WanaJF habari za ninyi. Ninaamini kwa wengi wetu sikukuu zilikuwa mswano tu, full bataaz na mambao kama hayo. Kwa wale ambao mambo yalikuwa arijojo, napenda kuchukua fursa hii kuwafikishia pole za dhati kutoka kunako mtimani.
Turudi kwenye mada sasa. Imezoeleka katika jamii zetu za kitanzania kwa mtu mwenye mtoto/watoto kuitwa kwa kutumia jina la mtoto wake. Utasikia mama Semeniiiii, njoo huku muuza mboga anataka kuondoka, hapo snowhite anaitiwa mchicha au mama Dullah mwanao anatuletea usiku, sisi tunakuheshimu ila akizidisha kuna siku tutamtia ndimu ujue, huyu ni Kongosho mwenye mtoto mtukutu haswaa. Kwa upande wa wanaume hali ni hiyo hiyo. James anakuwa Baba V, watu8 anakuwa baba Magimbi, basi alimradi kila mtu aitwa kwa jina la mtotowe.
Tabia hii ipo hata kwa wanandoa wenyewe. Unakuta mtu kaoa basi mkewe akishatotoa tu, jina la mke linakufa na tangia hapo anakuwa mama fulani, na yeye pia hataki kusikia anaitwa jina lake isipokuwa baba fulani tu!!!. Tena wengine utasikia akiulizwa wewe iina lako nani mwenzetu, naitwa mama Ana au naitwa baba Mwaipenye, na ukisisitizia jina, mtu hataki kabisa anakwambia we niite hivyo hivyo tu.
Tuje kwenye hoja sasa. Japokuwa si jambo baya kutumia huu utaratibu lakini mimi naona kama unawanyanyapaa sana wale wasio na watoto, hususan wale wanaohitaji watoto lakini hawakujaaliwa kuwa nao. Fikiria kila wakisikia mama/baba fulani huko mitaani wanapata mawazo kiasi gani? Nadhani imefika mahali tuache huu utaratibu kwa sababu unawaumiza sana wenzetu ambao hawajajaaliwa. Wengi humu tunajua kuwa ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu kukosa mtoto linaangaliwa kama tatizo kubwa. Inabidi ifike mahali tutambue kuwa watoto ni majaaliwa tu kutoka kwa muumba. Yaani saa nyingine unakuta watu tunajisiiifu kwa kuwa na watoto kama vile kuna chochote kikubwa tumefanya zaidi ya ngono. Kabla sijapaluliwa naomba niseme kuwa natambua malezi ni kazi ya ziada, kwa hiyo hongera zao wote waliokuza.
Turudi kwenye mada sasa. Imezoeleka katika jamii zetu za kitanzania kwa mtu mwenye mtoto/watoto kuitwa kwa kutumia jina la mtoto wake. Utasikia mama Semeniiiii, njoo huku muuza mboga anataka kuondoka, hapo snowhite anaitiwa mchicha au mama Dullah mwanao anatuletea usiku, sisi tunakuheshimu ila akizidisha kuna siku tutamtia ndimu ujue, huyu ni Kongosho mwenye mtoto mtukutu haswaa. Kwa upande wa wanaume hali ni hiyo hiyo. James anakuwa Baba V, watu8 anakuwa baba Magimbi, basi alimradi kila mtu aitwa kwa jina la mtotowe.
Tabia hii ipo hata kwa wanandoa wenyewe. Unakuta mtu kaoa basi mkewe akishatotoa tu, jina la mke linakufa na tangia hapo anakuwa mama fulani, na yeye pia hataki kusikia anaitwa jina lake isipokuwa baba fulani tu!!!. Tena wengine utasikia akiulizwa wewe iina lako nani mwenzetu, naitwa mama Ana au naitwa baba Mwaipenye, na ukisisitizia jina, mtu hataki kabisa anakwambia we niite hivyo hivyo tu.
Tuje kwenye hoja sasa. Japokuwa si jambo baya kutumia huu utaratibu lakini mimi naona kama unawanyanyapaa sana wale wasio na watoto, hususan wale wanaohitaji watoto lakini hawakujaaliwa kuwa nao. Fikiria kila wakisikia mama/baba fulani huko mitaani wanapata mawazo kiasi gani? Nadhani imefika mahali tuache huu utaratibu kwa sababu unawaumiza sana wenzetu ambao hawajajaaliwa. Wengi humu tunajua kuwa ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu kukosa mtoto linaangaliwa kama tatizo kubwa. Inabidi ifike mahali tutambue kuwa watoto ni majaaliwa tu kutoka kwa muumba. Yaani saa nyingine unakuta watu tunajisiiifu kwa kuwa na watoto kama vile kuna chochote kikubwa tumefanya zaidi ya ngono. Kabla sijapaluliwa naomba niseme kuwa natambua malezi ni kazi ya ziada, kwa hiyo hongera zao wote waliokuza.
Last edited by a moderator: