes too much confidence zinaweza kukufanya ushindwe kama ilivyotokea kwa bondia huyu kutoka Japan alijiamini kupita kiasi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini haikuwa rahisi kama alivyofikiri mzunguko wa kwanza unaanza baada ya kutambulishwa dogo alianza kwa kujihami na kuwa makini na ngumi za Mayweather zinazotoka kwa kasi kubwa.
Dogo alijitutumua akafanikiwa kumpiga mpinzani wake ngumi moja usoni lakini Mayweather hakujali akawa anacheza pambano lile kimasikhara! alikuwa anapiga ngumi kama hataki vile na zisizokuwa na kasi kama ilivyo kawaida yake, Nasukawa akapata imani anang'oa mwamba ulioshindikana ghafla kibano kikamgeukia alipigwa combination zilizomfanya alambe sakafu mara ya kwanza alihesabiwa na kuamka faster! na kusema yuko timamu kuendelea.
Game liliendelea alijaribu kujibu mapigo lakini alidhibitiwa na Floyd ambaye alimpeleka kwenye angle na kumpiga ya chembe na kumalizia na uppercut iliyompeleka chini dogo kwa mara nyingine, Mayweather alirudi kwenye angle yake na kuanza kucheza rhumba. Dogo alihesabiwa kama kawaida alinyanyuka faster na kusema anaendelea lakini sura ikionyesha dhahiri amepata maumivu makali
Mzunguko wa mwisho Floyd aliamua kummaliza kabisa dogo Tenshin Nasukawa kwa kumpiga konde zito kichwani lililomlambisha sakafu kwa mara nyingine, dogo alihesabiwa kila akijaribu kunyanyuka alikuwa akipepesuka na kwenda chini. Team Nasukawa ilibidi warushe taulo kumusuru kijana wao aliyekuwa akilia kutokana na kisago cha nguvu.
Huku akiendelea kububujikwa na machozi Floyd alikwenda kumpongeza na kumnyanyua mkono wake juu kuashiria kwamba dogo ni mshindi huo ndio ukawa mwisho wa mpambano, lakini niconclude kwa kusema sometimes too much confidence zinaweza kukufanya ushindwe kama ilivyotokea kwa bondia huyu kutoka Japan alijiamini kupita kiasi.
Sent using Jamii Forums mobile app