Kuhusu vyeti

Kuhusu vyeti

chapashoka

Member
Joined
Mar 9, 2017
Posts
19
Reaction score
5
Ndugu habari zenu, naomba anayefahamu anisaidie ,Nina wadogo zangu wawili mapacha walimaliza kidato cha nne mwaka 2015 ,kulingana na hali yangu ya kipato kuwa ngumu sikuweza kumaliza kulipa ada yao ,hivo wanadaiwa deni kubwa hapo shuleni na hadi sasa hawana vyeti vyao vilibaki hadi watakapomaliza ada. Mwaka huu nilihitaji waende chuo na sina pesa ya kulipia hiyo ada wanayodaiwa isipokuwa Nina ada wanayotakiwa kulipa chuo. Je niki apply vyuo kwa kutumia result slip wataweza kuchaguliwa vyuoni? Au njia ipi watu wanatumia kama hawana pesa ya kulipia?
 
vyuo vya level ipi ?ya elimu..??
kama ni veta nadhani si lazima
 
Kuhusu application NACTE hawahitaji vyeti,cha msingi ni index no.
ila chuo atakakoripoti ndipo watamwomba cheti. Ila kwa direct applications vyuoni hapo ni heri uwalipe wakupe vyeti
 
Pia nilihitaji ikiwezekana zikitoka nafasi za jeshi kwa kujitolea mmoja nimuombee maana kuna mmoja anatamani kwenda huko
 
Komboa vyeti mkuu ni muhimu sana, ada utapata tena bado sana chuo mpaka September utakutwa umepata pesa nyingine.
 
Back
Top Bottom