Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Naomba, kwa niaba ya wazalendo wenzangu wa Isansa Mbozi nitoe ufafanuzi kuhusu na kilichoandikwa na gazeti la NIPASHE la leo tarehe 14 January 2019, kwenye kichwa cha habari _"Bil 13.9 kukarabati Bombadier Canada"_
Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandidi Isack Kamwele , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege
Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini
Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani
Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili
Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu
Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service
Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,
Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo
Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_
Ni kwamba tarehe 10 mwezi huu, mh waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandidi Isack Kamwele , alialikwa kama mgeni rasmi katika chuo cha usafirishaji( NIT) katika uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege
Katika hotuba yake, alieleza changamoto katika sekta hii ya usafiri wa anga hapa nchini, mojawapo ya changamoto aliosema, ni ukosefu wa karakana( Hanga) za kukarabati ndege zenye ubora na ukubwa wa kutosha hapa nchini
Hivyo akasema kwa mfano mwakani wanapaswa kupeleka ndege zetu 2 za bombadier kwa ajili ya kuzifanyia service( Schedule service), kwa kawaida kila ndege ina muda wake maalumu wa kufanyiwa service kutokana na flying hours, ambapo kwa bombadier Q 400 hufanyiwa service kila baada ya masaa( Flying hours) 600 ya kuwa angani
Na akasema, kama watapeleka ndege hizo nchini Canada kwa ajili ya service itawagharimu serikali takribani $ 3m kwa ndege moja na $ 6m kwa ndege zote mbili
Lakini akasema, baada ya kuambiwa hilo, alimfuata mh Rais na kumuomba apewe fedha kwa ajili ya ukarabati wa hanga yetu, iliyopo katika uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro( KIA) ambapo kimsingi ombi lake lilikubaliwa na mh Rais, na serikali wameshaanza ukarabati mkubwa katika hanga hiyo na pia wameshaingia mikataba 3, ikiwemo ya kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya ukarabati wa ndege zetu
Na yote hii, inafanyika ili tuweze kuokoa fedha nyingi za kupeleka ndege Canada kwa ajili ya service
Binafsi kama mzalendo nitoe wito, hasa kwa vyombo vya hsbari kama magazeti, kujiepusha kuwa na vichwa vya habari vyenye kuweza kupotosha umma,
Nadhani kwa hili la NIPASHE, nina imani mamlaka husika zitachukua hatua stahiki juu ya jambo hilo
Mzalendo
_Ngamanya Kitangalala_